Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,116
Anaandika Baba Askofu Dkt. Benson Bagonza - KKKT Dayosisi ya Karagwe.
HATUGOMBEI, TUNAGOMBEZWA
Wapendwa wangu, nimejizuia sana kuandika au kusema chochote. Lakini mmenisonga sana, nami nimo safarini. Kwa kuwa sijui kama nitafika niendako (Vienna) kabla hamjakata tamaa na kuzimia, naomba msome kwa furaha mambo haya matatu:
1. Tumetazamwa na dunia nzima kwa siku nne. Mmoja aliyeona na alikuwa mgeni akaniuliza: “Hivi nyie wenzetu Wachungaji na Maaskofu mmeishagundua mbingu haipo mkafanya iwe siri yenu tu?” Akaongeza, “kama mbingu ipo kwa nini mfanyiane haya mabaya hadharani?
2. Nilizoezwa kuamini kuwa watu wanakataliwa kwa sababu ya ubaya wao na wengine hupendwa kwa sababu ya uzuri wao. Sasa nimeamini wapo wanaoweza kukataliwa kwa uzuri na wakapendwa kwa ubaya wao. Cha msingi, ubaya hauwezi kukaa kwa amani na wema. Tumefundishwa:
Katika Agano la Kale, kichafu kikigusana na kitakatifu, kile kitakatifu kinaharibika.
Katika Agano Jipya, kichafu kikigusana na kitakatifu, kile kichafu kinatakasika. TKKK ni ya Agano Jipya au la Kale?
3. Watu wakatili na waovu hujiandaa kupiga na kuangamiza wabaya wao wakati wote. Watu wema hutafuta kuushinda ubaya kwa wema.
Hutokea wakati, wapigaji wakapiga na kufurahi kuwa wamepiga. Wakitulia hugundua kuwa kumbe wamepigwa sana. Kutosamehe ni sawa na kunywa sumu ukitegemea afe adui yako. Sumu uliyokumywa bila kukusudia inaua vibaya.
Humu kibandani kwetu huwa hatugombei bali tunagombezwa na kuzodolewa.
Unione nitakapokuona.
HATUGOMBEI, TUNAGOMBEZWA
Wapendwa wangu, nimejizuia sana kuandika au kusema chochote. Lakini mmenisonga sana, nami nimo safarini. Kwa kuwa sijui kama nitafika niendako (Vienna) kabla hamjakata tamaa na kuzimia, naomba msome kwa furaha mambo haya matatu:
1. Tumetazamwa na dunia nzima kwa siku nne. Mmoja aliyeona na alikuwa mgeni akaniuliza: “Hivi nyie wenzetu Wachungaji na Maaskofu mmeishagundua mbingu haipo mkafanya iwe siri yenu tu?” Akaongeza, “kama mbingu ipo kwa nini mfanyiane haya mabaya hadharani?
2. Nilizoezwa kuamini kuwa watu wanakataliwa kwa sababu ya ubaya wao na wengine hupendwa kwa sababu ya uzuri wao. Sasa nimeamini wapo wanaoweza kukataliwa kwa uzuri na wakapendwa kwa ubaya wao. Cha msingi, ubaya hauwezi kukaa kwa amani na wema. Tumefundishwa:
Katika Agano la Kale, kichafu kikigusana na kitakatifu, kile kitakatifu kinaharibika.
Katika Agano Jipya, kichafu kikigusana na kitakatifu, kile kichafu kinatakasika. TKKK ni ya Agano Jipya au la Kale?
3. Watu wakatili na waovu hujiandaa kupiga na kuangamiza wabaya wao wakati wote. Watu wema hutafuta kuushinda ubaya kwa wema.
Hutokea wakati, wapigaji wakapiga na kufurahi kuwa wamepiga. Wakitulia hugundua kuwa kumbe wamepigwa sana. Kutosamehe ni sawa na kunywa sumu ukitegemea afe adui yako. Sumu uliyokumywa bila kukusudia inaua vibaya.
Humu kibandani kwetu huwa hatugombei bali tunagombezwa na kuzodolewa.
Unione nitakapokuona.