Mtaka Haki
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 492
- 149
Kuna Askofu mmoja huko Moshi alisema kuwa uchaguzi mkuu mwaka huu utashangaza na kama haitakuwa hivyo basi yuko tayari kupigwa mawe.
Nakubaliana naye na hapa kuna mengi ya kuangalia.
Ndio mwaka pekee ambao CCM kuliko vyama vingine vyote vimkumbwa na kamata kamata ya takukuru.
Wengine wamesema kuwa Karibu mkuu Makamba ndiye chagua la Mungu kipindi hiki kwa ajili ya kuimalizia CCM.
Yaani amekuwa kila maamuzi anayoyatoa yanaingamiza CCM. Nitatoa mifano.
1. Kuwaruhusu wanachama wenye kadi hata kama ni mpya apige kura za maoni. Wenye kadi walizotengeneza walifaidika.
2. Kuwanyima wagombea kutokushiriki mdahalo. Wapinzania wamepata angalao fursa ambayo wabunge wa CCM hawana.
Kikwete naye anatabiri kumalizia kipindi chake.
1. Dr. Slaa alisema wakati mwisho wa uongozi wa mtu ukifika Mungu huachia useme mwenyewe kumalizika kwako. ( Alisema hataki kura za wafanyakazi) Hapa wafanyakazi ni pamoja na nyie polisi, Usalama wa taifa, Wasimamizi wa uchaguzi, Mahakimu, Wakuu wa wilaya, Msajili, waalimu,nk.
Wengine wanaweza kutafsiri kuwa anataka za wale wasiofanya kazi yaani wanaotumia jasho la wengine bila kazi?
2. Anawashambulia wagonjwa wa ukimwi na kusema ni kiherehere chao.
Watu wengine wasio na busara wanaweza kusema kuwa anafanya hivyo kisaikolojia kuficha kitu fulani. Kwani washauri wangeshamnyima kuendelea kusema hivyo. Niliwahi kusikia kisa cha watu wawili waliokuwa wakivusha magendo. Mmoja alipokamatwa mwingine akamwendee yule aliyekamatwa na kumshambulia juu ya ubaya wa magendo na anathubutuje kufanya magendo.
Ilikuwa ni vigumu kwa polisi kudhani kuwa huyo aliyekuwa anafoka anaweza kuwa na magendo.
Hivyo ameacha kuona hilo wanaloweza kufikiri watu.
3. Kuanguka siku ya kwanza ya uzinduzi yaweza kuwa ishara toka kwa Mungu ya kuanguka nafasi yake ya uraisi.
4. Kushindwa kuheshimu watanzania angalao hata kwa unafiki na kujiweka mbali na wenye tuhuma zinazochukiwa na watanzania na hata kuwapigia debe ni ishara ya kuanguka.
Kushindwa kukemea wanaonunua uongozi na hata baadhi ya waliopita bila kupingwa kuiharibu demokrasia kwa kutumia umaskini wa watanzania ni ishara ya kuonyesha wananchi na Mungu anavyoweza kushangaza wenye jeuri mwaka huu.
5. Kuwasimamisha washirikina waliofika drs la saba huku umaarufu wao ukiwa ni ramli, kugombea ubunge na kusifiwa na rais hiyo ni ishara nyingine kuwa busara imepotea au wanausalama wamekubali kumnyima kura zao.
Ni vizuri akaendelea kupewa heshima na kuagwa vizuri kila anakopita mpendwa raisi wetu.
Nakubaliana naye na hapa kuna mengi ya kuangalia.
Ndio mwaka pekee ambao CCM kuliko vyama vingine vyote vimkumbwa na kamata kamata ya takukuru.
Wengine wamesema kuwa Karibu mkuu Makamba ndiye chagua la Mungu kipindi hiki kwa ajili ya kuimalizia CCM.
Yaani amekuwa kila maamuzi anayoyatoa yanaingamiza CCM. Nitatoa mifano.
1. Kuwaruhusu wanachama wenye kadi hata kama ni mpya apige kura za maoni. Wenye kadi walizotengeneza walifaidika.
2. Kuwanyima wagombea kutokushiriki mdahalo. Wapinzania wamepata angalao fursa ambayo wabunge wa CCM hawana.
Kikwete naye anatabiri kumalizia kipindi chake.
1. Dr. Slaa alisema wakati mwisho wa uongozi wa mtu ukifika Mungu huachia useme mwenyewe kumalizika kwako. ( Alisema hataki kura za wafanyakazi) Hapa wafanyakazi ni pamoja na nyie polisi, Usalama wa taifa, Wasimamizi wa uchaguzi, Mahakimu, Wakuu wa wilaya, Msajili, waalimu,nk.
Wengine wanaweza kutafsiri kuwa anataka za wale wasiofanya kazi yaani wanaotumia jasho la wengine bila kazi?
2. Anawashambulia wagonjwa wa ukimwi na kusema ni kiherehere chao.
Watu wengine wasio na busara wanaweza kusema kuwa anafanya hivyo kisaikolojia kuficha kitu fulani. Kwani washauri wangeshamnyima kuendelea kusema hivyo. Niliwahi kusikia kisa cha watu wawili waliokuwa wakivusha magendo. Mmoja alipokamatwa mwingine akamwendee yule aliyekamatwa na kumshambulia juu ya ubaya wa magendo na anathubutuje kufanya magendo.
Ilikuwa ni vigumu kwa polisi kudhani kuwa huyo aliyekuwa anafoka anaweza kuwa na magendo.
Hivyo ameacha kuona hilo wanaloweza kufikiri watu.
3. Kuanguka siku ya kwanza ya uzinduzi yaweza kuwa ishara toka kwa Mungu ya kuanguka nafasi yake ya uraisi.
4. Kushindwa kuheshimu watanzania angalao hata kwa unafiki na kujiweka mbali na wenye tuhuma zinazochukiwa na watanzania na hata kuwapigia debe ni ishara ya kuanguka.
Kushindwa kukemea wanaonunua uongozi na hata baadhi ya waliopita bila kupingwa kuiharibu demokrasia kwa kutumia umaskini wa watanzania ni ishara ya kuonyesha wananchi na Mungu anavyoweza kushangaza wenye jeuri mwaka huu.
5. Kuwasimamisha washirikina waliofika drs la saba huku umaarufu wao ukiwa ni ramli, kugombea ubunge na kusifiwa na rais hiyo ni ishara nyingine kuwa busara imepotea au wanausalama wamekubali kumnyima kura zao.
Ni vizuri akaendelea kupewa heshima na kuagwa vizuri kila anakopita mpendwa raisi wetu.