Sasa hiyo itamsaidia kitu gani?
Yeye hajui kwamba kwa wakati huu tuliomo sasa akisimama kidete na kusimamia hayo anayowatangazia waTanzania na wakaona kweli kuwa amenuia iwe hivyo, kitendo hicho kingemweka kwenye hali tofauti kabisa mbele za waTanzania?
Kwanza kitendo hicho tu kingebadilisha hali yote si huko kwenye mahakama pekee; bali hata viongozi wengine wangeanza kuiga na kuwa na ujasiri wa kuangusha uovu huu.
Sasa yeye anajificha na kuzungumzia mvunguni tu, bila hata ya kufuatilia chochote, anataka kuwahadaa waTanzania ili iweje?