Athari za Kutohimiza Kiingereza

Augustine Moshi

JF-Expert Member
Apr 22, 2006
2,554
1,382
Madhara ya Kutokipa Kiingereza Umuhimu

Siku hizi nchi yetu ina tatizo la wananchi wengi kutoweza kuandika na kuzungumza kwa lugha ya Kiingereza. Kiuchumi, TAZIZO HILI SIYO HIMILIVU.

Adhari zake ni pamoja na zifuatazo:

1. Kukosa ajira za kimataifa. Nchi kama Uingereza inakuwa na upungufu wa manesi mara kwa mara. Wanaajiri toka Malawi, Kenya na nchi nyingine ambazo raia wake wanamudu lugha ya Kiingereza.

Mashirika kama Emirates huwa yanahitaji waajiriwa wachache wanaoweza kuongea Kiswahili na Kiingereza. Huwa wanaajiri Wakenya kwani wana hiyo sifa.

2. Kukosa ajira nchini. Nyumbani kwenyewe mashirika binafsi wanapenda zaidi wahitimu waliosoma nje kwani wao humudu lugha zote mbili.

3. Kukosa fursa za kusikika ulimwenguni. Mashirika ya habari kama Aljazeera na BBC World service wanapotaka kuongea na mtu wa Afrika Mashariki, kwa Kiingereza, huwa hawachagui Mtanzania. Wataongea na mwalimu wa chuo kikuu Mkenya au Mganda. Hii inafifisha umaarufu wa vyuo vyetu. Vinashuka kwenye viwango rasmi vya ubora duniani.

Ukiweka YouTube kitu kwa Kiswahili maana yake unakilenga kwa watu milioni 200. Ukiweka kwa Kiingereza basi umekielekeza kwa watu zaidi ya mara tano ya hao.

4. Kudumaza elimu. Reading materials mtandaoni sehemu kubwa ni za Kiingereza. Mtu asiyeelewa vizuri Kiingereza tayari anajinyima asilimia kubwa ya maarifa yaliyopo duniani.

5. Kudumaza utalii. Kutosikika kimataifa kunatunyima watalii wengi. Pia wachache wanaokuja wanajikuta hata watu wa uhamiaji na polisi hawawezi kuzungumza nao kwa Kiingereza.

Miaka ya sitini tulikuwa vizuri tu kwenye Kiingereza. Mhitimu wa shule ya sekondari alikuwa anabidika kufaulu Oral and written English.

Napendekeza kwamba:
1. Interview za ajira serikalini zizingatie uwezo wa kusema na kuandika Kiswahili na Kiingereza. Kumudu Kiingereza iwe a condition for employment of ALL civil servants.

2. Kuwe na sera ya wanafunzi shule za sekondari kuongea tu Kiingereza wawapo shuleni. Hii haitadhoofisha Kiswahili kwani watakiongea sana nyumbani na mitaani.

3. Kufaulu kidato cha nne iwe ni pamoja na kufaulu Oral English. Mitihani yake itasimamiwa na shule kama ilivyokuwa miaka ya sitini.
 
Tatizo ni kwamba tuna watu wenye IQ ndogo sana. Uthibitisho mojawapo wa low IQ ni kutofundishika. Mtu amesoma English akiwa primary, secondary, high school, bachelor degree, masters degree, mpaka PhD. Huko kote anasoma Kiingereza lakini bado haelewi!

Miaka ya hivi karibuni, ilikuwa ya maajabu zaidi. Nilikuwa sijawahi kushuhudia PhD holder aliyesoma kwa miaka yote kwa Kiingereza lakini hawezi kuongea Kiingereza.
 
Tatizo ni kwamba tuna watu wenye IQ ndogo sana. Uthibitisho mojawapo wa low IQ ni kutofundishika. Mtu amesoma English akiwa primary, secondary...
Sikubaliani nawe kwamba tuna IQ ndogo. Yaani IQ zetu zimeshuka? Maana miaka ya huko nyuma tulikuwa tunakimudu Kiingereza vizuri. Na hata sasa wanaosoma nje wanakimudu Kiingereza. Kwani IQ zao ni kubwa zaidi?
 
Kiingereza ni lugha Tu kama lugha zingine tatizo ni exposure tu

Hebu uwe kabila lolote hujui kiingereza uzamie Kwa wanaozungumza kiingereza tu uone kama hutajua.

Kuna mataifa yaliyoendelea kama Japan , urusi, German, China ,nk yanafundisha kilugha Chao na sasa yameendelea kuliko Sisi ma half cast wa lugha
 
Ujerumani na Japan ni nchi zenye teknolojia kubwa duniani na hawatumii kiingereza katika mitaala Yao yote na hata Kama lugha ya Taifa , Taifa imara ni lile linalosimamia misingi yake kuanzia kuwa na lugha yake wenyewe ukisema tuhamasishwe kutumia kiingereza ina maana unaturudisha katika utumwa wa kifikra na kuendelea kujiona dhaifu Kwa kudharau vitu vyetu
 
Kiingereza ni lugha Tu kama lugha zingine tatizo ni exposure tu

Hebu uwe kabila lolote hujui kiingereza uzamie Kwa wanaozungumza kiingereza tu uone kama hutajua.

Kuna mataifa yaliyoendelea kama Japan , urusi, German, China ,nk yanafundisha kilugha Chao na sasa yameendelea kuliko Sisi ma half cast wa lugha
Fact mkuu, issue hapo ni exposure tu, l
 
Madhara ya Kutokipa Kiingereza Umuhimu

Siku hizi nchi yetu ina tatizo la wananchi wengi kutoweza kuandika na kuzungumza kwa lugha ya Kiingereza. Kiuchumi, TAZIZO HILI SIYO HIMILIVU...
Umeongea vyema chifu,yaani sijui kwanini watu wanadhani kukipa kiingereza na lugha zingine za kimataifa nafasi kwenye mfumo wa Elimu,ni kudumaza kiswahili.

Mimi hizi lugha huwa nazichukulia kama silaha!!ukienda vitani huchagui silaha!!unaenda na yoyote itakayosaidia mapambano,Jameni hebu fikiria kama mtoto wa Kitanzania,anamaliza darasa la saba na anakuwa na uwezo wa kuongea kifaransa,kichina,kireno,kijerumani!! So amazing!!
 
Sasa,wewe sikiliza Mabongo yaliyofeli Kingereza yatakavyokujibu hapa!

Kingereza hayajui,Kiswahili na chenyewe hayajui,utasikia "shure","mbadara","halakisha",etc..
Kama bado mawazo yetu yapo mufilisi ivi, tatizo la ujinga Tz haliwezi kuisha, haiwezekani kwa mtu anayejielewa kuamini katika lugha ya kiingereza ndio kuwa imara zaidi huu ni ujinga ulioendelea, lugha si kigezo cha kupima contents ya mtu alizonazo kichwani kiingereza ni sawa na lugha nyingine..
 
Zambia,Malawi,Kenya,Ghana wanaongea kingereza sana tu. Je wametupita nini katika maendelea ya kiuchum,sayansi na teknolojia?
Kinachowasumbua ni utimwa wa kifikra, huu ugonjwa kumtoka mwafrika ni kazi sana.
Wkati wewe unawaza kingereza kuna waafrika wenzio wanawaza kifaransa kifundishwe vizuri lakini kuna wengine wanawaza kireno bila kusahau kiarabu.
Ni ukoloni tu unaowasumbua watu weusi hakuna kingine.
 
Zambia,Malawi,Kenya,Ghana wanaongea kingereza sana tu. Je wametupita nini katika maendelea ya kiuchum,sayansi na teknolojia?
Kinachowasumbua ni utimwa wa kifikra, huu ugonjwa kumtoka mwafrika ni kazi sana.
Wkati wewe unawaza kingereza kuna waafrika wenzio wanawaza kifaransa kifundishwe vizuri lakini kuna wengine wanawaza kireno bila kusahau kiarabu.
Ni ukoloni tu unaowasumbua watu weusi hakuna kingine.
Fact mkuu, mtu mweusi kumtoa kwenye giza na kumpeleka kwenye nuru ni Nazi zaidi kuliko kumtoa kwenye nuru na kumpeleka kwenye Giza, hii ngozi hii ni shida tumekuwa watumwa kifikra ,lugha na kiuchumi pia
 
Mwehu kabisa wewe

Nani amekuambia tunataka ujue Kingereza ndio kigezo cha ubora wa content kwenye bongo lako bovu hilo?

Tunataka kutumia Kingereza kama "nyenzo" ya kupambana na walimwengu upate unachotaka kwa urahisi na wingi

Yaani ukishaongelea Kingereza tu,stupid people like you mnadhani tunazungumzia una akili kiasi gani na mnaanza kujiharishia...

Kama kweli wewe unapenda Utanzania hasa,tuna lugha 350,unajua hata mojawapo hapo kwa ufasaha hata ile ya kabila unalotoka wewe?HUJUI

Tupo duniani,ni uwanja wa vita,nyenzo ya kushinda vita ili upate unachotaka kwa walimwengu ni Kingereza na sio Kiswahili wala Kichagga

Stay in your place and shit on yourself you dummy!
Acha fikra za kitumwa mkuu, China,Russia, German,Korea wanatumia kiingereza??,hizi fikra zetu za kitumwa zinatufanya tuwaze mawazo ya kitumwa na tuishi kitumwa tumwa tu, jinga kabisa
 
Acha fikra za kitumwa mkuu, China,Russia, German,Korea wanatumia kiingereza??,hizi fikra zetu za kitumwa zinatufanya tuwaze mawazo ya kitumwa na tuishi kitumwa tumwa tu, jinga kabisa
Mkuu huyo bado kid ak teenager achana nae.
Mtu mzima kama mimi siwezi waza kama huyo mtoto.Akikua ataacha, zamani tuliamini hadi nzi wa kizungu wapo kumbe ulikuwa utoto.
Kama anapenda sana kingereza ajifunze vyuo vipo tele,shule za english media zipo tele, rasi simba yupo kila mkoa, mitandaoni zimejaa tutorials za kingereza nyingi sana, maktaba zimejaa mavitabu ya kingereza bado analia kingereza hajui.
Wache kuilamu serikali kuhusu kingereza maana imeweka demokrasua ya hali ya juu katika kujifunza lugha hadi kifaransa, kiarabu zipo kwenye mtaala wa Tanzania,.
Walichokalia ni kulaumu tu.
 
Kiingereza ni lugha Tu kama lugha zingine tatizo ni exposure tu

Hebu uwe kabila lolote hujui kiingereza uzamie Kwa wanaozungumza kiingereza tu uone kama hutajua.

Kuna mataifa yaliyoendelea kama Japan , urusi, German, China ,nk yanafundisha kilugha Chao na sasa yameendelea kuliko Sisi ma half cast wa lugha
Hatuna uchumi huo wa kutegemea lugha ya kiswahili itusogeze mbele kimaendeleo, watu wetu lazima wafundishwe na wajue kingereza kwa ufasaha ili waweze walau kucompete katika soko la ajira hata kwa East Africa tu.

Usifananishe Tz na nchi hizo, nchi ambazo majasusi wao wa kiuchumi wamejaa nchi zingine wakitafutia nchi zao fursa na wakiongea kingereza kwa ufasaha kabisa.
 
Madhara ya Kutokipa Kiingereza Umuhimu

Siku hizi nchi yetu ina tatizo la wananchi wengi kutoweza kuandika na kuzungumza kwa lugha ya Kiingereza. Kiuchumi, TAZIZO HILI SIYO HIMILIVU.

Adhari zake ni pamoja na zifuatazo:

1. Kukosa ajira za kimataifa. Nchi kama Uingereza inakuwa na upungufu wa manesi mara kwa mara. Wanaajiri toka Malawi, Kenya na nchi nyingine ambazo raia wake wanamudu lugha ya Kiingereza.

Mashirika kama Emirates huwa yanahitaji waajiriwa wachache wanaoweza kuongea Kiswahili na Kiingereza. Huwa wanaajiri Wakenya kwani wana hiyo sifa.

2. Kukosa ajira nchini. Nyumbani kwenyewe mashirika binafsi wanapenda zaidi wahitimu waliosoma nje kwani wao humudu lugha zote mbili.

3. Kukosa fursa za kusikika ulimwenguni. Mashirika ya habari kama Aljazeera na BBC World service wanapotaka kuongea na mtu wa Afrika Mashariki, kwa Kiingereza, huwa hawachagui Mtanzania. Wataongea na mwalimu wa chuo kikuu Mkenya au Mganda. Hii inafifisha umaarufu wa vyuo vyetu. Vinashuka kwenye viwango rasmi vya ubora duniani.

Ukiweka YouTube kitu kwa Kiswahili maana yake unakilenga kwa watu milioni 200. Ukiweka kwa Kiingereza basi umekielekeza kwa watu zaidi ya mara tano ya hao.

4. Kudumaza elimu. Reading materials mtandaoni sehemu kubwa ni za Kiingereza. Mtu asiyeelewa vizuri Kiingereza tayari anajinyima asilimia kubwa ya maarifa yaliyopo duniani.

5. Kudumaza utalii. Kutosikika kimataifa kunatunyima watalii wengi. Pia wachache wanaokuja wanajikuta hata watu wa uhamiaji na polisi hawawezi kuzungumza nao kwa Kiingereza.

Miaka ya sitini tulikuwa vizuri tu kwenye Kiingereza. Mhitimu wa shule ya sekondari alikuwa anabidika kufaulu Oral and written English.

Napendekeza kwamba:
1. Interview za ajira serikalini zizingatie uwezo wa kusema na kuandika Kiswahili na Kiingereza. Kumudu Kiingereza iwe a condition for employment of ALL civil servants.

2. Kuwe na sera ya wanafunzi shule za sekondari kuongea tu Kiingereza wawapo shuleni. Hii haitadhoofisha Kiswahili kwani watakiongea sana nyumbani na mitaani.

3. Kufaulu kidato cha nne iwe ni pamoja na kufaulu Oral English. Mitihani yake itasimamiwa na shule kama ilivyokuwa miaka ya sitini.
Kwahiyo hutaki tukawa na wauza mitumba!
 
Back
Top Bottom