Augustine Mrema apitishwa tena na TLP kugombea ubunge Vunjo

Mwenyekiti wa chama cha TLP bwana Augustine Lyatonga Mrema ametangaza kuendelea kukitetea kiti chake cha ubunge katika jimbo lake la Vunjo kwa tiketi ya chama chake.



TLP imepitisha au amejipitisha kugombea Ubunge Vunjo? Naomba mnijuze wadau. Nijuavyo mimi, Mrema hana uwezo kwa sasa kushinda ubunge jimbo la Vunjo, nashauri apumzike asije kufa haraka kwa pressure za kampeni!
 
Mrema alipendwa sana Vunjo lakini sasa ni zamu ya ukawa (james Mbatia). Nimeshafanya utafiti.
 
Amepitishwa ama amejipitisha kuweka jina na picha kwenye orodha ya wagombea?Sidhani kama wanavunjo wanautayari wakurudia makosa.
 
Hivi Mrema ni msomali au mchagga.....??? Hebu tujuzeni ili tufanye maamuzi sahihi ikifika oktoba
 
Mzee Mrema najua huwa husomi jf lakini hata akitokea mtu anayemfaham akisoma, mwambie wengi humu wamemshauri ajilambie kiinua mgongo chake na akaangalie zile ng'ombe zake kule Kahe na kajumba kake pale Kiraracha.
Atakuwa ameifanyia haki nafsi yake aache kung'ang'ania madaraka. Huu si wakati wake tena meshafanya mengi mazuri abaki na sifa hiyo na kiinua mgongo.
Lakini akikaidi, angojee aibu ya mwaka
 
hata actccm ikusaidie ukawa tunabebe we unatak ufie bungeni
 
Umri si kigezo cha mtu kutokuwa Mbunge. Wa Nigeria wamemchagua rais wao Ana miaka 73, kwa wenyewe wajinga hawakuwaona hao Vijana. Mrema Jembe hizo porojo nyingine Kuhusu afya Yake ni chuki binafsi Za watu. Kwani Kwenye familia yako hakuna mgonjwa. He ww ni Mzima unaweza ukafa Na ukamuacha yeye.
 
Mrema atakuwa mbunge Vunjo mpaka atakapoamua mwenyewe. Sisi wenyeji wa jimbo hili tulimpigia kura mwaka 2010.Mpinzani wake ni CCM. Anayebisha aweke kura za pamoja za Chadema, NCCR na CUF uchaguzi uliopita jimboni hapa. Kumshinda Mrema Vunjo mpaka UKAWA wachanganye na CCM which is impossible. Hakuna kilichobadilika.Mrema ni mbunge anayengoja kuapishwa.Tutampigia kura tena Oktoba. Tembeleeni Vunjo huwezi ku describe alivyo na support kubwa.
 
Mrema atakuwa mbunge Vunjo mpaka atakapoamua mwenyewe. Sisi wenyeji wa jimbo hili tulimpigia kura mwaka 2010.Mpinzani wake ni CCM. Anayebisha aweke kura za pamoja za Chadema, NCCR na CUF uchaguzi uliopita jimboni hapa. Kumshinda Mrema Vunjo mpaka UKAWA wachanganye na CCM which is impossible. Hakuna kilichobadilika.Mrema ni mbunge anayengoja kuapishwa.Tutampigia kura tena Oktoba. Tembeleeni Vunjo huwezi ku describe alivyo na support kubwa.

Nakupa big up kwa analysis ya kweli uliyotoa: hapa watu wana coment tu kuhusu jimbo au mtu, wakati hawajawahi kufika jimboni humo na kuangalia hali ya kisiasa ilivyo:
 
Nakupa big up kwa analysis ya kweli uliyotoa: hapa watu wana coment tu kuhusu jimbo au mtu, wakati hawajawahi kufika jimboni humo na kuangalia hali ya kisiasa ilivyo:

Duu kumbe kuna majimbo yana watu wao
 
Back
Top Bottom