Ethos
JF-Expert Member
- Aug 1, 2015
- 2,294
- 2,090
Miaka ya Hivi karibuni watanzania wamekuwa wakiamka na kubuni vitu ambavyo vinalinufaisha taifa Kwa kiasi kikubwa .Kama Edwin Bruno alivotengeneza app ya kusoma magazeti Dr Hilonga yeye anagusa maisha ya watu kivingine kabisa!
Kama wengi tujuavyo na wanaharakati wasemavyo kuwa maji ni uhai basi Dr Askwar Hilonga ameamua kulidhihirisha hilo Kwa Vitendo na Sio Maneno Peke yake.
Changamoto ya maji safi na Salama ni yetu sote hivyo wanapotokea wataalam mbalimbali na kuja na njia mbadala ni budi kupongezwa na kupewa Fursa zaidi ili ubunifu huo uifaidishe jamii yote.
Dr Hilonga amebuni Kifaa kiitwacho Nanofilter ambacho kimeshinda tuzo ya ubunifu ya Royal Academy of Engineering mwaka 2015.
Kifaa hicho ambacho kinatumia mchanga ikiongezewa na Nano Materials ili kuondoa vijidudu.
Dr Hilonga akielezea katika video yaYouTube amesema Nanofilter hiyo ina uwezo wa kuondoa vijidudu Kwa Asilimia 97 ila lengo Lake ni kuondoa Kwa Asilimia 99.999 hapo baadae!
Baada ya kutofurahishwa na kitendo cha familia huko kijijini alipozaliwa kutumia maji yasiyo salama alijiuliza Je PhD yake aliyoipata nchini Korea itasaidiaje watu wa kijijini kwake ndipo alipoamua kubuni teknolojia hiyo muhimu katika maswala ya usafi wa maji na afya.
Kwa sasa Dr Hilonga ni mmiliki wa kampuni ya Gongali Model ambayo Jina hilo ni Jina la kijiji alipozaliwa yaani kijiji cha Gongali wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.
gongalimodel.com | Empowering Tanzanians; YES, WE CAN
Makao Makuu ya Kampuni hiyo yapo Njiro – Nane Nane mkoani Arusha unaweza watembelea kujifunza zaidi au kujipatia mtambo huo Kwa ajili ya Biashara au Familia yako.
Unaweza mpata na kumfuata katika twitter na facebook pia kwa kutafuta jina Akwar Hilonga au kusoma zaidi katika mtandao wa kampuni inayosambaza mitambo hiyo yaGongali Model.
Source : Askwar Hilonga-Mbunifu anayeokoa mamia ya watanzania Kwa kubuni Kifaa cha Kuyafanya maji yawe safi na Salama!
Kuhusu Tuzo unaweza Pata maelezo kamili hapa... Engineering for clean water across Africa – Tanzanian entrepreneur wins first Africa Prize for Engin - Royal Academy of Engineering
Kama wengi tujuavyo na wanaharakati wasemavyo kuwa maji ni uhai basi Dr Askwar Hilonga ameamua kulidhihirisha hilo Kwa Vitendo na Sio Maneno Peke yake.
Changamoto ya maji safi na Salama ni yetu sote hivyo wanapotokea wataalam mbalimbali na kuja na njia mbadala ni budi kupongezwa na kupewa Fursa zaidi ili ubunifu huo uifaidishe jamii yote.
Dr Hilonga amebuni Kifaa kiitwacho Nanofilter ambacho kimeshinda tuzo ya ubunifu ya Royal Academy of Engineering mwaka 2015.
Kifaa hicho ambacho kinatumia mchanga ikiongezewa na Nano Materials ili kuondoa vijidudu.
Dr Hilonga akielezea katika video yaYouTube amesema Nanofilter hiyo ina uwezo wa kuondoa vijidudu Kwa Asilimia 97 ila lengo Lake ni kuondoa Kwa Asilimia 99.999 hapo baadae!
Baada ya kutofurahishwa na kitendo cha familia huko kijijini alipozaliwa kutumia maji yasiyo salama alijiuliza Je PhD yake aliyoipata nchini Korea itasaidiaje watu wa kijijini kwake ndipo alipoamua kubuni teknolojia hiyo muhimu katika maswala ya usafi wa maji na afya.
Kwa sasa Dr Hilonga ni mmiliki wa kampuni ya Gongali Model ambayo Jina hilo ni Jina la kijiji alipozaliwa yaani kijiji cha Gongali wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.
gongalimodel.com | Empowering Tanzanians; YES, WE CAN
Makao Makuu ya Kampuni hiyo yapo Njiro – Nane Nane mkoani Arusha unaweza watembelea kujifunza zaidi au kujipatia mtambo huo Kwa ajili ya Biashara au Familia yako.
Unaweza mpata na kumfuata katika twitter na facebook pia kwa kutafuta jina Akwar Hilonga au kusoma zaidi katika mtandao wa kampuni inayosambaza mitambo hiyo yaGongali Model.
Source : Askwar Hilonga-Mbunifu anayeokoa mamia ya watanzania Kwa kubuni Kifaa cha Kuyafanya maji yawe safi na Salama!
Kuhusu Tuzo unaweza Pata maelezo kamili hapa... Engineering for clean water across Africa – Tanzanian entrepreneur wins first Africa Prize for Engin - Royal Academy of Engineering