Askofu Stephen Munga: Mdude CHADEMA karibu tena duniani

Askofu Stephen Munga: Mdude CHADEMA karibu tena duniani

Amkumbushe pia aishi kwa kuheshimu mamlaka. Maana kama mdude alivyosema hataacha kutukana, ndivyo na wafundisha tabia wameapa kuwa hawatamuua ila ataendelea kukiona cha moto. Sasa asije akaja tena na tsmko kama hatamfundisha njia iliyo bora.
 
narudia tena nasema wewe ni falasi sana
Unakurupuka tuu MTU akivunja sheria anatakiwa auwawe?
Unakuta wewe ni kimwanajeshi umeishia drs la tano upoo jkt unalima kahawa
 
Kwa kumteka na kuumiza mwili ndio uchumi utapanda?
hapo VIWANDA 550 vimejengwa na wakiteka MWINGINE viwanda 250 vinaongezeka kwa kuteka kuendelee ili viwanda vijengwe kwa wingi 😂😂😂😂😂 viwanda oyeee😂😂

uchumi wa katikati oyeee
😅😂😂😂😃
 
Tangu nilipoyaona yale matusi how I wish wangekaua huko huko Goddamn siku zote mdomo unaponza kichwa halafu kijana unamdharau unamtukana na kumdhalilisha rais kiasi kile? Mimi kama mwanajeshi mwenye uzalendo na nchi hii na nisiyefungamana na upande wa chama chochote ningepewa hii mission ningekunyoosha vizuri bwana mdogo mpaka ungefurahi na roho yako .

Kutoka kambini.
Hivi unalipwa mshahara unaotokana na Kodi zetu kwa ajili ya kuwaua wanaokulipa? Sasa ukimaliza kuwaua mshahara utapata kutoka wapi?
Kama kweli wewe ni mwanajeshi hufai kuwa hapo kambini tukikutunza kwa jasho letu! Hufai, hufai na hufai kuwa mwanajeshi!
 
Tunamshukuru Mungu kwamba umerudi katika maisha haya. Naungana na wengine kukupa pole. Hukurudi kwa ajili ya wema na huruma ya watekaji na watesi wako bali umerudi kwa huruma na kusudi la Mungu. Unapaswa kumshukuru sana Mungu na kamwe usimuache. Pia wakumbuke kwa moyo wa shukrani wale wote waliokuombea na kupaza sauti zao ili uachiliwe huru. Ni furaha na faraja iliyoje kwamba siku moja sote tutakufa na kusimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mfalme wa wafalme! .

Ulipokuwa mikononi mwa watekaji na watesi wako hukuwa na thamani. Kwa kuwa hukuwa na thamani basi kwa vyovyote waliburudisha mioyo yao kwa kukufanyia walivyotaka. Wao walikuwa na malengo yao na bila shaka njia zozote za kutimiza malengo hayo zilikuwa halali. Ujue kwamba mateso yako, maumivu yako, kilio chako na machozi yako ndio ilikuwa furaha yao. Nakupa pole sana.

Watu hao waliokuteka na kukutesa hawajulikani lakini wapo hapa duniani na pengine tunapishana nao mitaani. Njia walizotumia kukuteka na kukurejesha inaonyesha kuwa wanafanya kazi nje ya mfumo na taratibu za kisheria ndio sababu hawakukurejeshea hospitali. Wapo wengine wanaotajwa kwamba nao walitekwa na hadi leo hawajapatikana. Ungana na wale wanaoendelea kuwaombea watu hao kwamba katika mateso, maumivu na machozi yao Mungu asimame upande wao.

Bila shaka unayo mengi ya kusimulia lakini kila simulizi yako uimalizie kwa kumshukuru Mungu. Ninamuomba Mungu akupe kupona na kusimama tena. Pia tafuta sana makusudi ya Bwana kukurejesha toka tundu la simba. Bwana Yesu anatuambia tuwaombee wanaotuudhi. Wewe waombee wala usiwalaani kwani ukifanya hivyo utakuwa umewapalia makaa ya moto vichwani mwao. Hata sasa usidhani kwamba waliokufanyia haya wana amani na furaha mioyoni mwao. La hasha! Damu na uhai wa mwanadamu sio mali ya mtu awaye yote bali ya Mungu. Kucheza na hivyo kinyume na sheria za nchi ni kuingilia himaya ya Mungu. Kwa hiyo wewe huhitaji kuwalaani kwani watekaji na watesi wako walikwisha kujilaani wenyewe. Jambo moja ambalo napenda kukuhakikishia ni kwamba: mateso yako, maumivu yako, uchungu wako, na machozi yako vitabaki kuwa kumbukumbu madhabahuni mbele ya kiti cha enzi cha Mungu aliye hakimu wa haki. Hivyo vitabaki kuwa kumbukumbu mpaka wale wote waliofanya hayo watakapokuja kusimama mbele za Mungu BWANA. Amani iwe nawe Mdude Chadema.View attachment 1093684
Mimi pia naungana na wewe baba askofu kumpa pole ila namshauri tu awe anatumia lugha ya busara kukosoa viongozi na sio kuwatukana maandiko matakatifu yanatuasa tutii mamlaka.
 
Mimi pia naungana na wewe baba askofu kumpa pole ila namshauri tu awe anatumia lugha ya busara kukosoa viongozi na sio kuwatukana maandiko matakatifu yanatuasa tutii mamlaka.
Atakua amejifunza na naamini hata viongozi wake watamshauri the same
 
Zezeta la kukurupuka, Mendez wa kutukana viongozi. hakuna siku uliyoacha kuporomosha matusi. Brain yako ina virus wa kutukana milele?
Ipo siku ambapo utaona raha ya kuteka watu.
Waswahili wanasema,muosha huoshwa.
Utakapotekwa na ww utajua kile tunachokisema.
 
Ni kweli,maandiko yanatuasa tutii mamlaka.
Lakini tukikosa kutii mamlaka,wenye mamlaka hawakuambiwa na maandiko kwamba wateke watu wasio watii.
Zipo mamlaka za kisheria wanapaswa kuzitumia. Vinginevyo sote tutahukumiwa kutokana na matendo yetu mbele ya Mungu
 
Tangu nilipoyaona yale matusi how I wish wangekaua huko huko Goddamn siku zote mdomo unaponza kichwa halafu kijana unamdharau unamtukana na kumdhalilisha rais kiasi kile? Mimi kama mwanajeshi mwenye uzalendo na nchi hii na nisiyefungamana na upande wa chama chochote ningepewa hii mission ningekunyoosha vizuri bwana mdogo mpaka ungefurahi na roho yako .
Kutoka kambini.
Eti kutoka kambini. Kambi ya sungusungu hiyo. Mwanajesshi timamu hawezi kuwa na akili za hovyohovyo namna hiyo. Mpuuzi.
 
Tangu nilipoyaona yale matusi how I wish wangekaua huko huko Goddamn siku zote mdomo unaponza kichwa halafu kijana unamdharau unamtukana na kumdhalilisha rais kiasi kile? Mimi kama mwanajeshi mwenye uzalendo na nchi hii na nisiyefungamana na upande wa chama chochote ningepewa hii mission ningekunyoosha vizuri bwana mdogo mpaka ungefurahi na roho yako .

Kutoka kambini.
Alitukanwa Yesu na akavumilia sembuse huyu anayejiita kichaa ?? Hii generation Ni tofauti na iliyopita , usitake kutawala kama unatawala familia yako
 
Tangu nilipoyaona yale matusi how I wish wangekaua huko huko Goddamn siku zote mdomo unaponza kichwa halafu kijana unamdharau unamtukana na kumdhalilisha rais kiasi kile? Mimi kama mwanajeshi mwenye uzalendo na nchi hii na nisiyefungamana na upande wa chama chochote ningepewa hii mission ningekunyoosha vizuri bwana mdogo mpaka ungefurahi na roho yako .

Kutoka kambini.
Kutoka kambi ya vichaa Mirembe 😀😀😀
 
Hotuba yote hiyo hakuna hata neno la kibaba la kumwonyesha binafsi kuwa ana makosa ya kiutu, matusi na dharau. Hapo tu ndo naona ni KIKI tu.
Tunamshukuru Mungu kwamba umerudi katika maisha haya. Naungana na wengine kukupa pole. Hukurudi kwa ajili ya wema na huruma ya watekaji na watesi wako bali umerudi kwa huruma na kusudi la Mungu. Unapaswa kumshukuru sana Mungu na kamwe usimuache. Pia wakumbuke kwa moyo wa shukrani wale wote waliokuombea na kupaza sauti zao ili uachiliwe huru. Ni furaha na faraja iliyoje kwamba siku moja sote tutakufa na kusimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mfalme wa wafalme! .

Ulipokuwa mikononi mwa watekaji na watesi wako hukuwa na thamani. Kwa kuwa hukuwa na thamani basi kwa vyovyote waliburudisha mioyo yao kwa kukufanyia walivyotaka. Wao walikuwa na malengo yao na bila shaka njia zozote za kutimiza malengo hayo zilikuwa halali. Ujue kwamba mateso yako, maumivu yako, kilio chako na machozi yako ndio ilikuwa furaha yao. Nakupa pole sana.

Watu hao waliokuteka na kukutesa hawajulikani lakini wapo hapa duniani na pengine tunapishana nao mitaani. Njia walizotumia kukuteka na kukurejesha inaonyesha kuwa wanafanya kazi nje ya mfumo na taratibu za kisheria ndio sababu hawakukurejeshea hospitali. Wapo wengine wanaotajwa kwamba nao walitekwa na hadi leo hawajapatikana. Ungana na wale wanaoendelea kuwaombea watu hao kwamba katika mateso, maumivu na machozi yao Mungu asimame upande wao.

Bila shaka unayo mengi ya kusimulia lakini kila simulizi yako uimalizie kwa kumshukuru Mungu. Ninamuomba Mungu akupe kupona na kusimama tena. Pia tafuta sana makusudi ya Bwana kukurejesha toka tundu la simba. Bwana Yesu anatuambia tuwaombee wanaotuudhi. Wewe waombee wala usiwalaani kwani ukifanya hivyo utakuwa umewapalia makaa ya moto vichwani mwao. Hata sasa usidhani kwamba waliokufanyia haya wana amani na furaha mioyoni mwao. La hasha! Damu na uhai wa mwanadamu sio mali ya mtu awaye yote bali ya Mungu. Kucheza na hivyo kinyume na sheria za nchi ni kuingilia himaya ya Mungu. Kwa hiyo wewe huhitaji kuwalaani kwani watekaji na watesi wako walikwisha kujilaani wenyewe. Jambo moja ambalo napenda kukuhakikishia ni kwamba: mateso yako, maumivu yako, uchungu wako, na machozi yako vitabaki kuwa kumbukumbu madhabahuni mbele ya kiti cha enzi cha Mungu aliye hakimu wa haki. Hivyo vitabaki kuwa kumbukumbu mpaka wale wote waliofanya hayo watakapokuja kusimama mbele za Mungu BWANA. Amani iwe nawe Mdude Chadema.View attachment 1093684
 
Back
Top Bottom