AUDIO: Nilichokisema Jana Makutano na Fina Mango!

Kumbe uliugua kwashiakor, nimekusamehe utumbo wote uliosema kuanzia CDM na viongozi wake, na kuhusu Mzee Lowassa.

...daah kamanda umegonga na msumari wa moto kwenye jipu,side efects zinamsumbua dogo,ngoja limamvi limsikie linapambanaga kimyakimya na mjombaake mh sita kalichokoza juzikati...
 
We mtoto mdogo sana kwa Lowasa. Mwenzako ameanza siasa wewe unafundishwa arif be te ke madrasa. Utaumia dogo ukijifanya kupimishana ubavu naye. We lete vululu vululu zako tu uone kama hajakupoteza kwenye siasa.
hongera mfuasi wa ustadh Abdallah lowasa, tumekusoma,.
 
Ndani ya ccm lowasa ni moto wa kuotea mbali, sio Nape, mangula au kikwete, wote wanamgwaya, je wewe utaweza pingana naye? Mh. Mbunge labda uondoke ccm, vinginevyo atakupotezea mbali huyu jamaa, mwigulu kaanza kulamba viatu vya Lowasa mapema!
 
Hivi kwanini wanaCCM wenzangu ni waoga sana kusema kile wanachokiamini na kubaki kupaka paka rangi upepo?
Hapa Dr.Kigwangwala hamtaki Lowassa lakini anasema kwa woga sana, why so?
Hivi Lowassa atahitaji kura ya Kigwangwalla au atahitaji nguvu kazi yake?

Kwanini Kigwangwalla usiseme wazi kwamba Lowassa HAFAI KABISA na kama CCM wakimpitisha kuwa mgombea urais 2015 basi hautamuunga mkono na ikibidi utampinga wazi wazi.

Mbona kanyoosha maneno kabisa kuwa yeye hatampigia mwizi nyanyi Lowassa?
 
Mbona kanyoosha maneno kabisa kuwa yeye hatampigia mwizi nyanyi Lowassa?

Haha...Yericko..Km ni kura yake tuu ndhani wal hakuhitaji sema.Km ni pamoja na kura za wengine alitaka nazo zisimwendee ni wazi kuwa anasema kuwa kuwa si tu kwamba hatompigia kura ila pia atakampeni dhidi yake.NI wazi Dr. anayo shida hapa.

Ndio maana nimemwambia aachane na siasa za kujisjikiza kwa watu.. ajenge identity yake inayoishia kwake na wengine watakaomwona kuwa yeye ni kiongozi wao full stop.Muda wake mwingine ajenge heshima ktk career yake ya mwanzo.Hata awafundishe watu wake kutumia vyoo, kusafisha maji, na mengine ambayo ahata akina Messi wanapenda tembelea kijiji yao rosario huwa huru kushirikiana na watu wake.Pia hii itamjenga kw akiasi cha siku moja kuwa ktk nafsi ya kusimama kwa nafasi ya urais.Kwani km watu wanaomwamini na kumuona kiongozi wataongezeka over the years before jamii nzime kusema tunadhania huyu anafaa kuwa rais haalfu wengi waseme kweli.

Hawa wanasiasa wachanga hawaamini kuwa unaweza kuwa string kwa kuheshimu sheria za chama, za nchi, na kuwa principal za kweli utakazozifuata kwa moyo wote.

Zijawahi msikia Mnyika akikikimbizana na siasa za makambi, siku zote kaheshimu sheria, na kubaki na choices zake hadi muda muafaka ukifika.Na hajakosana na mtu mwenye akili CDM yeyote.Wala hahitaji weka rehani chochote chake kwa sababua ya makambi.
 
Kura ni siri yako hukupaswa kutangaza. Hata hivyo km ccm watamsimamisha ina maana utapigia upinzani!? Km ulikuwa una maanisha hutamuunga mkono kutokana nguvu zako za kisiasa,hapo umechemka! Huna ushawishi wowote na una 1% ya kurudi Bungeni. Na safari hii waliokubeba hawatakuwepo.
 
Mbona sijasikia sehemu anakosema kua rais KIKWETE uongozi wake ni mbovu? je anampendaje Kikwete na kumchukia LOWASA? wakati wote wametupa hasara na wanazidi kutupa hasara?
 
mnahangaika sana vijana na kambi zenu za kudidimiza nchi

umpe usimpe ni issue yako ndio maana kura hazipigwi redioni wana ku kuhesabu vichwa, uamuzi wako ni siri yako na ballot paper

Mkuu Hamis, you are an ectopic in CCM, kauli zakko na matendo yako vinachanganyana mno kiasi kwamba yaonekana hata wewe umechanganyikiwa

DONT GET YOURSELF IN THE LINES OF FIRE KWA KUTAFUTA SIFA ZA MUDA MFUPI... ZIP IT AND DO YOUR "THANG"....
 
Nategemea Dr. ajipambanue kwa umakini hapa kabla yakwenda lala, ajaribu jibu maswali yote yenye challenge kwake..kwani hii ni hatua mojawapo kujijenga ktk kizazi hiki cha dot com.NIsingependa ajiangushe km Zitto.. kwani wote ni wanatambulika km vijana, tena vijana waliopewa upendeleo wa kipekee, kwani ahta wafanye blunder kiasi gani bado watanzania wanawapa nafsi ya kuwasikiliza tena..Ila Zitto yeye huja na hoja ya kuchukiwa tuu kuliko kujibu maswali magumu.Ila yote hayo yana mwishoNa mwisho ni pale vijana makini wanapoingia ktk siasa.Ujana wa hawa wanasiasa wetu uatapotelea hewani wote, na ktk undi la wakomavu pia nako hapatakuwa na nafasi kwao.Watabaki kulazimishwa kuwa washambiki wa wengine..na sijui km watapata nafasi ya kujitetea hata km wazee wa music wa Dance walivyokuwa wakijitetea kuwa mizki ya enzi yao ilikuwa na maadili sijui na mafunzo hadi professor J, na Sugu wakashuka mashairi yaliyowafanya wazee watafute tuu namna ya kufanya kolabo.
 
hahahahah HKigwangalla unatudanganya tuu ili umlidhishe Nape Nnauye na membe.

Ni wazi kuwa ccm mnamuogopa sana lowasa.

pole sana kwa huo ugonjwa hila kura ni siri yako usiwadanganye watu.
 
Last edited by a moderator:
......Kumbe uliugua kwashiokor na Marasmus wakati upo mtoto!!, Leo nimepata jibu katika swali nililokuwa najiulizaga mara kwa mara ulivyokuwa unachangia hoja zako bungeni. Bila shaka ulienda kuponea kwa Waganga wa kienyeji. Pole sana!
 
Kigwangala kwa mara nyingine umeharibu sana, na nina hakika unajuta huko uliko

1. awali CCM yote ni wezi na hata nafsi yako inajua hilo
2. swala la Richmond muhusika mkubwa ni Kikwete na kila mtu anajua hilo
3. hujasema sababu za kutompa kura Lowassa, umesema tu Richmond, swala ambalo 'Kisiasa' alishwajibika nalo kwa kujiuzulu, au hauamini katika kujiuzulu? japo alifanya hivyo kukilinda chama ambacho wewe unavaa kijani
4. umeingia kwenye mkumbo wa kuwaza urais, na umeongea myth.....inaonyesha unamwogopa Lowassa na uko kwenye kundi ambalo unatumika, au kujipendekeza, bila kujua hawana msaada wowote kwako
5. huwezi, na hutaweza kushindana na Lowassa, Lowassa alivyoondoka madarakani, na alivyoanza kurudi ni dhahiri ana nguvu kuliko akina nyie na membe wako

6. ukkiwa kijana, kwepa kuongelea 'logic' zinazokinzana; wewe ni CCM, Lowassa ni CCM, sasa kusubiri mtu au kumwona mchafu kipindi anagombea urais....ILA MSAFI AKIWA MWANACHAMA NI UNAFIKI WA JUU KABISA , ambao nikikutana na ww nakutemea mate , you r not different from DOG; stand up now, ondoa wachafu wote ndani ya CCM, Lowassa anafanya shughuli zote za chama na kibunge........AU KWAKO WEWE UNAMTAMBUA MCHAFU AKIWA MGOMBEA URAIS TU??? ILA AKIWA NA VYEO VINGINE NI SAWA....umeona...

7. siendelei nimemaliza
 
......Kumbe uliugua kwashiokor na Marasmus wakati upo mtoto!!, Leo nimepata jibu katika swali nililokuwa najiulizaga mara kwa mara ulivyokuwa unachangia hoja zako bungeni. Bila shaka ulienda kuponea kwa Waganga. Pole sana!

Duh..aisee mna hasira nae..hembu mpeni muda kidogo achangie jamani asijeogopa kabisa jibu maswali aliyoulizwa na baadaye ikaonekana alinyimwa haki yake.Angekuwa Zitto na Nape ni wazi wangesepa km hakuna ch akuwasifia.Tena Zitto angesema ni wale wanchukiao kwa ukanda na dini yake..

Tumpe Muda ajitetee na kujitofautisha na wanasiasa vijana wetu wengine ambao ni too naive.Kujibu hoja kwa upade wa CCM ni extremely challenging.Ningependa sana kumsikia ataonyesha umahiri gani ktk hili.Inaweza kuwa mwanzo wake wa kufanya mapinduzi ktk mwelekeo wake kisiasa.
 
i said this b4. i say this again...to a dog it doesnt matter whether the rat is pregnant or not...mkuu Kigs hata ubunge ulibebwa mno na chama chako. istoshe u cnt eat a cake and hav it! unalamba viatu vyao alaf nyoo cwapgi kura, just bcoz u hate smone? vp mkipatanishwa? utakula ur vomitus? b a man and think twic bro' b urself and decide, either u ar with us or with the terrorists(in this cas mafsad) the choic is urs.
 
i said this b4. i say this again...to a dog it doesnt matter whether the rat is pregnant or not...mkuu Kigs hata ubunge ulibebwa mno na chama chako. istoshe u cnt eat a cake and hav it! unalamba viatu vyao alaf nyoo cwapgi kura, just bcoz u hate smone? vp mkipatanishwa? utakula ur vomitus? b a man and think twic bro' b urself and decide, either u ar with us or with the terrorists(in this cas mafsad) the choic is urs.

Watu mnawajuana sana humu ndani..yaani kwa jinsi unavyomsema nini npata tafsiri km vile jamaa anaongeza dau tuu kwa makeke km ya kwenye mnada na si kingine,halafu baadaye asema kwa hili imebidi nimkubali Mong`o. .a.k.a Rafiki.
 
Hamisi nafasi Kama hizi za kuhojiwa na vyombo vya habari ni nzuri sana kwa mwanasiasa japo pia zaweza kukuua kisiasa, hukuwa na haja yeyote ya kutuonyesha kambi yako kisiasa maana hata hao unawawakirisha hawajasema kama watagombea so umemwonea sana Lowasa. Nakushauri uende taratibu muda unao na bahati unayo siunaona ulipewa nafasi ya kuwakirisha ccm japo ulishindwa kwenye kura za maoni. Hakuna adui wa kudumu katika siasa kesho Kikwete atakuwa rafiki wa Lowasa na utakosa pakujificha.
 
Back
Top Bottom