BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
NI NYERERE TU..
Leo ni siku ya NYERERE. Jina hili ni fursa kwetu sote.
Amani na umoja wetu ni matunda ya ubongo na mikono yake.
Mapema mwaka 1996 nilifika Kijijini Butiama kwa kazi maalum ya maandalizi ya masomo yangu ya juu nchini Marekani.
Majira ya saa 4 asubuhi nilipokelewa na kusubirishwa kuonana naye. Yeye alikuwa na maongezi watu wengine wanne walioonekana walikuwa wamelala hapo nyumbani. Niliwatambua watatu: Makongoro Nyerere, Masumbuko Lamwai na Mabere Marando. Hawa walikuwa ni wabunge machachari wa chama Cha upinzani cha NCCR-Mageuzi na mmoja wao akiwa ni mtoto wake wa kuzaa.
Katika uchanga wa demokrasia ya vyama vingi wakati ule, tulikuwa na Baba wa Taifa aliyewapokea nyumbani kwake wapinzani, wakalala kwake, wakala naye, wakazungumza naye na wakaendelea kukipinga na kukikosoa chama alichokiasisi. Kwenye kampeini za 1995, Vijana hawa walikuwa wamempa taabu Baba wa Taifa wakati akimnadi mgombea wa CCM (Hayati Mkapa) wakati wao wakimnadi Mzee Lyatonga Mrema.
Kwenye mitihani ya darasani tunapoulizwa kwa nini Tanzania tuna amani, huwa tunadai kuwa ni sababu ya lugha moja, kutoruhusu ukabila na udini, na program maalum za kuunganisha watu kama JKT.
Tunasahau kuwa nchi kadhaa za kiafrika zenye mifumo ya kijamaa na za kibepari, zenye lugha moja, zenye dini moja au nyingi nk, hazina umoja wala amani. Kwa nini Tanzania?
Mimi nasema ni kwa sababu ya Mwalimu Nyerere. Nchi hizo zilikuwa na kila kitu tulicho nacho lakini hazikuwa na Mwalimu Nyerere. Yeye alikuwa mwana CCM na Mpinzani hapo hapo. Hakuabudu vitu, aliabudu utu. Hakuabudu watu aliabudu utu. Hakuabudu taasisi yoyote, aliabudu sera na maono (aliwahi kusema CCM si mama yake), hakuleweshwa na sifa alizopewa, aliwahoji wanaomsifia. Alikuwa mtetezi wa HAKI ndani na nje. Alichukia ubeberu si kuchukia rangi ya ngozi yao. Kama ubeberu ungekuwa ni rangi asingekuwa na karani mzungu ofisini kwake (Mama Joan Wickens). Aliamini binadamu wote ni sawa na kulitetea hilo.
ILI kuonyesha uumini wake katika umoja wa kitaifa, alipoona mnyukano wa matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar mwaka 1995, alipendekeza kwa mara ya kwanza uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa. Alipuuzwa wakati huo, akakubaliwa baadaye.
Kama Mwalimu ni kipimo chetu, tukubali tumerudi nyuma. Hatuna amani tuna utulivu. Hatuna HAKI tuna uvumilivu. Hatuna matumaini, tuna dukuduku.
Inawezekana sana, HATUMJUI MWALIMU.
Happy Nyerere Day.
Leo ni siku ya NYERERE. Jina hili ni fursa kwetu sote.
Amani na umoja wetu ni matunda ya ubongo na mikono yake.
Mapema mwaka 1996 nilifika Kijijini Butiama kwa kazi maalum ya maandalizi ya masomo yangu ya juu nchini Marekani.
Majira ya saa 4 asubuhi nilipokelewa na kusubirishwa kuonana naye. Yeye alikuwa na maongezi watu wengine wanne walioonekana walikuwa wamelala hapo nyumbani. Niliwatambua watatu: Makongoro Nyerere, Masumbuko Lamwai na Mabere Marando. Hawa walikuwa ni wabunge machachari wa chama Cha upinzani cha NCCR-Mageuzi na mmoja wao akiwa ni mtoto wake wa kuzaa.
Katika uchanga wa demokrasia ya vyama vingi wakati ule, tulikuwa na Baba wa Taifa aliyewapokea nyumbani kwake wapinzani, wakalala kwake, wakala naye, wakazungumza naye na wakaendelea kukipinga na kukikosoa chama alichokiasisi. Kwenye kampeini za 1995, Vijana hawa walikuwa wamempa taabu Baba wa Taifa wakati akimnadi mgombea wa CCM (Hayati Mkapa) wakati wao wakimnadi Mzee Lyatonga Mrema.
Kwenye mitihani ya darasani tunapoulizwa kwa nini Tanzania tuna amani, huwa tunadai kuwa ni sababu ya lugha moja, kutoruhusu ukabila na udini, na program maalum za kuunganisha watu kama JKT.
Tunasahau kuwa nchi kadhaa za kiafrika zenye mifumo ya kijamaa na za kibepari, zenye lugha moja, zenye dini moja au nyingi nk, hazina umoja wala amani. Kwa nini Tanzania?
Mimi nasema ni kwa sababu ya Mwalimu Nyerere. Nchi hizo zilikuwa na kila kitu tulicho nacho lakini hazikuwa na Mwalimu Nyerere. Yeye alikuwa mwana CCM na Mpinzani hapo hapo. Hakuabudu vitu, aliabudu utu. Hakuabudu watu aliabudu utu. Hakuabudu taasisi yoyote, aliabudu sera na maono (aliwahi kusema CCM si mama yake), hakuleweshwa na sifa alizopewa, aliwahoji wanaomsifia. Alikuwa mtetezi wa HAKI ndani na nje. Alichukia ubeberu si kuchukia rangi ya ngozi yao. Kama ubeberu ungekuwa ni rangi asingekuwa na karani mzungu ofisini kwake (Mama Joan Wickens). Aliamini binadamu wote ni sawa na kulitetea hilo.
ILI kuonyesha uumini wake katika umoja wa kitaifa, alipoona mnyukano wa matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar mwaka 1995, alipendekeza kwa mara ya kwanza uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa. Alipuuzwa wakati huo, akakubaliwa baadaye.
Kama Mwalimu ni kipimo chetu, tukubali tumerudi nyuma. Hatuna amani tuna utulivu. Hatuna HAKI tuna uvumilivu. Hatuna matumaini, tuna dukuduku.
Inawezekana sana, HATUMJUI MWALIMU.
Happy Nyerere Day.