Atakayejaribu kuharibu amani yetu ni heri atangulie akatuandalie makazi ya milele

Usitutisheeee
Sidhani kama waweza kuwa mama kweli.!
Jukumu kubwa la mama ni kuangalia madhara yajayo kwa watoto wake!
Ukiona mama anajiwazia yeye kwanza waweza kumuweka katika kundi la wanawake waliopata mimba kwa bahati mbaya.!

1: ikitokea vurugu kisha Nchi ikakosa uelekea thabiti wewe na wanao mtakaa wapi kwa amani?
Mifano ipo hai.. fikiri kuhusu wamama wa Syria, Libya, Congo,Iraq, Ukraine. Somalia, South Sudan.. na Nk.

Na hapa nikukumbushe tu. Inapotokea vita ama machafuko yoyote ya kisiasa wanaoathirika zaidi ni akina mama na watoto.!

2: unapochochea machafuko yoyote tegemea kupata pande mbili zinazo kinzana wale wanaoona wako sawa na wale wana ona hawatendewi sawasawa.!

Katika harakati hizo inategemea mwenye Nguvu ni yupi.!

Utakapoenda barabarani kupigania unachodhani ni haki yako.! Huenda ukakutana na askari ambaye atakujeruhi. Ukavunjika ama mguu au kiuno ama mgongo! Kumbuka askari huyu kafundishwa kituliza ghasia kwa nguvu (Field Force Unit.) Ni kitengo maalumu kwa kazi hiyo..

Sidhani kama atakubembeleza ili uache ufanyacho.! Ukipata hayo majeraha atakayetunza wanao ili wawe na afya bora na malezi kutoka kwa mama ni nani?

Huoni kuwa yamkini utakuwa hukuwatendea haki wanao?

Mwisho:

Kabla hujachochewa ama kujichochea mwenyewe kufanya vurugu zozote tafakari..

1:Je hiki ninacho ambiwa nikipinge ni kweli kina huo uovu?

2: baada ya kukipinga wewe binafsi utapata faida gani?

Natumai unaweza ambulia kitu hapa ukitaka.
 
Leo ninawaletea makala fupi yenye lengo la kukufahamisha wewe Mtanzania namna mbinu chafu za Wamagharibi( Marekani & Ulaya) zinavyotumika katika nchi nyingi za Afrika, Latini Amerika na Asia kuangusha Utawala uendao kinyume na matakwa yao.

Nchi za Marekani na Ulaya kwa asili yao ni nchi za Kibepari na msingi mkuu wa Ubepari ni unyonyaji katika kile kiitwacho mwenye nguvu na apate ( Suvival for the Fittest ).

Kutokana na msingi huo mkuu wa Ubepari Mataifa haya hufanya kila mbinu kuhakikisha Nchi za Afrika, Asia na Latini Amerika kuwa na viongozi wanaowanyeyekea na wenye ulimbukeni wa Ulaya na Amerika ya Marekani ili iwe rahisi kuwalaghai na Unyonyaji uendelee kutamalaki na kuota mizizi zaidi.

Inapotokea Nchi imempata kiongozi ambaye kwa namna yoyote, matendo yake, kauli zake na hulka yake haiendani na matakwa yao yaani anakuwa kizuizi kati ya Taifa hilo na malengo ya Maperari ambayo ni Unyonyaji, Nchi hiyo aidha ya Latini Amerika, Asia ama Afrika hujikuta katika wakati mgumu kuendesha utawala wake kwa maana Mabepari huanza kutumia mbinu mbali mbali kuuangusha utawala huo thabiti.

Hakika nasikitika kuona Tanzania tumeingia rasmi kwenye Mgogoro huo na Wamagharibi lakini zaidi nasikitika kuona baadhi ya Watanzania wakiungana nao kwa wengi kutokukujua na wachache kwa kujua kutokana na maslahi binafsi kwanza.

Tanzania kupitia uongozi huu wa Awamu ya Tano umejinasibu kwa vitendo, hulka na maneno kuwa haukubaliani na Unyonyaji wa aina yoyote kwa Taifa letu kwa kufanya mambo kadhaa.

Kwanza, ni kufuta Safari zote za nje zisizo na tija kwa Watanzania ambazo kwa kiasi kikubwa zilikuwa zikifanywa na viongozi wa Serikali, Bunge na Mahakama na hii ilikuwa inatumika kama njia mojawapo ya kuwashawishi viongozi hao kukubaliana na matakwa mbalimbali wakiwa huko ughaibuni kwa maana ni rahisi zidi kumshawishi mtu akiwa nyumbani kwako kuliko akiwa nyumbani kwake. Hii kwa kiasi kikubwa imewanyima fursa nyeti Mabepari ya kukutana mara kwa mara na viongozi wenye dhamana ya maamuzi hapa Tanzania.

Pili, ni namna Serikali ya awamu ya tano inavyoshughulika na wala rushwa na inavyopambana kukemea na kutokomeza ufisadi.

Kiukweli hakuna Taifa lolote la Magharibi linalotamani Tanzania tuwe ni moja ya mifano bora katika jambo lolote kwa kuwa wanatambua kwa sisi kuwa bora katika kupambana na rushwa itakuwa ndio njia ya sisi kupiga hatua za kimaendeleo na kuondokana na umasikini kwa sababu umasikini kwa kiasi kikubwa hutokana na ubadhirifu wa mali za umma ( Ufisadi & Rushwa ), wakati mpango wa "Siri" wa Mataifa ya Magharibi ni kuhakikisha kwa namna yoyote Nchi za Afrika, Latini Amerika na Asia zinaendelea kubaki masikini ili kufanya kuwa jalala la bidhaa duni na mifano mibaya kwa Wananchi wao.

Tatu, Ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa, usafiri wa anga na mtandao thabiti wa barabara Nchi nzima.

Wamagaribi wanatambua matokea ya kuimarisha njia kuu za usafiri na pia wanatambua ni kwa jinsi gani wao wamepiga hatua kubwa kutokana na mchango wa njia za usafirishaji. Hiki kinachofanyika leo hapa Tanzania hakiwapendezi kwa maana sheria yao na msimamo wao mkuu ni kwamba " Don't Ignore the light smoke as may turn to a big fire", hivyo msimamo wao ni kuzima kila chembe ya moshi wauonao na Tanzania ni miongoni.

Nne, ni kubadilisha sheria za madini. Hii haijawahi tokea katika mataifa mengi ya Afrika, Asia na Latini Amerika ila Tanzania imetokea katika Serikali hii ya awamu ya Tano. Si jambo la kawaida kukemea kwa sauti kuwa "Nyie ni Wezi" na tunataka usawa katika nchi yetu na kila kipatikanacho katika ardhi ya Tanzania ni mali yetu na tunahaki ya kugawana sawa.

Hakika hiki si kitu cha kawaida na mpaka sasa Wamagharibi wanaendelea na mkakati madhubuti wa kulipiza kwa madai ya kuwadhalilisha kwa kuwakemea hadharini kwa kuwa hawajazoea kuambiwa ukweli kutokana na ukubwa waliojijengea na kuwajaza hofu watawala wa Mataifa mengi ya Dunia ya Tatu.

Kutokana na mwenendo huo wa Tanzania kimataifa, ni lazima sisi Watanzania tujiandae kukabiliana na mbinu chafu za kutugawa ambazo zimewezekana katika Mataifa mbalimbali.

Kuna njia kuu tano zinazoweza kutumika kutugombanisha na kutufanya tuingie katika mapambano ya wenyewe kwa wenyewe.

Moja, ni kuunga mkono Chama Kikuu cha Upinzani na kukipatia uwezo wa kifedha ili kukabiliana na Chama tawala. Hii hufanyika kwa kukipa fedha kwa masharti kuwa endapo watafanikiwa kuangusha utawala watashirikishwa kuunda Serikali kwa mujibu ya matakwa yao. Imefanyika hivo katika mataifa mengi ya Latini Amerika mfano South Vietinam mwaka 1963 ambapo kundi dogo la upinzani lilipatiwa fedha na kulaghai Wavietnam hususani vijana, Pia ilitokea hivo hivo Brazili na Guatemala. Sisemi wamefanya hivo ila ni lazima kama Watanzania tuwe makini kufuatilia mienendo ya Vyama vya Siasa katika kipindi hichi tunapokabiliana na mapambano ya Kiuchumi na Mataifa makubwa.

Pili, Mauaji ya Viongozi thabiti na wenye msimamo. Hii hufanyika pale ambapo inatokea kiongozi kuwa na ushawishi mkubwa na hata kushindwa kupandikiza upinzani.
Hii ilitokea kwa Bw. Patrice Lumumba Mwaka 1961 kule Katanga na kusababisha Taifa hilo kutokuweza kutawalika mpaka sasa, vilevile iliweza kufanyika Ghana mwaka 1966 pale alipouawa Mzee wetu Kwame Nkurumah. Lakini pia Mataifa haya makubwa hutumia njia ya kuteka ama kuua wanasiasa maarufu, waandishi wa habari, viongozi wa dini na hata wanafunzi ili kuonesha kuwa utawala uliopo madarakani umeshindwa kulinda raia wake ama pia kuonesha hakuna utawala wa Demokrasia.

Njia ya Tatu ni kudumaza uchumi wa Taifa yaani kuweka Vikwazo katika maeneo muhimu ya kiuchumi. Njia hii hutumika sana na Mataifa ya Mahharibi ili kushinikiza kuangusha utawala ama utawala uliopo ukubaliane na mashariti ya kinyonyaji. Inaweza kuwa vikwazo vya kiuchumi katika Usafirishaji, uuzaji bidhaa nje kama nchi inapiga hatua za viwanda, mfano Taifa la la Chile mwaka 1973 ilifanyika hivo na kufanikiwa kuangusha utawala kwa maisha kuwa magumu na kuwapa nafasi Wapinzani kuipindua Serikali, Kinachoendelea kufanyika pale Korea ya Kaskazini ni moja ya mifano dhahiri.

Lakini pia mbali na kilichofanyika Chile na kinachoendelea kufanyika Korea ya kaskazini pia inaweza kufanyika taratibu ikiwa ni pamoja na kuzuia mali za nchi husika kwa kisingizio cha madeni wakati Taifa linaloongoza kwa kudaiwa Duniani ni Marekani ila haijawahi tokea akazuiliwa kuchukuwa mali ama bidhaa zake kutoka nchi fulani kwa sababu ya madeni.

Mbinu ya Nne, hii ni kutumia Vyombo vya habari na dini. ( MeDiaProPaGanDa ) hufanyika kwa kununua Makampuni ya Magazeti, Vituo vya Televisheni na Radio na wakati mwingine kirahisi kabisa huwanunua waandishi wa Habari na kuwawekea mifumo ya mishahara isiyo rasmi kwa kazi wanayoifanya ya kubadili ufikiri wa Wananchi kwa kuandika wakitakacho Wamagharibi.

Dini kwa kiasi kikubwa pia hutumika kwa kuwashawishi baadhi ya viongozi wa dini wenye ushawishi kuhubiri chuki dhidi ya utawala uliopo madarakani, yote hii huwa ni mbinu mahususi ya kubadili ufikiri wa wananchi maana viongozi wengi wa dini kwa asili huaminiwa na wakisemacho waumini huamini kumbe baadhi yao huwa ni mpango na mkakati wa kuingusha Serikali.

Mbinu hii kutumia dini na vyombo vya habari kwa sasa inashika hatamu kwa kiasi kikubwa ikiwa na lengo la kubadili mtazamo wa wananchi wa maeneo lengwa kwa kutumia muda mwingi kueleza mabaya pekee yasiyo halisi ya nchi za Afrika hususani Tanzania kwa sasa.

Mfano Vituo vingi vya Televisheni vya kimataifa kwa sasa wamepewa jukumu la kuzishambuliwa Nchi za Afrika zote zenye kuchukua jitihada ya kujikomboa kiuchumi ikiwepo Tanzania kwa kueleza mabaya kwa wingi pasipo uhalisia ili Wananchi husika wapoteze imani na uongozi.

Mbali na vituo vya kimataifa pia kuna baadhi ya vituo vya ndani na waandishi binafsi hulipwa pesa na kazi yao kubwa ni kukosoa kwenye kila jambo ili kubadili mtazamo wa wananchi dhidi ya Serikali yao. Mbali na Vyombo vya habari lakini pia kuna watu hudhaminiwa kufungua kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii mfano Twitter, Facebook na Instagram kwa ajili ya kusambaza taarifa za chuki na uongo kwa wananchi dhidi ya Serikali yao.

Na hili hufanyika kwa kuwa wameshatambua nguvu kubwa kwa sasa ipo katika Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Njia tano ni Kutengeneza Vurugu, maandamano na migomo. Hili hufanyika kwa ustadi mkubwa na zaidi hufanyika kwa kuwapumbaza wananchi wakaingia katika maandamano wakiwa hawajui kiundani hasa wanahitaji nini ama madai yao ni yapi dhidi ya Serikali iliyopo madarakani. Njia hii isipodhibitiwa huangusha serikali kwa maana ikatokea waandamaji wakawa wengi zaidi katika mji mmoja wanaweza kuwashinda polisi na wakaanza kufanya uhalifu, kuchoma maduka, majumba makubwa na kuchoma matairi ya gari barabarani huku wakiimba nyimbo za hamasa hatimaye Nchi inaingia katika Vurugu na hatimaye kung'oa utawala wa Haki.

Mbinu hii imewahi fanyika katika nchi kadhaa ikafanikiwa na kwa nchi thabiti ilishindwa na kwa sasa imebaki kumbukumbu kwa vizazi na vizazi.

Hii imewahi fanyika mataifa ya Misri, Libya, Iraq na ilifanimiwa miaka ya 2000 na 2010 na kwa sasa kinachoendelea kufanyika Syria ni muendelezo wa mbinu hizi chafu za Wamagharibi. Miaka ya 1970 walitaka wajaribu katika Taifa thabiti la Uchina ila Mao alisimama imara na Vijana maelfu walipoteza maisha kwa kusagwa na vifaru na sasa ni kumbukumbu njema inamulika na kuangaza kwa Taifa hilo kubwa lenye mafanikio thabiti ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Rai yangu kwa Watanzania wote wazalendo wa Taifa hili, Nchi haijengwi kwa mkate na asali ila hujengwa kwa kukubali kujikana, kukataa Unyonyaji, kuchagua Utanzania kuwa kipaumbele na kuamini kuwa kila mmoja ni mdogo kuliko Tanzania na zaidi kutambua kuwa Tanzania kuna Utawala thabiti wenye lengo la kutufikisha mahala ambapo hata vizazi vyetu havitokuja kutulaumu na kutudharau.

Yeyote anayecheza na Amani ya Nchi yetu huyo ni Adui yetu namba moja. Ni heri akatangulia kutuandalia makazi ya milele kuliko kutuchafulia Tanzania.

Tanzania ni kubwa na Nzuri kuliko mimi na wewe.

Tutunze amani yetu
Tulinde Utawala wetu.
Tunatafutwa
Ni vema tushikamane.

Imeandaliwa na;
Said Said Nguya.
 
1.Hivi CAG kusemaje?
2. Hivi sisi wenye amani na hizo nchi zisizo na amani uchumi upi upo chini?
3.
4.
5.
 
Vipi umefikiria juu
Na Said Said Nguya
Kutoka Nzasa Dodoma.

Leo ninawaletea makala fupi yenye lengo la kukufahamisha wewe Mtanzania namna mbinu chafu za Wamagharibi( Marekani & Ulaya) zinavyotumika katika nchi nyingi za Afrika, Latini Amerika na Asia kuangusha Utawala uendao kinyume na matakwa yao.

Nchi za Marekani na Ulaya kwa asili yao ni nchi za Kibepari na msingi mkuu wa Ubepari ni unyonyaji katika kile kiitwacho mwenye nguvu na apate ( Suvival for the Fittest ).

Kutokana na msingi huo mkuu wa Ubepari Mataifa haya hufanya kila mbinu kuhakikisha Nchi za Afrika, Asia na Latini Amerika kuwa na viongozi wanaowanyeyekea na wenye ulimbukeni wa Ulaya na Amerika ya Marekani ili iwe rahisi kuwalaghai na Unyonyaji uendelee kutamalaki na kuota mizizi zaidi.

Inapotokea Nchi imempata kiongozi ambaye kwa namna yoyote, matendo yake, kauli zake na hulka yake haiendani na matakwa yao yaani anakuwa kizuizi kati ya Taifa hilo na malengo ya Maperari ambayo ni Unyonyaji, Nchi hiyo aidha ya Latini Amerika, Asia ama Afrika hujikuta katika wakati mgumu kuendesha utawala wake kwa maana Mabepari huanza kutumia mbinu mbali mbali kuuangusha utawala huo thabiti.

Hakika nasikitika kuona Tanzania tumeingia rasmi kwenye Mgogoro huo na Wamagharibi lakini zaidi nasikitika kuona baadhi ya Watanzania wakiungana nao kwa wengi kutokukujua na wachache kwa kujua kutokana na maslahi binafsi kwanza.

Tanzania kupitia uongozi huu wa Awamu ya Tano umejinasibu kwa vitendo, hulka na maneno kuwa haukubaliani na Unyonyaji wa aina yoyote kwa Taifa letu kwa kufanya mambo kadhaa.

Kwanza, ni kufuta Safari zote za nje zisizo na tija kwa Watanzania ambazo kwa kiasi kikubwa zilikuwa zikifanywa na viongozi wa Serikali, Bunge na Mahakama na hii ilikuwa inatumika kama njia mojawapo ya kuwashawishi viongozi hao kukubaliana na matakwa mbalimbali wakiwa huko ughaibuni kwa maana ni rahisi zidi kumshawishi mtu akiwa nyumbani kwako kuliko akiwa nyumbani kwake. Hii kwa kiasi kikubwa imewanyima fursa nyeti Mabepari ya kukutana mara kwa mara na viongozi wenye dhamana ya maamuzi hapa Tanzania.

Pili, ni namna Serikali ya awamu ya tano inavyoshughulika na wala rushwa na inavyopambana kukemea na kutokomeza ufisadi.

Kiukweli hakuna Taifa lolote la Magharibi linalotamani Tanzania tuwe ni moja ya mifano bora katika jambo lolote kwa kuwa wanatambua kwa sisi kuwa bora katika kupambana na rushwa itakuwa ndio njia ya sisi kupiga hatua za kimaendeleo na kuondokana na umasikini kwa sababu umasikini kwa kiasi kikubwa hutokana na ubadhirifu wa mali za umma ( Ufisadi & Rushwa ), wakati mpango wa "Siri" wa Mataifa ya Magharibi ni kuhakikisha kwa namna yoyote Nchi za Afrika, Latini Amerika na Asia zinaendelea kubaki masikini ili kufanya kuwa jalala la bidhaa duni na mifano mibaya kwa Wananchi wao.

Tatu, Ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa, usafiri wa anga na mtandao thabiti wa barabara Nchi nzima.

Wamagaribi wanatambua matokea ya kuimarisha njia kuu za usafiri na pia wanatambua ni kwa jinsi gani wao wamepiga hatua kubwa kutokana na mchango wa njia za usafirishaji. Hiki kinachofanyika leo hapa Tanzania hakiwapendezi kwa maana sheria yao na msimamo wao mkuu ni kwamba " Don't Ignore the light smoke as may turn to a big fire", hivyo msimamo wao ni kuzima kila chembe ya moshi wauonao na Tanzania ni miongoni.

Nne, ni kubadilisha sheria za madini. Hii haijawahi tokea katika mataifa mengi ya Afrika, Asia na Latini Amerika ila Tanzania imetokea katika Serikali hii ya awamu ya Tano. Si jambo la kawaida kukemea kwa sauti kuwa "Nyie ni Wezi" na tunataka usawa katika nchi yetu na kila kipatikanacho katika ardhi ya Tanzania ni mali yetu na tunahaki ya kugawana sawa.

Hakika hiki si kitu cha kawaida na mpaka sasa Wamagharibi wanaendelea na mkakati madhubuti wa kulipiza kwa madai ya kuwadhalilisha kwa kuwakemea hadharini kwa kuwa hawajazoea kuambiwa ukweli kutokana na ukubwa waliojijengea na kuwajaza hofu watawala wa Mataifa mengi ya Dunia ya Tatu.

Kutokana na mwenendo huo wa Tanzania kimataifa, ni lazima sisi Watanzania tujiandae kukabiliana na mbinu chafu za kutugawa ambazo zimewezekana katika Mataifa mbalimbali.

Kuna njia kuu tano zinazoweza kutumika kutugombanisha na kutufanya tuingie katika mapambano ya wenyewe kwa wenyewe.

Moja, ni kuunga mkono Chama Kikuu cha Upinzani na kukipatia uwezo wa kifedha ili kukabiliana na Chama tawala. Hii hufanyika kwa kukipa fedha kwa masharti kuwa endapo watafanikiwa kuangusha utawala watashirikishwa kuunda Serikali kwa mujibu ya matakwa yao. Imefanyika hivo katika mataifa mengi ya Latini Amerika mfano South Vietinam mwaka 1963 ambapo kundi dogo la upinzani lilipatiwa fedha na kulaghai Wavietnam hususani vijana, Pia ilitokea hivo hivo Brazili na Guatemala. Sisemi wamefanya hivo ila ni lazima kama Watanzania tuwe makini kufuatilia mienendo ya Vyama vya Siasa katika kipindi hichi tunapokabiliana na mapambano ya Kiuchumi na Mataifa makubwa.

Pili, Mauaji ya Viongozi thabiti na wenye msimamo. Hii hufanyika pale ambapo inatokea kiongozi kuwa na ushawishi mkubwa na hata kushindwa kupandikiza upinzani.
Hii ilitokea kwa Bw. Patrice Lumumba Mwaka 1961 kule Katanga na kusababisha Taifa hilo kutokuweza kutawalika mpaka sasa, vilevile iliweza kufanyika Ghana mwaka 1966 pale alipouawa Mzee wetu Kwame Nkurumah. Lakini pia Mataifa haya makubwa hutumia njia ya kuteka ama kuua wanasiasa maarufu, waandishi wa habari, viongozi wa dini na hata wanafunzi ili kuonesha kuwa utawala uliopo madarakani umeshindwa kulinda raia wake ama pia kuonesha hakuna utawala wa Demokrasia.

Njia ya Tatu ni kudumaza uchumi wa Taifa yaani kuweka Vikwazo katika maeneo muhimu ya kiuchumi. Njia hii hutumika sana na Mataifa ya Mahharibi ili kushinikiza kuangusha utawala ama utawala uliopo ukubaliane na mashariti ya kinyonyaji. Inaweza kuwa vikwazo vya kiuchumi katika Usafirishaji, uuzaji bidhaa nje kama nchi inapiga hatua za viwanda, mfano Taifa la la Chile mwaka 1973 ilifanyika hivo na kufanikiwa kuangusha utawala kwa maisha kuwa magumu na kuwapa nafasi Wapinzani kuipindua Serikali, Kinachoendelea kufanyika pale Korea ya Kaskazini ni moja ya mifano dhahiri.

Lakini pia mbali na kilichofanyika Chile na kinachoendelea kufanyika Korea ya kaskazini pia inaweza kufanyika taratibu ikiwa ni pamoja na kuzuia mali za nchi husika kwa kisingizio cha madeni wakati Taifa linaloongoza kwa kudaiwa Duniani ni Marekani ila haijawahi tokea akazuiliwa kuchukuwa mali ama bidhaa zake kutoka nchi fulani kwa sababu ya madeni.

Mbinu ya Nne, hii ni kutumia Vyombo vya habari na dini. ( MeDiaProPaGanDa ) hufanyika kwa kununua Makampuni ya Magazeti, Vituo vya Televisheni na Radio na wakati mwingine kirahisi kabisa huwanunua waandishi wa Habari na kuwawekea mifumo ya mishahara isiyo rasmi kwa kazi wanayoifanya ya kubadili ufikiri wa Wananchi kwa kuandika wakitakacho Wamagharibi.

Dini kwa kiasi kikubwa pia hutumika kwa kuwashawishi baadhi ya viongozi wa dini wenye ushawishi kuhubiri chuki dhidi ya utawala uliopo madarakani, yote hii huwa ni mbinu mahususi ya kubadili ufikiri wa wananchi maana viongozi wengi wa dini kwa asili huaminiwa na wakisemacho waumini huamini kumbe baadhi yao huwa ni mpango na mkakati wa kuingusha Serikali.

Mbinu hii kutumia dini na vyombo vya habari kwa sasa inashika hatamu kwa kiasi kikubwa ikiwa na lengo la kubadili mtazamo wa wananchi wa maeneo lengwa kwa kutumia muda mwingi kueleza mabaya pekee yasiyo halisi ya nchi za Afrika hususani Tanzania kwa sasa.

Mfano Vituo vingi vya Televisheni vya kimataifa kwa sasa wamepewa jukumu la kuzishambuliwa Nchi za Afrika zote zenye kuchukua jitihada ya kujikomboa kiuchumi ikiwepo Tanzania kwa kueleza mabaya kwa wingi pasipo uhalisia ili Wananchi husika wapoteze imani na uongozi.

Mbali na vituo vya kimataifa pia kuna baadhi ya vituo vya ndani na waandishi binafsi hulipwa pesa na kazi yao kubwa ni kukosoa kwenye kila jambo ili kubadili mtazamo wa wananchi dhidi ya Serikali yao. Mbali na Vyombo vya habari lakini pia kuna watu hudhaminiwa kufungua kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii mfano Twitter, Facebook na Instagram kwa ajili ya kusambaza taarifa za chuki na uongo kwa wananchi dhidi ya Serikali yao.

Na hili hufanyika kwa kuwa wameshatambua nguvu kubwa kwa sasa ipo katika Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Njia tano ni Kutengeneza Vurugu, maandamano na migomo. Hili hufanyika kwa ustadi mkubwa na zaidi hufanyika kwa kuwapumbaza wananchi wakaingia katika maandamano wakiwa hawajui kiundani hasa wanahitaji nini ama madai yao ni yapi dhidi ya Serikali iliyopo madarakani. Njia hii isipodhibitiwa huangusha serikali kwa maana ikatokea waandamaji wakawa wengi zaidi katika mji mmoja wanaweza kuwashinda polisi na wakaanza kufanya uhalifu, kuchoma maduka, majumba makubwa na kuchoma matairi ya gari barabarani huku wakiimba nyimbo za hamasa hatimaye Nchi inaingia katika Vurugu na hatimaye kung'oa utawala wa Haki.

Mbinu hii imewahi fanyika katika nchi kadhaa ikafanikiwa na kwa nchi thabiti ilishindwa na kwa sasa imebaki kumbukumbu kwa vizazi na vizazi.

Hii imewahi fanyika mataifa ya Misri, Libya, Iraq na ilifanimiwa miaka ya 2000 na 2010 na kwa sasa kinachoendelea kufanyika Syria ni muendelezo wa mbinu hizi chafu za Wamagharibi. Miaka ya 1970 walitaka wajaribu katika Taifa thabiti la Uchina ila Mao alisimama imara na Vijana maelfu walipoteza maisha kwa kusagwa na vifaru na sasa ni kumbukumbu njema inamulika na kuangaza kwa Taifa hilo kubwa lenye mafanikio thabiti ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Rai yangu kwa Watanzania wote wazalendo wa Taifa hili, Nchi haijengwi kwa mkate na asali ila hujengwa kwa kukubali kujikana, kukataa Unyonyaji, kuchagua Utanzania kuwa kipaumbele na kuamini kuwa kila mmoja ni mdogo kuliko Tanzania na zaidi kutambua kuwa Tanzania kuna Utawala thabiti wenye lengo la kutufikisha mahala ambapo hata vizazi vyetu havitokuja kutulaumu na kutudharau.

Yeyote anayecheza na Amani ya Nchi yetu huyo ni Adui yetu namba moja. Ni heri akatangulia kutuandalia makazi ya milele kuliko kutuchafulia Tanzania.

Tanzania ni kubwa na Nzuri kuliko mimi na wewe.Tutunze amani yetu, Tulinde Utawala wetu.Tunatafutwa, Ni vema tushikamane.
Ya kupandikiza watu ndani ya nchi wanakulia humo na wanaua uchumi. Moles.
 
USA walishatuzoea vibaya walitegemea Rais JPM mara akipishwa tu akwee pipa kwenda kupiga picha na boyz mbili men, kipindi hiki wamenoa ile kutudanganya na misaada ya vyandarua wasahau. Halafu vyandarua vingine vitumike kufugia vifaranga wasipitiwe na mwewe, wasahau.
Wanatupiga tu hatuna ujanja watatumia hata Rafiki kushawishi aachie. Huwezi uza bidhaa yeyote duniani bila kibali cha marekani. Juzi tu mmefyata mitumba
 
Mkuu umenena hawa watu waliokuwa walifaidi kutajirika kwa mfumo wa ufisadi hawatawacha kulalamika ama kuhujumu serikali ya awamu ya tano. Mfano Rais mstaafu wa Brazil amefungwa jela kwa njama za hawahawa mabeberu baada ya kuona ana nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi mkuu ujao. Ni muhimu kwa watanzania kuwa macho na wanasiasa na vyama vinavyotaka kutumika kuharibu amani yetu.
I saw this on the BBC and thought you should see it:

How President Lula changed Brazil - How President Lula changed Brazil
 
Na Said Said Nguya
Kutoka Nzasa Dodoma.

Leo ninawaletea makala fupi yenye lengo la kukufahamisha wewe Mtanzania namna mbinu chafu za Wamagharibi( Marekani & Ulaya) zinavyotumika katika nchi nyingi za Afrika, Latini Amerika na Asia kuangusha Utawala uendao kinyume na matakwa yao.

Nchi za Marekani na Ulaya kwa asili yao ni nchi za Kibepari na msingi mkuu wa Ubepari ni unyonyaji katika kile kiitwacho mwenye nguvu na apate ( Suvival for the Fittest ).

Kutokana na msingi huo mkuu wa Ubepari Mataifa haya hufanya kila mbinu kuhakikisha Nchi za Afrika, Asia na Latini Amerika kuwa na viongozi wanaowanyeyekea na wenye ulimbukeni wa Ulaya na Amerika ya Marekani ili iwe rahisi kuwalaghai na Unyonyaji uendelee kutamalaki na kuota mizizi zaidi.

Inapotokea Nchi imempata kiongozi ambaye kwa namna yoyote, matendo yake, kauli zake na hulka yake haiendani na matakwa yao yaani anakuwa kizuizi kati ya Taifa hilo na malengo ya Maperari ambayo ni Unyonyaji, Nchi hiyo aidha ya Latini Amerika, Asia ama Afrika hujikuta katika wakati mgumu kuendesha utawala wake kwa maana Mabepari huanza kutumia mbinu mbali mbali kuuangusha utawala huo thabiti.

Hakika nasikitika kuona Tanzania tumeingia rasmi kwenye Mgogoro huo na Wamagharibi lakini zaidi nasikitika kuona baadhi ya Watanzania wakiungana nao kwa wengi kutokukujua na wachache kwa kujua kutokana na maslahi binafsi kwanza.

Tanzania kupitia uongozi huu wa Awamu ya Tano umejinasibu kwa vitendo, hulka na maneno kuwa haukubaliani na Unyonyaji wa aina yoyote kwa Taifa letu kwa kufanya mambo kadhaa.

Kwanza, ni kufuta Safari zote za nje zisizo na tija kwa Watanzania ambazo kwa kiasi kikubwa zilikuwa zikifanywa na viongozi wa Serikali, Bunge na Mahakama na hii ilikuwa inatumika kama njia mojawapo ya kuwashawishi viongozi hao kukubaliana na matakwa mbalimbali wakiwa huko ughaibuni kwa maana ni rahisi zidi kumshawishi mtu akiwa nyumbani kwako kuliko akiwa nyumbani kwake. Hii kwa kiasi kikubwa imewanyima fursa nyeti Mabepari ya kukutana mara kwa mara na viongozi wenye dhamana ya maamuzi hapa Tanzania.

Pili, ni namna Serikali ya awamu ya tano inavyoshughulika na wala rushwa na inavyopambana kukemea na kutokomeza ufisadi.

Kiukweli hakuna Taifa lolote la Magharibi linalotamani Tanzania tuwe ni moja ya mifano bora katika jambo lolote kwa kuwa wanatambua kwa sisi kuwa bora katika kupambana na rushwa itakuwa ndio njia ya sisi kupiga hatua za kimaendeleo na kuondokana na umasikini kwa sababu umasikini kwa kiasi kikubwa hutokana na ubadhirifu wa mali za umma ( Ufisadi & Rushwa ), wakati mpango wa "Siri" wa Mataifa ya Magharibi ni kuhakikisha kwa namna yoyote Nchi za Afrika, Latini Amerika na Asia zinaendelea kubaki masikini ili kufanya kuwa jalala la bidhaa duni na mifano mibaya kwa Wananchi wao.

Tatu, Ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa, usafiri wa anga na mtandao thabiti wa barabara Nchi nzima.

Wamagaribi wanatambua matokea ya kuimarisha njia kuu za usafiri na pia wanatambua ni kwa jinsi gani wao wamepiga hatua kubwa kutokana na mchango wa njia za usafirishaji. Hiki kinachofanyika leo hapa Tanzania hakiwapendezi kwa maana sheria yao na msimamo wao mkuu ni kwamba " Don't Ignore the light smoke as may turn to a big fire", hivyo msimamo wao ni kuzima kila chembe ya moshi wauonao na Tanzania ni miongoni.

Nne, ni kubadilisha sheria za madini. Hii haijawahi tokea katika mataifa mengi ya Afrika, Asia na Latini Amerika ila Tanzania imetokea katika Serikali hii ya awamu ya Tano. Si jambo la kawaida kukemea kwa sauti kuwa "Nyie ni Wezi" na tunataka usawa katika nchi yetu na kila kipatikanacho katika ardhi ya Tanzania ni mali yetu na tunahaki ya kugawana sawa.

Hakika hiki si kitu cha kawaida na mpaka sasa Wamagharibi wanaendelea na mkakati madhubuti wa kulipiza kwa madai ya kuwadhalilisha kwa kuwakemea hadharini kwa kuwa hawajazoea kuambiwa ukweli kutokana na ukubwa waliojijengea na kuwajaza hofu watawala wa Mataifa mengi ya Dunia ya Tatu.

Kutokana na mwenendo huo wa Tanzania kimataifa, ni lazima sisi Watanzania tujiandae kukabiliana na mbinu chafu za kutugawa ambazo zimewezekana katika Mataifa mbalimbali.

Kuna njia kuu tano zinazoweza kutumika kutugombanisha na kutufanya tuingie katika mapambano ya wenyewe kwa wenyewe.

Moja, ni kuunga mkono Chama Kikuu cha Upinzani na kukipatia uwezo wa kifedha ili kukabiliana na Chama tawala. Hii hufanyika kwa kukipa fedha kwa masharti kuwa endapo watafanikiwa kuangusha utawala watashirikishwa kuunda Serikali kwa mujibu ya matakwa yao. Imefanyika hivo katika mataifa mengi ya Latini Amerika mfano South Vietinam mwaka 1963 ambapo kundi dogo la upinzani lilipatiwa fedha na kulaghai Wavietnam hususani vijana, Pia ilitokea hivo hivo Brazili na Guatemala. Sisemi wamefanya hivo ila ni lazima kama Watanzania tuwe makini kufuatilia mienendo ya Vyama vya Siasa katika kipindi hichi tunapokabiliana na mapambano ya Kiuchumi na Mataifa makubwa.

Pili, Mauaji ya Viongozi thabiti na wenye msimamo. Hii hufanyika pale ambapo inatokea kiongozi kuwa na ushawishi mkubwa na hata kushindwa kupandikiza upinzani.
Hii ilitokea kwa Bw. Patrice Lumumba Mwaka 1961 kule Katanga na kusababisha Taifa hilo kutokuweza kutawalika mpaka sasa, vilevile iliweza kufanyika Ghana mwaka 1966 pale alipouawa Mzee wetu Kwame Nkurumah. Lakini pia Mataifa haya makubwa hutumia njia ya kuteka ama kuua wanasiasa maarufu, waandishi wa habari, viongozi wa dini na hata wanafunzi ili kuonesha kuwa utawala uliopo madarakani umeshindwa kulinda raia wake ama pia kuonesha hakuna utawala wa Demokrasia.

Njia ya Tatu ni kudumaza uchumi wa Taifa yaani kuweka Vikwazo katika maeneo muhimu ya kiuchumi. Njia hii hutumika sana na Mataifa ya Mahharibi ili kushinikiza kuangusha utawala ama utawala uliopo ukubaliane na mashariti ya kinyonyaji. Inaweza kuwa vikwazo vya kiuchumi katika Usafirishaji, uuzaji bidhaa nje kama nchi inapiga hatua za viwanda, mfano Taifa la la Chile mwaka 1973 ilifanyika hivo na kufanikiwa kuangusha utawala kwa maisha kuwa magumu na kuwapa nafasi Wapinzani kuipindua Serikali, Kinachoendelea kufanyika pale Korea ya Kaskazini ni moja ya mifano dhahiri.

Lakini pia mbali na kilichofanyika Chile na kinachoendelea kufanyika Korea ya kaskazini pia inaweza kufanyika taratibu ikiwa ni pamoja na kuzuia mali za nchi husika kwa kisingizio cha madeni wakati Taifa linaloongoza kwa kudaiwa Duniani ni Marekani ila haijawahi tokea akazuiliwa kuchukuwa mali ama bidhaa zake kutoka nchi fulani kwa sababu ya madeni.

Mbinu ya Nne, hii ni kutumia Vyombo vya habari na dini. ( MeDiaProPaGanDa ) hufanyika kwa kununua Makampuni ya Magazeti, Vituo vya Televisheni na Radio na wakati mwingine kirahisi kabisa huwanunua waandishi wa Habari na kuwawekea mifumo ya mishahara isiyo rasmi kwa kazi wanayoifanya ya kubadili ufikiri wa Wananchi kwa kuandika wakitakacho Wamagharibi.

Dini kwa kiasi kikubwa pia hutumika kwa kuwashawishi baadhi ya viongozi wa dini wenye ushawishi kuhubiri chuki dhidi ya utawala uliopo madarakani, yote hii huwa ni mbinu mahususi ya kubadili ufikiri wa wananchi maana viongozi wengi wa dini kwa asili huaminiwa na wakisemacho waumini huamini kumbe baadhi yao huwa ni mpango na mkakati wa kuingusha Serikali.

Mbinu hii kutumia dini na vyombo vya habari kwa sasa inashika hatamu kwa kiasi kikubwa ikiwa na lengo la kubadili mtazamo wa wananchi wa maeneo lengwa kwa kutumia muda mwingi kueleza mabaya pekee yasiyo halisi ya nchi za Afrika hususani Tanzania kwa sasa.

Mfano Vituo vingi vya Televisheni vya kimataifa kwa sasa wamepewa jukumu la kuzishambuliwa Nchi za Afrika zote zenye kuchukua jitihada ya kujikomboa kiuchumi ikiwepo Tanzania kwa kueleza mabaya kwa wingi pasipo uhalisia ili Wananchi husika wapoteze imani na uongozi.

Mbali na vituo vya kimataifa pia kuna baadhi ya vituo vya ndani na waandishi binafsi hulipwa pesa na kazi yao kubwa ni kukosoa kwenye kila jambo ili kubadili mtazamo wa wananchi dhidi ya Serikali yao. Mbali na Vyombo vya habari lakini pia kuna watu hudhaminiwa kufungua kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii mfano Twitter, Facebook na Instagram kwa ajili ya kusambaza taarifa za chuki na uongo kwa wananchi dhidi ya Serikali yao.

Na hili hufanyika kwa kuwa wameshatambua nguvu kubwa kwa sasa ipo katika Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Njia tano ni Kutengeneza Vurugu, maandamano na migomo. Hili hufanyika kwa ustadi mkubwa na zaidi hufanyika kwa kuwapumbaza wananchi wakaingia katika maandamano wakiwa hawajui kiundani hasa wanahitaji nini ama madai yao ni yapi dhidi ya Serikali iliyopo madarakani. Njia hii isipodhibitiwa huangusha serikali kwa maana ikatokea waandamaji wakawa wengi zaidi katika mji mmoja wanaweza kuwashinda polisi na wakaanza kufanya uhalifu, kuchoma maduka, majumba makubwa na kuchoma matairi ya gari barabarani huku wakiimba nyimbo za hamasa hatimaye Nchi inaingia katika Vurugu na hatimaye kung'oa utawala wa Haki.

Mbinu hii imewahi fanyika katika nchi kadhaa ikafanikiwa na kwa nchi thabiti ilishindwa na kwa sasa imebaki kumbukumbu kwa vizazi na vizazi.

Hii imewahi fanyika mataifa ya Misri, Libya, Iraq na ilifanimiwa miaka ya 2000 na 2010 na kwa sasa kinachoendelea kufanyika Syria ni muendelezo wa mbinu hizi chafu za Wamagharibi. Miaka ya 1970 walitaka wajaribu katika Taifa thabiti la Uchina ila Mao alisimama imara na Vijana maelfu walipoteza maisha kwa kusagwa na vifaru na sasa ni kumbukumbu njema inamulika na kuangaza kwa Taifa hilo kubwa lenye mafanikio thabiti ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Rai yangu kwa Watanzania wote wazalendo wa Taifa hili, Nchi haijengwi kwa mkate na asali ila hujengwa kwa kukubali kujikana, kukataa Unyonyaji, kuchagua Utanzania kuwa kipaumbele na kuamini kuwa kila mmoja ni mdogo kuliko Tanzania na zaidi kutambua kuwa Tanzania kuna Utawala thabiti wenye lengo la kutufikisha mahala ambapo hata vizazi vyetu havitokuja kutulaumu na kutudharau.

Yeyote anayecheza na Amani ya Nchi yetu huyo ni Adui yetu namba moja. Ni heri akatangulia kutuandalia makazi ya milele kuliko kutuchafulia Tanzania.

Tanzania ni kubwa na Nzuri kuliko mimi na wewe.Tutunze amani yetu, Tulinde Utawala wetu.Tunatafutwa, Ni vema tushikamane.
stori yako imekaa kisiasa sana na kutisha watu kabla ya kuandika unatakiwa utafakari na kuelewa unacho manisha
Njia ya muongo huwa ni ndefu. Hakika wahenga walikosea. Maelezo yako marefu yanaonesha uongo wako.

Watanzania hawahitaji mmarekani kujua kuwa kunawatu wanatekwa na kuuwawa. Watanzania hawahitaji mmarekani kujua kuwa wamefisadiwa 1.5tr. Watz hawahitaji mmarekani kujua kuwa bei ya sukar imepanda... watanzania hawahitaji mmarekani kujua kuwa serkal inaongoza na vchaa.
Watz hawahitaji mmarekani kujua kuwa mmiliki wa vichwa vya Train ni TRL.

Hayo mawazo ya kupoteza na kutanguliza wengine kwa maslahi ya madaraka ndio kupoteza amani ya nchi.
Mana hakuna kondoo watakaokubali kupotezwa au kupotezewa ndugu zao kila siku ili wengine watawale na famili.
zao zitafune matril. ya fedha.
Kabla ya mali na mareli na majumba Binadamu amepewa roho na mwili mmoja tu na kabla ya kulinda chochote anaanza kulinda roho ya yake.

Haya matamko ya kuua na kumaliza wengine ni mabaya sana na ni hatari kuliko hata yale ya Mange Kimambi. Huu ndio uchochezi wa daraja la kwanza usio na tija kabisa.
Wakati Hao hao CCM walipokua wanaliibia taifa kwa wazi watu walitumia demokrasia kuwakosoa na sio vitisho na kutishia maisha ya wezi hao.
Leo bado CCM inatunyonya kwa mbinu mpya halafu wanatokea makada uchwara wanahamasisha mauaji na kupoteza wale wale waliokua wanawakosoa tangu awali.
Hivi Mkuu wa Wilaya au mkoa au waziri au balozi au kiongozi wa juu ya chama analipwa mshahara sawa na Mwalimu wa shule ya msingi???
Kwa nini musianze kupambana na huu unyonyaji wa ndani kwa ndani kupitia kodi ya wananchi?
Ambao nao asili yake ni watawala kuiga umagharibi ili hali watawaliwa wakitakiwa wakaze mikanda nchi inajengwa?

Umagharibi ndio uliopo dunia nzima hata udikteta uliasisiwa na hao hao wamagharibi na kwa faida zao na watawala kwenye nchi za Afrika.
 
USA walishatuzoea vibaya walitegemea Rais JPM mara akipishwa tu akwee pipa kwenda kupiga picha na boyz mbili men, kipindi hiki wamenoa ile kutudanganya na misaada ya vyandarua wasahau. Halafu vyandarua vingine vitumike kufugia vifaranga wasipitiwe na mwewe, wasahau.
Lini mmeacha kupokea misaada...? Lini mmeanza kuishi 100% kwa fedha zenu...? Juzi mmezindua JK Foundation pale Ikulu mnafikiri mnaiendesha kwa pesa zenu?
Siamini iwapo kuwa mwana-CCM lazima uwe mpumbavu wakati wote.
 
Una ugonjwa wa hofu ya Magu. Magu anapopoteza watu, anaua, anawasweka ndani upinzani yeye hajui kuwa anaikimbiza amani na watoto ndugu na jamaa na jamii wanaothiriwa na matendo yake wanatakiwa wainame tu. Huelewi kabisa maana ya amani sawa na Magu.

Kabla hujachochewa ama kujichochea mwenyewe kufanya vurugu zozote tafakari.

Anaechochewa ni wewe kueneza upuuzi bila tafakari

1:Je hiki ninacho ambiwa nikipinge ni kweli kina huo uovu?

Ni ujinga kutoona kuwa ni uovu uliokithiri watu wanapotea na hakuna uchunguzi.

2: baada ya kukipinga wewe binafsi utapata faida gani?

Wewe unapoandika upuuzi huu unapata faida gani zaidi ya hasara.

Natumai unaweza ambulia kitu hapa ukitaka.

Sijawahi ona mtu anaambulia ujinga na upuuzi kama wako.
 
Lini mmeacha kupokea misaada...? Lini mmeanza kuishi 100% kwa fedha zenu...? Juzi mmezindua JK Foundation pale Ikulu mnafikiri mnaiendesha kwa pesa zenu?
Siamini iwapo kuwa mwana-CCM lazima uwe mpumbavu wakati wote.

Kama huwezi kuona hata bembea hapa nchini utaona vipi utajiri wa nchi hii? Bembea ikibadilishwa muundo uifuate Costa Blanca. Ndio uerevu huo huko kwenu.
 
Hapa unamuinkludi aliyetumia trilioni moja na nusu kinyume na taratibu? Maana hatuwezi lips Kofi alafu MTU akazitumia isivyoeleweka atakuwa anaihatarisha amani
 
Kama huwezi kuona hata bembea hapa nchini utaona vipi utajiri wa nchi hii? Bembea ikibadilishwa muundo uifuate Costa Blanca. Ndio uerevu huo huko kwenu.
Kichwa changu hakina tongotongo unazotakaniwe nazo, sikatai kujitegemea ila sikubaliana na ujinga wa kujifanya Super Power ili hali back door mnapokea na kufurahia fedha za hao mnaowadharau...
Acha kujitia huna akili...Mungu alituumba akatupa utashi na ufahamu ili tuweze kuyapambanua mambo katika upana wake, acha kujifanya huna huo utashi na ufahamu.
 
Leo ninawaletea makala fupi yenye lengo la kukufahamisha wewe Mtanzania namna mbinu chafu za Wamagharibi( Marekani & Ulaya) zinavyotumika katika nchi nyingi za Afrika, Latini Amerika na Asia kuangusha Utawala uendao kinyume na matakwa yao.

Nchi za Marekani na Ulaya kwa asili yao ni nchi za Kibepari na msingi mkuu wa Ubepari ni unyonyaji katika kile kiitwacho mwenye nguvu na apate ( Suvival for the Fittest ).

Kutokana na msingi huo mkuu wa Ubepari Mataifa haya hufanya kila mbinu kuhakikisha Nchi za Afrika, Asia na Latini Amerika kuwa na viongozi wanaowanyeyekea na wenye ulimbukeni wa Ulaya na Amerika ya Marekani ili iwe rahisi kuwalaghai na Unyonyaji uendelee kutamalaki na kuota mizizi zaidi.

Inapotokea Nchi imempata kiongozi ambaye kwa namna yoyote, matendo yake, kauli zake na hulka yake haiendani na matakwa yao yaani anakuwa kizuizi kati ya Taifa hilo na malengo ya Maperari ambayo ni Unyonyaji, Nchi hiyo aidha ya Latini Amerika, Asia ama Afrika hujikuta katika wakati mgumu kuendesha utawala wake kwa maana Mabepari huanza kutumia mbinu mbali mbali kuuangusha utawala huo thabiti.

Hakika nasikitika kuona Tanzania tumeingia rasmi kwenye Mgogoro huo na Wamagharibi lakini zaidi nasikitika kuona baadhi ya Watanzania wakiungana nao kwa wengi kutokukujua na wachache kwa kujua kutokana na maslahi binafsi kwanza.

Tanzania kupitia uongozi huu wa Awamu ya Tano umejinasibu kwa vitendo, hulka na maneno kuwa haukubaliani na Unyonyaji wa aina yoyote kwa Taifa letu kwa kufanya mambo kadhaa.

Kwanza, ni kufuta Safari zote za nje zisizo na tija kwa Watanzania ambazo kwa kiasi kikubwa zilikuwa zikifanywa na viongozi wa Serikali, Bunge na Mahakama na hii ilikuwa inatumika kama njia mojawapo ya kuwashawishi viongozi hao kukubaliana na matakwa mbalimbali wakiwa huko ughaibuni kwa maana ni rahisi zidi kumshawishi mtu akiwa nyumbani kwako kuliko akiwa nyumbani kwake. Hii kwa kiasi kikubwa imewanyima fursa nyeti Mabepari ya kukutana mara kwa mara na viongozi wenye dhamana ya maamuzi hapa Tanzania.

Pili, ni namna Serikali ya awamu ya tano inavyoshughulika na wala rushwa na inavyopambana kukemea na kutokomeza ufisadi.

Kiukweli hakuna Taifa lolote la Magharibi linalotamani Tanzania tuwe ni moja ya mifano bora katika jambo lolote kwa kuwa wanatambua kwa sisi kuwa bora katika kupambana na rushwa itakuwa ndio njia ya sisi kupiga hatua za kimaendeleo na kuondokana na umasikini kwa sababu umasikini kwa kiasi kikubwa hutokana na ubadhirifu wa mali za umma ( Ufisadi & Rushwa ), wakati mpango wa "Siri" wa Mataifa ya Magharibi ni kuhakikisha kwa namna yoyote Nchi za Afrika, Latini Amerika na Asia zinaendelea kubaki masikini ili kufanya kuwa jalala la bidhaa duni na mifano mibaya kwa Wananchi wao.

Tatu, Ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa, usafiri wa anga na mtandao thabiti wa barabara Nchi nzima.

Wamagaribi wanatambua matokea ya kuimarisha njia kuu za usafiri na pia wanatambua ni kwa jinsi gani wao wamepiga hatua kubwa kutokana na mchango wa njia za usafirishaji. Hiki kinachofanyika leo hapa Tanzania hakiwapendezi kwa maana sheria yao na msimamo wao mkuu ni kwamba " Don't Ignore the light smoke as may turn to a big fire", hivyo msimamo wao ni kuzima kila chembe ya moshi wauonao na Tanzania ni miongoni.

Nne, ni kubadilisha sheria za madini. Hii haijawahi tokea katika mataifa mengi ya Afrika, Asia na Latini Amerika ila Tanzania imetokea katika Serikali hii ya awamu ya Tano. Si jambo la kawaida kukemea kwa sauti kuwa "Nyie ni Wezi" na tunataka usawa katika nchi yetu na kila kipatikanacho katika ardhi ya Tanzania ni mali yetu na tunahaki ya kugawana sawa.

Hakika hiki si kitu cha kawaida na mpaka sasa Wamagharibi wanaendelea na mkakati madhubuti wa kulipiza kwa madai ya kuwadhalilisha kwa kuwakemea hadharini kwa kuwa hawajazoea kuambiwa ukweli kutokana na ukubwa waliojijengea na kuwajaza hofu watawala wa Mataifa mengi ya Dunia ya Tatu.

Kutokana na mwenendo huo wa Tanzania kimataifa, ni lazima sisi Watanzania tujiandae kukabiliana na mbinu chafu za kutugawa ambazo zimewezekana katika Mataifa mbalimbali.

Kuna njia kuu tano zinazoweza kutumika kutugombanisha na kutufanya tuingie katika mapambano ya wenyewe kwa wenyewe.

Moja, ni kuunga mkono Chama Kikuu cha Upinzani na kukipatia uwezo wa kifedha ili kukabiliana na Chama tawala. Hii hufanyika kwa kukipa fedha kwa masharti kuwa endapo watafanikiwa kuangusha utawala watashirikishwa kuunda Serikali kwa mujibu ya matakwa yao. Imefanyika hivo katika mataifa mengi ya Latini Amerika mfano South Vietinam mwaka 1963 ambapo kundi dogo la upinzani lilipatiwa fedha na kulaghai Wavietnam hususani vijana, Pia ilitokea hivo hivo Brazili na Guatemala. Sisemi wamefanya hivo ila ni lazima kama Watanzania tuwe makini kufuatilia mienendo ya Vyama vya Siasa katika kipindi hichi tunapokabiliana na mapambano ya Kiuchumi na Mataifa makubwa.

Pili, Mauaji ya Viongozi thabiti na wenye msimamo. Hii hufanyika pale ambapo inatokea kiongozi kuwa na ushawishi mkubwa na hata kushindwa kupandikiza upinzani.
Hii ilitokea kwa Bw. Patrice Lumumba Mwaka 1961 kule Katanga na kusababisha Taifa hilo kutokuweza kutawalika mpaka sasa, vilevile iliweza kufanyika Ghana mwaka 1966 pale alipouawa Mzee wetu Kwame Nkurumah. Lakini pia Mataifa haya makubwa hutumia njia ya kuteka ama kuua wanasiasa maarufu, waandishi wa habari, viongozi wa dini na hata wanafunzi ili kuonesha kuwa utawala uliopo madarakani umeshindwa kulinda raia wake ama pia kuonesha hakuna utawala wa Demokrasia.

Njia ya Tatu ni kudumaza uchumi wa Taifa yaani kuweka Vikwazo katika maeneo muhimu ya kiuchumi. Njia hii hutumika sana na Mataifa ya Mahharibi ili kushinikiza kuangusha utawala ama utawala uliopo ukubaliane na mashariti ya kinyonyaji. Inaweza kuwa vikwazo vya kiuchumi katika Usafirishaji, uuzaji bidhaa nje kama nchi inapiga hatua za viwanda, mfano Taifa la la Chile mwaka 1973 ilifanyika hivo na kufanikiwa kuangusha utawala kwa maisha kuwa magumu na kuwapa nafasi Wapinzani kuipindua Serikali, Kinachoendelea kufanyika pale Korea ya Kaskazini ni moja ya mifano dhahiri.

Lakini pia mbali na kilichofanyika Chile na kinachoendelea kufanyika Korea ya kaskazini pia inaweza kufanyika taratibu ikiwa ni pamoja na kuzuia mali za nchi husika kwa kisingizio cha madeni wakati Taifa linaloongoza kwa kudaiwa Duniani ni Marekani ila haijawahi tokea akazuiliwa kuchukuwa mali ama bidhaa zake kutoka nchi fulani kwa sababu ya madeni.

Mbinu ya Nne, hii ni kutumia Vyombo vya habari na dini. ( MeDiaProPaGanDa ) hufanyika kwa kununua Makampuni ya Magazeti, Vituo vya Televisheni na Radio na wakati mwingine kirahisi kabisa huwanunua waandishi wa Habari na kuwawekea mifumo ya mishahara isiyo rasmi kwa kazi wanayoifanya ya kubadili ufikiri wa Wananchi kwa kuandika wakitakacho Wamagharibi.

Dini kwa kiasi kikubwa pia hutumika kwa kuwashawishi baadhi ya viongozi wa dini wenye ushawishi kuhubiri chuki dhidi ya utawala uliopo madarakani, yote hii huwa ni mbinu mahususi ya kubadili ufikiri wa wananchi maana viongozi wengi wa dini kwa asili huaminiwa na wakisemacho waumini huamini kumbe baadhi yao huwa ni mpango na mkakati wa kuingusha Serikali.

Mbinu hii kutumia dini na vyombo vya habari kwa sasa inashika hatamu kwa kiasi kikubwa ikiwa na lengo la kubadili mtazamo wa wananchi wa maeneo lengwa kwa kutumia muda mwingi kueleza mabaya pekee yasiyo halisi ya nchi za Afrika hususani Tanzania kwa sasa.

Mfano Vituo vingi vya Televisheni vya kimataifa kwa sasa wamepewa jukumu la kuzishambuliwa Nchi za Afrika zote zenye kuchukua jitihada ya kujikomboa kiuchumi ikiwepo Tanzania kwa kueleza mabaya kwa wingi pasipo uhalisia ili Wananchi husika wapoteze imani na uongozi.

Mbali na vituo vya kimataifa pia kuna baadhi ya vituo vya ndani na waandishi binafsi hulipwa pesa na kazi yao kubwa ni kukosoa kwenye kila jambo ili kubadili mtazamo wa wananchi dhidi ya Serikali yao. Mbali na Vyombo vya habari lakini pia kuna watu hudhaminiwa kufungua kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii mfano Twitter, Facebook na Instagram kwa ajili ya kusambaza taarifa za chuki na uongo kwa wananchi dhidi ya Serikali yao.

Na hili hufanyika kwa kuwa wameshatambua nguvu kubwa kwa sasa ipo katika Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Njia tano ni Kutengeneza Vurugu, maandamano na migomo. Hili hufanyika kwa ustadi mkubwa na zaidi hufanyika kwa kuwapumbaza wananchi wakaingia katika maandamano wakiwa hawajui kiundani hasa wanahitaji nini ama madai yao ni yapi dhidi ya Serikali iliyopo madarakani. Njia hii isipodhibitiwa huangusha serikali kwa maana ikatokea waandamaji wakawa wengi zaidi katika mji mmoja wanaweza kuwashinda polisi na wakaanza kufanya uhalifu, kuchoma maduka, majumba makubwa na kuchoma matairi ya gari barabarani huku wakiimba nyimbo za hamasa hatimaye Nchi inaingia katika Vurugu na hatimaye kung'oa utawala wa Haki.

Mbinu hii imewahi fanyika katika nchi kadhaa ikafanikiwa na kwa nchi thabiti ilishindwa na kwa sasa imebaki kumbukumbu kwa vizazi na vizazi.

Hii imewahi fanyika mataifa ya Misri, Libya, Iraq na ilifanimiwa miaka ya 2000 na 2010 na kwa sasa kinachoendelea kufanyika Syria ni muendelezo wa mbinu hizi chafu za Wamagharibi. Miaka ya 1970 walitaka wajaribu katika Taifa thabiti la Uchina ila Mao alisimama imara na Vijana maelfu walipoteza maisha kwa kusagwa na vifaru na sasa ni kumbukumbu njema inamulika na kuangaza kwa Taifa hilo kubwa lenye mafanikio thabiti ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Rai yangu kwa Watanzania wote wazalendo wa Taifa hili, Nchi haijengwi kwa mkate na asali ila hujengwa kwa kukubali kujikana, kukataa Unyonyaji, kuchagua Utanzania kuwa kipaumbele na kuamini kuwa kila mmoja ni mdogo kuliko Tanzania na zaidi kutambua kuwa Tanzania kuna Utawala thabiti wenye lengo la kutufikisha mahala ambapo hata vizazi vyetu havitokuja kutulaumu na kutudharau.

Yeyote anayecheza na Amani ya Nchi yetu huyo ni Adui yetu namba moja. Ni heri akatangulia kutuandalia makazi ya milele kuliko kutuchafulia Tanzania.

Tanzania ni kubwa na Nzuri kuliko mimi na wewe.

Tutunze amani yetu
Tulinde Utawala wetu.
Tunatafutwa
Ni vema tushikamane.

Imeandaliwa na;
Said Said Nguya.
Amani ukiitaka kutest nenda na v8 vingunguti halafu iache mtaaani aada nusu SAA rudi ukaingalie
 
Mtu mwenyewe unakaa Dodoma, hizo mbinu za magharibi ulizipatia wapi? Halafu makazi ya milele anaanda Mungu mwenyewe sio binadamu. Na yashaandaliwa hata kabla wewe hujazailiwa. Unaleta uoga wako hapa, subirini 26042018
 
Na Said Said Nguya
Kutoka Nzasa Dodoma.

Leo ninawaletea makala fupi yenye lengo la kukufahamisha wewe Mtanzania namna mbinu chafu za Wamagharibi( Marekani & Ulaya) zinavyotumika katika nchi nyingi za Afrika, Latini Amerika na Asia kuangusha Utawala uendao kinyume na matakwa yao.

Nchi za Marekani na Ulaya kwa asili yao ni nchi za Kibepari na msingi mkuu wa Ubepari ni unyonyaji katika kile kiitwacho mwenye nguvu na apate ( Suvival for the Fittest ).

Kutokana na msingi huo mkuu wa Ubepari Mataifa haya hufanya kila mbinu kuhakikisha Nchi za Afrika, Asia na Latini Amerika kuwa na viongozi wanaowanyeyekea na wenye ulimbukeni wa Ulaya na Amerika ya Marekani ili iwe rahisi kuwalaghai na Unyonyaji uendelee kutamalaki na kuota mizizi zaidi.

Inapotokea Nchi imempata kiongozi ambaye kwa namna yoyote, matendo yake, kauli zake na hulka yake haiendani na matakwa yao yaani anakuwa kizuizi kati ya Taifa hilo na malengo ya Maperari ambayo ni Unyonyaji, Nchi hiyo aidha ya Latini Amerika, Asia ama Afrika hujikuta katika wakati mgumu kuendesha utawala wake kwa maana Mabepari huanza kutumia mbinu mbali mbali kuuangusha utawala huo thabiti.

Hakika nasikitika kuona Tanzania tumeingia rasmi kwenye Mgogoro huo na Wamagharibi lakini zaidi nasikitika kuona baadhi ya Watanzania wakiungana nao kwa wengi kutokukujua na wachache kwa kujua kutokana na maslahi binafsi kwanza.

Tanzania kupitia uongozi huu wa Awamu ya Tano umejinasibu kwa vitendo, hulka na maneno kuwa haukubaliani na Unyonyaji wa aina yoyote kwa Taifa letu kwa kufanya mambo kadhaa.

Kwanza, ni kufuta Safari zote za nje zisizo na tija kwa Watanzania ambazo kwa kiasi kikubwa zilikuwa zikifanywa na viongozi wa Serikali, Bunge na Mahakama na hii ilikuwa inatumika kama njia mojawapo ya kuwashawishi viongozi hao kukubaliana na matakwa mbalimbali wakiwa huko ughaibuni kwa maana ni rahisi zidi kumshawishi mtu akiwa nyumbani kwako kuliko akiwa nyumbani kwake. Hii kwa kiasi kikubwa imewanyima fursa nyeti Mabepari ya kukutana mara kwa mara na viongozi wenye dhamana ya maamuzi hapa Tanzania.

Pili, ni namna Serikali ya awamu ya tano inavyoshughulika na wala rushwa na inavyopambana kukemea na kutokomeza ufisadi.

Kiukweli hakuna Taifa lolote la Magharibi linalotamani Tanzania tuwe ni moja ya mifano bora katika jambo lolote kwa kuwa wanatambua kwa sisi kuwa bora katika kupambana na rushwa itakuwa ndio njia ya sisi kupiga hatua za kimaendeleo na kuondokana na umasikini kwa sababu umasikini kwa kiasi kikubwa hutokana na ubadhirifu wa mali za umma ( Ufisadi & Rushwa ), wakati mpango wa "Siri" wa Mataifa ya Magharibi ni kuhakikisha kwa namna yoyote Nchi za Afrika, Latini Amerika na Asia zinaendelea kubaki masikini ili kufanya kuwa jalala la bidhaa duni na mifano mibaya kwa Wananchi wao.

Tatu, Ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa, usafiri wa anga na mtandao thabiti wa barabara Nchi nzima.

Wamagaribi wanatambua matokea ya kuimarisha njia kuu za usafiri na pia wanatambua ni kwa jinsi gani wao wamepiga hatua kubwa kutokana na mchango wa njia za usafirishaji. Hiki kinachofanyika leo hapa Tanzania hakiwapendezi kwa maana sheria yao na msimamo wao mkuu ni kwamba " Don't Ignore the light smoke as may turn to a big fire", hivyo msimamo wao ni kuzima kila chembe ya moshi wauonao na Tanzania ni miongoni.

Nne, ni kubadilisha sheria za madini. Hii haijawahi tokea katika mataifa mengi ya Afrika, Asia na Latini Amerika ila Tanzania imetokea katika Serikali hii ya awamu ya Tano. Si jambo la kawaida kukemea kwa sauti kuwa "Nyie ni Wezi" na tunataka usawa katika nchi yetu na kila kipatikanacho katika ardhi ya Tanzania ni mali yetu na tunahaki ya kugawana sawa.

Hakika hiki si kitu cha kawaida na mpaka sasa Wamagharibi wanaendelea na mkakati madhubuti wa kulipiza kwa madai ya kuwadhalilisha kwa kuwakemea hadharini kwa kuwa hawajazoea kuambiwa ukweli kutokana na ukubwa waliojijengea na kuwajaza hofu watawala wa Mataifa mengi ya Dunia ya Tatu.

Kutokana na mwenendo huo wa Tanzania kimataifa, ni lazima sisi Watanzania tujiandae kukabiliana na mbinu chafu za kutugawa ambazo zimewezekana katika Mataifa mbalimbali.

Kuna njia kuu tano zinazoweza kutumika kutugombanisha na kutufanya tuingie katika mapambano ya wenyewe kwa wenyewe.

Moja, ni kuunga mkono Chama Kikuu cha Upinzani na kukipatia uwezo wa kifedha ili kukabiliana na Chama tawala. Hii hufanyika kwa kukipa fedha kwa masharti kuwa endapo watafanikiwa kuangusha utawala watashirikishwa kuunda Serikali kwa mujibu ya matakwa yao. Imefanyika hivo katika mataifa mengi ya Latini Amerika mfano South Vietinam mwaka 1963 ambapo kundi dogo la upinzani lilipatiwa fedha na kulaghai Wavietnam hususani vijana, Pia ilitokea hivo hivo Brazili na Guatemala. Sisemi wamefanya hivo ila ni lazima kama Watanzania tuwe makini kufuatilia mienendo ya Vyama vya Siasa katika kipindi hichi tunapokabiliana na mapambano ya Kiuchumi na Mataifa makubwa.

Pili, Mauaji ya Viongozi thabiti na wenye msimamo. Hii hufanyika pale ambapo inatokea kiongozi kuwa na ushawishi mkubwa na hata kushindwa kupandikiza upinzani.
Hii ilitokea kwa Bw. Patrice Lumumba Mwaka 1961 kule Katanga na kusababisha Taifa hilo kutokuweza kutawalika mpaka sasa, vilevile iliweza kufanyika Ghana mwaka 1966 pale alipouawa Mzee wetu Kwame Nkurumah. Lakini pia Mataifa haya makubwa hutumia njia ya kuteka ama kuua wanasiasa maarufu, waandishi wa habari, viongozi wa dini na hata wanafunzi ili kuonesha kuwa utawala uliopo madarakani umeshindwa kulinda raia wake ama pia kuonesha hakuna utawala wa Demokrasia.

Njia ya Tatu ni kudumaza uchumi wa Taifa yaani kuweka Vikwazo katika maeneo muhimu ya kiuchumi. Njia hii hutumika sana na Mataifa ya Mahharibi ili kushinikiza kuangusha utawala ama utawala uliopo ukubaliane na mashariti ya kinyonyaji. Inaweza kuwa vikwazo vya kiuchumi katika Usafirishaji, uuzaji bidhaa nje kama nchi inapiga hatua za viwanda, mfano Taifa la la Chile mwaka 1973 ilifanyika hivo na kufanikiwa kuangusha utawala kwa maisha kuwa magumu na kuwapa nafasi Wapinzani kuipindua Serikali, Kinachoendelea kufanyika pale Korea ya Kaskazini ni moja ya mifano dhahiri.

Lakini pia mbali na kilichofanyika Chile na kinachoendelea kufanyika Korea ya kaskazini pia inaweza kufanyika taratibu ikiwa ni pamoja na kuzuia mali za nchi husika kwa kisingizio cha madeni wakati Taifa linaloongoza kwa kudaiwa Duniani ni Marekani ila haijawahi tokea akazuiliwa kuchukuwa mali ama bidhaa zake kutoka nchi fulani kwa sababu ya madeni.

Mbinu ya Nne, hii ni kutumia Vyombo vya habari na dini. ( MeDiaProPaGanDa ) hufanyika kwa kununua Makampuni ya Magazeti, Vituo vya Televisheni na Radio na wakati mwingine kirahisi kabisa huwanunua waandishi wa Habari na kuwawekea mifumo ya mishahara isiyo rasmi kwa kazi wanayoifanya ya kubadili ufikiri wa Wananchi kwa kuandika wakitakacho Wamagharibi.

Dini kwa kiasi kikubwa pia hutumika kwa kuwashawishi baadhi ya viongozi wa dini wenye ushawishi kuhubiri chuki dhidi ya utawala uliopo madarakani, yote hii huwa ni mbinu mahususi ya kubadili ufikiri wa wananchi maana viongozi wengi wa dini kwa asili huaminiwa na wakisemacho waumini huamini kumbe baadhi yao huwa ni mpango na mkakati wa kuingusha Serikali.

Mbinu hii kutumia dini na vyombo vya habari kwa sasa inashika hatamu kwa kiasi kikubwa ikiwa na lengo la kubadili mtazamo wa wananchi wa maeneo lengwa kwa kutumia muda mwingi kueleza mabaya pekee yasiyo halisi ya nchi za Afrika hususani Tanzania kwa sasa.

Mfano Vituo vingi vya Televisheni vya kimataifa kwa sasa wamepewa jukumu la kuzishambuliwa Nchi za Afrika zote zenye kuchukua jitihada ya kujikomboa kiuchumi ikiwepo Tanzania kwa kueleza mabaya kwa wingi pasipo uhalisia ili Wananchi husika wapoteze imani na uongozi.

Mbali na vituo vya kimataifa pia kuna baadhi ya vituo vya ndani na waandishi binafsi hulipwa pesa na kazi yao kubwa ni kukosoa kwenye kila jambo ili kubadili mtazamo wa wananchi dhidi ya Serikali yao. Mbali na Vyombo vya habari lakini pia kuna watu hudhaminiwa kufungua kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii mfano Twitter, Facebook na Instagram kwa ajili ya kusambaza taarifa za chuki na uongo kwa wananchi dhidi ya Serikali yao.

Na hili hufanyika kwa kuwa wameshatambua nguvu kubwa kwa sasa ipo katika Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Njia tano ni Kutengeneza Vurugu, maandamano na migomo. Hili hufanyika kwa ustadi mkubwa na zaidi hufanyika kwa kuwapumbaza wananchi wakaingia katika maandamano wakiwa hawajui kiundani hasa wanahitaji nini ama madai yao ni yapi dhidi ya Serikali iliyopo madarakani. Njia hii isipodhibitiwa huangusha serikali kwa maana ikatokea waandamaji wakawa wengi zaidi katika mji mmoja wanaweza kuwashinda polisi na wakaanza kufanya uhalifu, kuchoma maduka, majumba makubwa na kuchoma matairi ya gari barabarani huku wakiimba nyimbo za hamasa hatimaye Nchi inaingia katika Vurugu na hatimaye kung'oa utawala wa Haki.

Mbinu hii imewahi fanyika katika nchi kadhaa ikafanikiwa na kwa nchi thabiti ilishindwa na kwa sasa imebaki kumbukumbu kwa vizazi na vizazi.

Hii imewahi fanyika mataifa ya Misri, Libya, Iraq na ilifanimiwa miaka ya 2000 na 2010 na kwa sasa kinachoendelea kufanyika Syria ni muendelezo wa mbinu hizi chafu za Wamagharibi. Miaka ya 1970 walitaka wajaribu katika Taifa thabiti la Uchina ila Mao alisimama imara na Vijana maelfu walipoteza maisha kwa kusagwa na vifaru na sasa ni kumbukumbu njema inamulika na kuangaza kwa Taifa hilo kubwa lenye mafanikio thabiti ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Rai yangu kwa Watanzania wote wazalendo wa Taifa hili, Nchi haijengwi kwa mkate na asali ila hujengwa kwa kukubali kujikana, kukataa Unyonyaji, kuchagua Utanzania kuwa kipaumbele na kuamini kuwa kila mmoja ni mdogo kuliko Tanzania na zaidi kutambua kuwa Tanzania kuna Utawala thabiti wenye lengo la kutufikisha mahala ambapo hata vizazi vyetu havitokuja kutulaumu na kutudharau.

Yeyote anayecheza na Amani ya Nchi yetu huyo ni Adui yetu namba moja. Ni heri akatangulia kutuandalia makazi ya milele kuliko kutuchafulia Tanzania.

Tanzania ni kubwa na Nzuri kuliko mimi na wewe.Tutunze amani yetu, Tulinde Utawala wetu.Tunatafutwa, Ni vema tushikamane.
Kweli kabisa na hao wamarekani huenda wametuibia T1.5 zetu wabaya sana hawa.Tuwakemee
 
Nawaza tu Mfano watu wanawapa misaada na bado mnakula hela.Haya Mkuu flani hajaenda kwa hao tunao waita wanyonyaji lakini cha ajabu kabisa kushinda yote.Makusanyo yetu BINAFSI tumejiibia wenyewe pasipo mkono wa Mmarekani wala Mange Kimambi.1.5 Trln hazina maelezo ni siku ya tano watu bado wanawaza majibu ya kuja nayo.
Wazungu tunawaonea sana,nasema ukitaka kumkwepa Mzungu acha kutumia kila kitu andaa chako.Kwa waliosoma vyema wataelewa nacho maanisha,tunashindwa kujiendesha sisi wenyewe tunabaki kulalamikia nchi za watu huko mbele.Hata tungikuwa Bara la Africa lipo alone bado tusingefikia walipo hao jamaa.Watu wanategemeana kwa Hali na mali hapa duniani,UZEMBE,ULAFI na UCHOYO ndio hutuangamiza Africa.
Mtu mmoja analimbikiza pesa kibao na kujenga kwao kana kwamba wengine hawastahili mahitaji hayo.Bado anaona haitoshi anapeleka nje kwenye Bank za watu huko.Tafakari vyema kabla ya kuwalaumu MATAIFA haya makubwa.Tunao Miungu watu na MALAIKA huku Africa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom