kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
MKAZI wa Tambani Kitonga wilayani Ilala mkoani Dar es Salaam Kiraryo Chacha (39), amejinyonga baada ya kuudhiwa na wenzake katika kilabu cha pombe.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile alisema Chacha alikutwa amejinyonga kwa kutumia khanga ya mke wake aliyokuwa ameitundika katika mkorosho uliopo jirani na banda la kuku juzi saa 3 usiku nyumbani kwake Msongola.
Kwa mujibu wa mtoto wa marehemu (jina limehifadhiwa) muda mfupi kabla ya Chacha
kuchukua uamuzi huo, alirudi nyumbani akiwa amelewa na kusema atajinyonga kwa sababu kilabuni wamemuudhi.
Kijana huyo alisema baba yake alilalamika kuudhiwa na watu waliokuwamo kilabuni ingawa hakuwataja majina na baadaye aliingia chumbani kwake na hakumuona mpaka alipomkuta amejinyonga.
Maiti yake imehifadhiwa katika Hospitali ya Amana huku polisi wakiendelea na upelelezi.
Katika tukio jingine, mkazi wa Tabata Kisiwani aliyetambuliwa kwa jina moja la Lasta (30), amekutwa amekufa katika machinjio ya nguruwe ya Tabata wilayani Ilala huku akitokwa na povu mdomoni na mwili wake ukiwa hauna jeraha lolote.
Maiti hiyo iliokotwa juzi saa 12.30 asubuhi na chanzo cha kifo hicho hakijafahamika na maiti amehifadhiwa katika Hospitali ya Amana kwa uchunguzi zaidi.
Aidha mvuvi Ibrahimu Ally (30), mkazi wa Mtoni Sabasaba amekutwa akiwa amekufa huku maiti yake ikielea ufukweni mwa bahari ya Hindi eneo la Kurasini katika Kijiji cha Wavuvi.
Maiti hiyo ambayo iliopolewa na wananchi wa eneo hilo, iliokotwa ikiwa haina jeraha lolote na inasemekana marehemu alikuwa akivua samaki peke yake na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile alisema Chacha alikutwa amejinyonga kwa kutumia khanga ya mke wake aliyokuwa ameitundika katika mkorosho uliopo jirani na banda la kuku juzi saa 3 usiku nyumbani kwake Msongola.
Kwa mujibu wa mtoto wa marehemu (jina limehifadhiwa) muda mfupi kabla ya Chacha
kuchukua uamuzi huo, alirudi nyumbani akiwa amelewa na kusema atajinyonga kwa sababu kilabuni wamemuudhi.
Kijana huyo alisema baba yake alilalamika kuudhiwa na watu waliokuwamo kilabuni ingawa hakuwataja majina na baadaye aliingia chumbani kwake na hakumuona mpaka alipomkuta amejinyonga.
Maiti yake imehifadhiwa katika Hospitali ya Amana huku polisi wakiendelea na upelelezi.
Katika tukio jingine, mkazi wa Tabata Kisiwani aliyetambuliwa kwa jina moja la Lasta (30), amekutwa amekufa katika machinjio ya nguruwe ya Tabata wilayani Ilala huku akitokwa na povu mdomoni na mwili wake ukiwa hauna jeraha lolote.
Maiti hiyo iliokotwa juzi saa 12.30 asubuhi na chanzo cha kifo hicho hakijafahamika na maiti amehifadhiwa katika Hospitali ya Amana kwa uchunguzi zaidi.
Aidha mvuvi Ibrahimu Ally (30), mkazi wa Mtoni Sabasaba amekutwa akiwa amekufa huku maiti yake ikielea ufukweni mwa bahari ya Hindi eneo la Kurasini katika Kijiji cha Wavuvi.
Maiti hiyo ambayo iliopolewa na wananchi wa eneo hilo, iliokotwa ikiwa haina jeraha lolote na inasemekana marehemu alikuwa akivua samaki peke yake na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke.