Askofu KKKT: Hivi ndivyo wapinzani walivyosababisha vurugu bungeni

Tuweke ushabiki kando. Hawa watumishi wa Mungu wafanye kazi yao yakuokoa roho za watu waachane na siasa.
 
Hawa ndiyo viongozi wa dini waliopotea,ambao maishani mwao wameigeuza CCM ndiyo Alfa na omega katika nchi hii.Hata udokta wake unanitia shaka,sasa anaposema kuna wabunge waliosoma shule za kata,ni kweli ndani ya bunge lile kuna mbunge aliyesoma shule ya kata?na kama walifeli je,alipokuwa anaongea na Rais alimuuliza ni kwanini shule za kata zinafelisha sana?.Alafu kwani Rais JK alikuwemo bungeni siku ile au walikuwa wanapiga stori za madili tu?.Hapa sasa nimeamini ile thread iliyokuwa inasema "scientist are more intelligent than Antheists/clerics"
 
anajipendeze CCM ili aendelee kupate msamaha wa Kodi ili amalizie ile miradi yake..Aache ufisadi wa kidini akafanye siasa....
 
Mwenyezi Mungu nipe hekima kuchangia hii Mada Amina. Inawezekana nisiwe mzuri sana katika maneno ya Mungu lakini hapa napenda ninukuu machache. Kwa wale wakristo Biblia Inasema hivi:
1. Mwanadamu hawezi kutumikia mabwana wawili maana atampenda huyu na kumchukia huyu ama ataandamana na huyu na kumuacha yule. TAFAKARI!
2. Ole wao wachungaji wa mshahara maana Mawazo yao hutazama mishahara na kusahau kondoo hata wapotee. Wale wachungaji wanaojali cheo chao pesa kuliko kondoo
3. Mkiishika ile kweli nayo kweli itawaweka huru.
4. Heri ya mtu yule asiyekwenda pamoja na wasio haki watu wasio ikiri kweli yote! TAFAKARI
5. Matendo yane na yawe ndio ndio na sio sio na si kwa jinsi ya mataaifa na ya watenda dhambi!..TAFAKARI.
6. Tazama siku zinakuja watakuja Makristo wa uwongo!
7. Tazama siku zitakuja ambazo watakuja watu kwa namna ya utauwa kumbe si wateule, watu waliovaa ngozi za kondoo kumbe kwa ndani ni mbwa mwitu wakali!
Mtu wa Mungu atafakari kwa maneno hayo. Si muhukumu Askofu bali mpimeni kwa matendo yake ( MTAWATAMBUA KWA MATUNDA YAO!)
TUZI KUMUOMBA MUNGU KWA AJILI YA NCHI HII...
 
Ni katika ibada ya leo!
Askofu wa KKKT dayosisi ya Iringa Dr. Mdegela alipoamua kuwaambia waumini wake kuhusu kilichotokea bungeni tarehe 06/sept/2013 kama ifuatavyo:

anaanza "... ndugu zangu leo ngoja niwaambie kilichosababisha vurugu za juzi bungeni.... najua humu ndani (kanisani) kuna watu wa upinzani, lakini nawaambia tu kuwa WApINZANI WAMEKOSEA SANA... siku ile nami nilikuwa Dodoma na niliongea na waziri mkuu na baadae yake nikaongea na Mhe. Rais wakaniambia kila kitu! ... wapinzani walidai CCT (jumuiya ya kikristo Tanzania) hatujashirikishwa katika mchakato wa ule muswada; huo ni uongo kabisa! mimi Askofu jina langu limetajwa katika repoti ile pia na wenzangu watatu wakiwemo, sasa CCT haijashirikishwa kivipi!"

anaendelea " ... unajua mule bungeni watu wana sifa tofauti tofauti, kuna washamba na wa mjini, kuna wenye elimu na wajinga... sasa kilichotokea pale ni ujinga mtupu, na nyie wakristo tunawaambia fanyeni uchaguzi wa busara! ... manake sisi hatujawatuma kwenda kugeuza pale kuwa uwanja wa masumbwi...! ... ukiangalia waliofanya vurugu pale ni wale waliotoka shule za kata na walipata sifuri, wao ni kutumia nguvu tu badala ya akili na wanaenda kuwakilisha itikadi zao tu....! sasa nawaambia wakristo tuombee taifa letu na tuombee waliopo madarakani wamalize salama ndipo tuandae mchakato sasa, manake kilichotokea pale ni mchakato tu..." amemaliza kuongea, misa inaendela!

wana JF hayo katika nukuu ni baadhi ya maneno ya Askofu Dr. Mdegela! na katika alama hizo ( ... ) za muendelezo ni sehemu alizoniacha katika kumnukuu!

my take! kwa mimi sijaona Askofu akielezea chanzo cha vurugu husika, na pia amesema ameongea na Waziri mkuu na Mhe. Rais lakini sijaskia akisema ameongea na upande wa pili yaani upinzani ili kukidhi misingi ya kusikiliza pande zote kabla ya hukumu (audi arterum patem =right to be heard)!

karibuni tena mezani wana JF.
maaskofu wa kweli hawaropoki ,wanasikia,wanatafakari na kutoa hoja .Kwa vyovyote vile kondoo wamepotezwa hapa.
 
Nakumbuka kuna wakati Mh. Rais Kikwete alishasema kuna baadhi ya viongozi wa kiroho wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, nashauri Kamanda Nzowa amweke huyu askofu kwenye orodha ya watu anaotakiwa kuwafuatilia, ukiona kiongozi wa kiroho anaongea hayo lazima kuna kitu anaficha nyuma ya pazia. Hata hivyo kuwa askofu tu haina maana kwamba ni mkamilifu, kama Yuda Iskariote alikuwa bega kwa bega na Yesu na bado akamsaliti kwa vipande vya dhahabu sembuse huyo jamaa (Askofu)
 
Ngoja tu niheshimu mamlaka Mungu aliyompa kuwa kiongozi wng wa dini kwa kusema machache.......
1. Askofu Mdegela anapenda sifa za kijinga, inawezekana hajaonana.na pinda wala jk
2. CCM ndio waliomsafisha wakati wa kashfa zake zilizoandikwa na gazeti la mwanahalisi, hvyo simtegemei kwenda kinyume
3. Mdegela was so good siku zile, lkn kwa sasa ni "maziwa yaliyo ghoshiwa"
4. Mungu wasaidie viongozi wetu, maana maneno haya si mazuri kwa kinywa cha mtu anaepaswa kukusanya kondoo
 
mkuu wewe kwanza mbea sana, kwahiyo, hilo limekuchoma hukusubiri mpaka misa iishe unapost umu JF, tubu kwanza dhambi ya uchochezi maana wewe hukwenda kusali bali kusikiliza vya kupost humu jf.
sasa nitasali vp wakati msalishaji mwenyewe amegeuza kanisa kama uwanja wa kumwaga oil chafu! kuwaletea habari hapa naamini Mungu atanibariki zaidi, manake silipwi na mtu yeyote!
 
sasa nitasali vp wakati msalishaji mwenyewe amegeuza kanisa kama uwanja wa kumwaga oil chafu! kuwaletea habari hapa naamini Mungu atanibariki zaidi, manake silipwi na mtu yeyote!
wewe hujui hata baraka zinatafutwa vipi, ungetumia huo muda vizuri kumsikiliza mtumishi wa Mungu kuliko kuja kutuletea umbea, ona sasa umepata laana ya aibu..
 
mkuu wewe kwanza mbea sana, kwahiyo, hilo limekuchoma hukusubiri mpaka misa iishe unapost umu JF, tubu kwanza dhambi ya uchochezi maana wewe hukwenda kusali bali kusikiliza vya kupost humu jf.

Mkuu CDM ina viongozi wazinzi.
Halafu pengine mpaka hao wavuta bagi bungeni wabake ndio wataamini kuwa wanashabikia mabomu.
 
maaskofu wa kweli hawaropoki ,wanasikia,wanatafakari na kutoa hoja .Kwa vyovyote vile kondoo wamepotezwa hapa.
ameshindwa katika roho mtakatifu! na baadhi ya kondoo wengine tumemzidi imani, hatuwezi kupotea kamwe!
 
Back
Top Bottom