Askofu Dkt. Benson Bagonza: Hatugombei, tunagombezwa na kuzodolewa

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,116
Anaandika Baba Askofu Dkt. Benson Bagonza - KKKT Dayosisi ya Karagwe.

HATUGOMBEI, TUNAGOMBEZWA

Wapendwa wangu, nimejizuia sana kuandika au kusema chochote. Lakini mmenisonga sana, nami nimo safarini. Kwa kuwa sijui kama nitafika niendako (Vienna) kabla hamjakata tamaa na kuzimia, naomba msome kwa furaha mambo haya matatu:

1. Tumetazamwa na dunia nzima kwa siku nne. Mmoja aliyeona na alikuwa mgeni akaniuliza: “Hivi nyie wenzetu Wachungaji na Maaskofu mmeishagundua mbingu haipo mkafanya iwe siri yenu tu?” Akaongeza, “kama mbingu ipo kwa nini mfanyiane haya mabaya hadharani?

2. Nilizoezwa kuamini kuwa watu wanakataliwa kwa sababu ya ubaya wao na wengine hupendwa kwa sababu ya uzuri wao. Sasa nimeamini wapo wanaoweza kukataliwa kwa uzuri na wakapendwa kwa ubaya wao. Cha msingi, ubaya hauwezi kukaa kwa amani na wema. Tumefundishwa:

Katika Agano la Kale, kichafu kikigusana na kitakatifu, kile kitakatifu kinaharibika.

Katika Agano Jipya, kichafu kikigusana na kitakatifu, kile kichafu kinatakasika. TKKK ni ya Agano Jipya au la Kale?

3. Watu wakatili na waovu hujiandaa kupiga na kuangamiza wabaya wao wakati wote. Watu wema hutafuta kuushinda ubaya kwa wema.

Hutokea wakati, wapigaji wakapiga na kufurahi kuwa wamepiga. Wakitulia hugundua kuwa kumbe wamepigwa sana. Kutosamehe ni sawa na kunywa sumu ukitegemea afe adui yako. Sumu uliyokumywa bila kukusudia inaua vibaya.

Humu kibandani kwetu huwa hatugombei bali tunagombezwa na kuzodolewa.

Unione nitakapokuona.
 
Wanachokifanya maaskofu wa Tanganyika ni uthibitisho wa ile kauli ya Mfalme Suleiman "mshike sana Elimu usimwache aende zake".

Hata kama hutakubaliana nao ila lazima ukubaliane na ukweli kwamba wanazitumia elimu zao vizuri na wana uelewa mpana wa kinachoendelea hapa nchini.
 
Bagonza lake likifeli lazima aje na mafumbo
Ukimuelewa huyu Baba askofu hunge mtupia mawe.
Huyu alie shinda alikuwa amepandikizwa na mwenda zake kwenye kipindi cha pili cha Baba Askofu Shoo. Mtego uka tenguliwa.
Huyu mteule ni mtu wa Ccm kuliko kanisa. Sitoshangaa ikija kueleweka mbinu za miaka mnne iliyo pita. Pole Baba Bagonza. Linda imani yako.
 
Ukimuelewa huyu Baba askofu hunge mtupia mawe.
Huyu alie shinda alikuwa amepandikizwa na mwenda zake kwenye kipindi cha pili cha Baba Askofu Shoo. Mtego uka tenguliwa.
Huyu mteule ni mtu wa Ccm kuliko kanisa. Sitoshangaa ikija kueleweka mbinu za miaka mnne iliyo pita. Pole Baba Bagonza. Linda imani yako.
Vita ilipofikia sa hv haihtaji mafumbo ni kuchomana live live tuuu , Bagonza Muoga , aliyekuwa anawapa Kik ni Maghufuli sasa hayupo , na yeye kwisha habar yake
 
Ukimuelewa huyu Baba askofu hunge mtupia mawe.
Huyu alie shinda alikuwa amepandikizwa na mwenda zake kwenye kipindi cha pili cha Baba Askofu Shoo. Mtego uka tenguliwa.
Huyu mteule ni mtu wa Ccm kuliko kanisa. Sitoshangaa ikija kueleweka mbinu za miaka mnne iliyo pita. Pole Baba Bagonza. Linda imani yako.
Mwendazake aliwapelekea moto sana
 
Askofu Shoo ndio maana ameuma na kupuliza kuhusu ule mkataba wa hovyo wa bandari, hawa jamaa wa KKKT siasa za kifedhuli za CCM zimeshaingia kwenye kanisa lao, sasa wanapoteza thamani yao, na yote hii ni kwa sababu ya kuendelea kumkumbatia Malasusa.

Kanisa lililobaki linaloeleweka kwa misimamo isiyoyumba, yenye haki, lisiloegemea upande wowote ni lile Moja Takatifu Katoliki la Mitume.

Mungu wa mbinguni awalinde na kuwasimamia wasiyumbishwe na shetani.
 
Wanachokifanya maaskofu wa Tanganyika ni uthibitisho wa ile kauli ya Mfalme Suleiman "mshike sana Elimu usimwache aende zake". Hata kama hutakubaliana nao ila lazima ukubaliane na ukweli kwamba wanazitumia elimu zao vizuri na wana uelewa mpana wa kinachoendelea hapa nchini.
Lakini ukitazama chanzo cha malalamiko ya Askofu Bagonza utaona kimeanzia kwa maaskofu hao hao, wenye PhD zao, wao ndio wameamua kuweka taratibu pembeni, wakawatoa nje wagombea makusudi ili wakose sifa ya kugombea, hao jamaa wamegeuka wanazuoni mafedhuli wanaolitumikia Kanisa la Kilutheri, hii ni aibu kubwa sana kwa kanisa lao.
 
Back
Top Bottom