ATCL kuwaleta wachina 200 kila wiki nchini

ATCL kuwaleta wachina 200 kila wiki nchini

uzuri wa serikali ya JPM inawajibu matomaso kwa vitendo, wote wanaosema ni uongo si kwamba hawaamini itakuwa hivyo ila wanaogopa kuaibika kwa sababu walisema ndege zitakosa wateja.
 
Dege limepata pa kwenda bado watu hawataki, sasa mnataka liatamie mayai bila dume hili dege la kike walahi

Wacha likadange lituletee machotara wa kichina
 
Na kurudi wanarudi wangapi ? Tumechoka kuletewa wamachinga wakichina !
 
Aisee ni short term plan ama ni endelevu? Kwahiyo kwa mwezi litafanya safari NNE zenye jumla ya wavimba macho 800... Kwa hesabu za haraka ukiuza kila tiketi kwa bei ya juu ya USD 1500 utapata wastani wa USD 1.2... M... Ambazo ni sawa na 2.5B kwa makisio ya haraka
umisahau hizo safari wanaruka kwa UNGO bila gharama yoyote au?!!
 
Wachina na utalii???? tena 200 per month ...kuna chumvi imeongezwa kidogo.
 
uzuri wa serikali ya JPM inawajibu matomaso kwa vitendo, wote wanaosema ni uongo si kwamba hawaamini itakuwa hivyo ila wanaogopa kuaibika kwa sababu walisema ndege zitakosa wateja.
Mzee hujateuliwa tu!
Hata ujumbe wa nyumba 10

Ova
 
Shirika la Air Tanzania limeingia kwenye makubaliano na kampuni ya China iitwayo Touchroad International Holdings Group, ili kutangaza sekta ya utalii Tanzania kwa kuwasafirisha wageni wa kitalii kutoka Hangzhou China na kuwaleta moja Kwa moja hapa nchini kwa kutumia ndege ya Air Tanzania aina ya Boeing 787-8 Dreamliner.

Kwa mujibu wa makubaliano, safari hizo zitafanyika kila wiki ikiwa na wataliii sio chini ya mia mbili (200) na Safari ya kwanza itaanza mwezi wa nane mwaka huu.
Wachina siyo watalii, Wachina wanakuja kuchukua kazi yako. Ni Wachina wchache sana wanaokuja nchini kwa utalii. Nimewahi kutalii ktk mbuga zetu ckuwahi kukutana na Wachina. Wengi unaokutana nao ni wazungu. Wachina wao wanakuja kutafuta ajira na kuwaletea vitu feki. Wachina wameshajua watanzania tumelala. Ndio maana utawakuta kwenye kuuza karanga wapo, chips mayai wapo zile kazi ambazo wanatakiwa wafanye wazawa wao ndio wanafanya. Umewahi kumwona wapi mzungu kutoka Europe akiuza Karanga au chips kariakoo???
 
Kusapoti ufunguzi wa ubalozi Tanzania, kwa Tanzania kuwa nchi ya 13 Africa kukubali Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israël, kwa hiyo ile ilikuwa ni shukran na si vinginevyo wewe usiejua siasa za majitaka ujue.
Umekariri. Na wale waisrael huwa wanakuja kufanya nini?
 
Watalii wa Kichina. Mchina aje kutalii na kuondoka hivi hivi kweli ?. Wazee wa fursa hawa.
 
Tuache kudanganyana watalii wanatoka Ulaya na Marekani. Sio China wala India.


Kikawaida mtalii ni mtu mwenye pesa ambae husafiri kwenda eneo fulani kwa ajili ya leisure

Huko China kuna matajiri kama Matajiri waliopo Ulaya. Mtalii anaweza toka hataTanzania pia sababu hata hapa nchini tunao watu wenye vipato vikubwa ambao wanao uwezo wa kufanya matumizi ya milioni moja kila siku na tena ni wengi sana tu

Matajiri wapo nchi zote duniani leo hii sababu ukoloni haupo kwamba nchi fulani ni koloni halafu nchi fulani colonial masters
 
Watalii wa Kichina. Mchina aje kutalii na kuondoka hivi hivi kweli ?. Wazee wa fursa hawa.
huo ndio utalii unaopigwa chapuo sana duniani kwa sasa, utalii-uwekezaji. utalii- uwekezaji si tu unatangaza utamaduni na vivutio vya utalii bali unaenda mbali zaidi kwa kujikita katika uchumi, biashara na ujasiriamali kwa maana ya uwekezaji. kama wachina wanakuja kufanya utalii wakiwa na lengo la kutafuta fursa za uwekezaji itakuwa ni habari njema kwa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom