Naweza kusema ni kwasababu ya elimu inayotolewa upande huo na cha zaidi sana ni upendo unaohubiriwa humo.
Penye upendo pana maarifa, ila penye chuki hutawala ujinga kama sio upumbavu.
Mabadiliko/evolution katika viumbe yapo! Mabadiliko haya kama wasemavyo wataalamu tunaweza kusema mwislam akijitambua kiasi kidogo anarukia kwenye ukristo... Mkristo nae akijitambua kiasi anarukia kwenye kuhoji uhalali wa hizi dini pamoja na maisha kwa ujumla.
Ukivuka hizi ngazi zote unabaki kuwa mtazamaji huku ukiyashuhudia makosa yako katika maisha pamoja na dosari ndogondogo katika maisha ambazo zipo ndani ya uwezo wa mwanadamu ambapo zikirekebishwa maisha yanakua marahisi, matamu na yasiyo na majuto