gogologomonagongio
Senior Member
- Jan 11, 2014
- 120
- 50
Pole ndugu yangu. Hukufanikiwa kumfahamu Bishop Mhogolo.
Umeingia katika mtego wa wale waliomchukia na kumlisha maneno ambayo hakusema ili kuwafanya wafuasi pamoja na wewe, wamchukie na kumwondoa ili waingie katika nafasi hiyo. Kuhusu USHOGA alichosema kwa BBC alipohojiwa ni kuwa "Ushoga ni dhambi kama dhambi nyingine, huwezi kuwatenga, lazima uwe nao na uendelee kuwahubiri ili waiache dhambi hiyo. kwa kuwatenga hutawasaidia". Kwa taarifa yako kama ni mfuatiliaji wa mambo hata mtumishi wa Mungu Pope Frances (wa wakatoliki) miezi michache iliyopita aliulizwa msimamo wake kuhusu USHOGA alisema, "hatutakiwi kuwatenga". Aliensndelea kusema kwa kimombo, "Who am I to Judge them (mimi ni nani hata niwahukumu)?
Kuhusu Upendeleo kwa taarifa yako hiyo bookshop kwa muda mrefu haipo, na ungejua kuwa hata ndugu zake ni very limited katika familia usingeingiza hilo.
Mwache akapumzike vizuri alipopangiwa na Mungu wake kulingana na alivyotumika katika maisha yake.
Kwa macho ameiacha Dayosisi mahali pazuri hasa makao makuu. Kwa muda mrefu watumishi wa makao makuu hawajakopwa mishahara yao, wanalipwa vizuri na kwa wakati.
R.I.P Bishop.
Nakumbuka mwaka 2004 alikuta walimu wawili waislamu wameajiriwa katika shule ya DCT HOLY TRINITY wakati sio wakristo,walikuwa mr Kitundu na mwingine simkumbuki vizuri jina.Jamaa aliwatoa baru kama mbwa wezi.