zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 19,256
- 29,098
Duu yani we jamaa bhana mpaka unatia huruma pale juu ulisema sio maadili mtoto mwenye mimba kurudi shule na ukasupport kauli ya huyo askofu kafiri kwamba kumrudisha shule mwanafunzi aliyezaa ni kusupport uzinzi je iweje sahivi unaona ni sawa tu akiendelezwa na mzazi????? Kma sio maadili je iweje umuendeleze shule za private????Kazi kweli kweli !!! Sheria na kanuni za shule zinazomilikiwa na serikali na taasisi mbalimbali ikiwemo mashirika ya dini mwanafunzi akipata mimba anafukuzwa na hana nafasi tena hapo.
Mzazi/mlezi linabaki kuwa ni jukumu lake naye akimsusa unakuwa ni bahati mbaya kwa muathirika lkn kama akipewa plan b atatafutiwa shule nyingine.
ww c ujitoe katoliki wacha mboyoyo!;kanisa lipo litakuwepo na litaendelea kuwepoNa mie ni mkatoliki kama wewe...7 x 70 hapo iko wapi?
Pia tusisahau mtoto kapata mimba adhabu anakosa shule/ elimu wapi na wapi?
Askofu anasemaje kuhusu mapadre wanaotembea na wake za watu au kuzaa na wanawake wa mtaani na wanaogonga masista...au unajifanya huyajui hayo?..kwann hawavuliwi upadre wanapelekwa formation houses?
Ufike wakati tuache unafiki...kanisa katoliki limejaa madhambi kiasi lisingetakiwa kuwa la kwanza kumnyooshea mtu kidole....
TUMWACHIE MUNGU HUKUMU YA HAWA VIONGOZI WETU WA KIROHO...sie tunaweza kuwachoma moto wakiwa hai.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa mujibu wa taratibu za kanisa katoliki askofu wa eneo husika ndio anayetoa msimamo wa kichungaji
Ok maadili eeeh sasa kwanni wanafukuza wenye mimba ila hawafukuzi wanafunzu wasio na bikra/waliotolewa bikra kabla ya ndoa??? Au maadili ni kupinga mimba tuNa kitu ambacho mmesahau, ni kuwa Rais Magufuli ndiye aliyeamua kupigilia msumari msimamo wa Kanisa Katoliki wa siku nyingi..na wala siyo Kanisa ndio linashabikia kauli ya Rais..
Maadili ya Kanisa Katoliki mnayafahamu kabisa..hivyo ondoeni unafiki
Kwahiyo ni saw kutimua waliozaa shuleni ila mnafungisha ndoa ya mtu aliewahi kuzaa??? Sasa mbona double standarssww c ujitoe katoliki wacha mboyoyo!;kanisa lipo litakuwepo na litaendelea kuwepo
hakuna point hapa!
Kwahiyo kwakuwa ni ya miaka yote hata kma haina maana tena tuiache tu iendelew hata kma ni mbovu??? Mbona mikataba ya madini mmebadili ingawa ilikuepo kwa miaka zaidi ya 15??? Sasa kigumu kipi kubadilisha hi sheria kandamizi??Kwani watoto kuachishwa au kufukuzwa shule wakipata mimba si iko miaka yote?
Sent using Jamii Forums mobile app
Maadili ya kanisa ndio yapi? Mbona mnawafuata hao viongozi wa dini yenu blindly? Hata hamquestion matamko yao? Hata yesu alisema sikuja Kuwaita wasio na dhambi bali wenye dhambi ili waokoke.... Na ukiangalia kwa undani yesu alikufa msalabani kwa ajili yetu wote wenye dhambi, leo mnajipa madaraka ya kutosamehe wengine walipoteleza, nyie kama nani?Na kitu ambacho mmesahau, ni kuwa Rais Magufuli ndiye aliyeamua kupigilia msumari msimamo wa Kanisa Katoliki wa siku nyingi..na wala siyo Kanisa ndio linashabikia kauli ya Rais..
Maadili ya Kanisa Katoliki mnayafahamu kabisa..hivyo ondoeni unafiki
Mimba hiyo ipo wazi na uthibitisho wake wala hauitaji mkemia mkuu..(mimba ni pembe la ng'ombe halifichiki)..ila swala ni bikira kuwa ipo au haipo huwezi thibitisha..Ok maadili eeeh sasa kwanni wanafukuza wenye mimba ila hawafukuzi wanafunzu wasio na bikra/waliotolewa bikra kabla ya ndoa??? Au maadili ni kupinga mimba tu
Baba Askofu kaongelea kwa shule za Catholic...BTW, swala mimba kwa Shule za kanisa lipo wazi, na misimamo ya Kanisa ipo wazi..ni fukuza tuu..Ccm mmepoteza nchi.kila mmoja anataka aonekane mzuri kwa magufuli,sasa watu tunakiuka hata maandiko.hukumu hiyo sio ya ki Mungu !.
Hawawezi kumshangaa hakuna shule yoyote ya dhehebu au shirika la dini inayokubaliana mwanafunzi akipata mimba kuendelea na masomo baada ya kutoka kujifungua.labda a some vyuo vya UfundiAm sure, maaskofu wenzake wanamshangaa kwa kitendo chake mmnh
Atakuambia ni ruksa mtoto aliyelawitiwa kuendelea na masomo kwasababu hajapata mimba
Hivi kabla ya hii kauli ya Askofu, je! Shule za Kanisa Katoliki zilikuwa zinaruhusu wanafunzi wajawazito kuendelea na shule..?? Hivi unaifahamu misimamo ya Kanisa..Huyo askofu ajue sisi waumini ndiyo tunaomtunza na kama yeye hana dhambi basi ajitokeze mbele
Sent using Jamii Forums mobile app
Kanisa ndo limeanza leo au ndo nalo kutumika shule za kanisa Hata makosa madogo tu ya kinidhamu huwa eanafukuzwa shule. Makanisa yetu haya sijui tuASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Songea Mhashamu Damian Dallu amesema kuwa anaunga mkono hatua ya Rais John Magufuli kutoruhusu wanafunzi wanaopata ujauzito kuendelea na masomo, na kusema kuwa shule zinazomilikiwa na Kanisa Katoliki hazitaruhusu wanafunzi wanaopata ujauzito kuendelea na masomo.
Amesema hayo katika Ibada ya Misa Takatifu ya Upadrisho wa Shemasi Jerome Mtatifikolo, iliyofanyika katika Parokia ya Bikira Maria Afya ya wagonjwa Ilole jimboni Iringa ambapo amebainisha kuwa wanaoshabikia wanaopata mimba kurudi shule wanaharibu utamaduni wa kiafrika na kuchafua heshima ya Taifa.
“Hayo mambo siyo sehemu ya utamaduni wetu wa Afrika, ni mambo ya kigeni yanayotaka kutuchafulia utamaduni wetu. Nawashangaa eti wanapigania haki ya tendo la ndoa, haki ya wapi hiyo?.
Tutakuwa na shule za namna gani zinazoruhusu mwanafunzi kwenda kulea mtoto kisha arudi tena na akipata mimba nyingine aende tena nyumbani?” Amehoji Askofu Dallu.
Katika hatua nyingine Askofu Dallu amewaasa waamini kufanya maandalizi ya kutosha hasa ya kiroho wanapojiandaa kuingia katika Sakramenti ya Ndoa ili ndoa zao ziwe na mwelekeo wa kiimani zaidi. Amesema kuwa kabla ya kupewa upadri, Shemasi Jerome alihudhuria mafungo ya kiroho ya siku 5 jambo ambalo linapaswa kuigwa na wale wanaojiandaa kupokea Sakramenti ya ndoa badala ya kujikita katika kufanya maandalizi ya kimwili.
“Watu wa familia mnatumia siku ngapi kufanya mafungo kabla ya kufunga ndoa? Au ndiyo ile kufanya maandalizi mengine ya kimwili marefu. Mkumbuke kuwa hata sisi mapadri tunatoka kwenu, matokeo ya kukosa maandalizi ya kutosha kabla ya ndoa ndiyo haya tunayoshuhudia sasa hivi ambapo wanaoishi ndoa kama Sakramenti ni wachache,” ameeleza.
Aidha amesema kuwa watu wanaoishi maisha ya pamoja kwa muda mrefu hadi kuwa na watoto hawastahili kuitwa wachumba kwa kuwa uchumba kielelezo chake ni Maria na Yosefu, na kuwataka kuacha kutumia jina hilo na badala yake wajiite wachumba sugu.
“Ulisikia wapi watu wanaishi uchumba mpaka wanakuwa na wajukuu? Tafuteni jina jingine kuanzia sasa labda mjiite wachumba sugu. Tutapata mapadri na masista wa namna gani? Kielelezo cha uchumba ni Yesu na Maria,” Ameeleza.
Pia amesema kuwa kazi ya karama ni kujenga umoja wa Kanisa na siyo kuligawa, na kumtaka kila mmoja kutumia wito wake kumtajirisha mwingine.
View attachment 547182
Chanzo:Gazeti la Kiongozi..
Nadhani neno plan b ni gumu kwako maana yake nn?Duu yani we jamaa bhana mpaka unatia huruma pale juu ulisema sio maadili mtoto mwenye mimba kurudi shule na ukasupport kauli ya huyo askofu kafiri kwamba kumrudisha shule mwanafunzi aliyezaa ni kusupport uzinzi je iweje sahivi unaona ni sawa tu akiendelezwa na mzazi????? Kma sio maadili je iweje umuendeleze shule za private????
Hivi hoja yako ni ipi hasa mbona unaokoteza maana kumbe unaafiki mwanafunzi aendelww kusoma hata kma ana mimba ila at individual capacity si ndio sasa kma unaona kuna umuhim wa kuendelezwa je kwanni hutaki serikali ibadilishe sheria ili cku moja pia waruhusiwe kuendelezwa shule za serikali!!!!
Eti ehh...Ila shule za kikatoliki wana roho mbaya kushinda askari magereza.
Post sent using JamiiForums mobile app