Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,611
- 86,305
Anaandika baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
_____
"Utusamehe Makosa Yetu"
Mwezi Machi mwaka 2017 Baba Mtakatifu, Papa Francis, katika ukuu wake na nafasi yake katika Kanisa, alichukua wajibu wa kuomba msamaha kwa ajili ya mauaji ya kimbari (genocide) ya Rwanda yaliyotokea mwaka 1994.
Makosa ya kanisa yalikuwa ya aina nne:
1. Baadhi ya mapadre kugoma kufungua makanisa ili kuwahifadhi waliokuwa wakiwakimbia wauaji.
2. Baadhi ya mapadre kuwahifadhi wakimbizi kisha wakapigia simu wauaji ili waje kuwaua wakimbizi waliojificha ndani ya kanisa.
3. Baadhi ya mapadre na maaskofu kusifu, kupongeza, na kuunga mkono juhudi za Rais Habyarimana kabla ya mauaji ya kimbari.
4. Baadhi ya mapadre na maaskofu kukaa kimya kabla ya mauaji, wakati wa mauaji na baada ya mauaji.
Haya hayakufanywa na Kanisa Katoliki peke yake tu, bali makanisa mengi nchini humo. Kanisa Katoliki linaonekana kwa sababu ya ukubwa wake, lakini viongozi wa makanisa mengine wanapaswa pia kuomba msamaha.
TUNAJIFUNZA NINI?
Kimya kinaua
Kuunga mkono kunaua
Kukaa katikati kunaua
Kwa hiyo, kusema inapotakiwa ni bora kuliko kukaa kimya inapotakiwa. Kukemea vibaya ni bora kuliko kupongeza vibaya.!
_____
"Utusamehe Makosa Yetu"
Mwezi Machi mwaka 2017 Baba Mtakatifu, Papa Francis, katika ukuu wake na nafasi yake katika Kanisa, alichukua wajibu wa kuomba msamaha kwa ajili ya mauaji ya kimbari (genocide) ya Rwanda yaliyotokea mwaka 1994.
Makosa ya kanisa yalikuwa ya aina nne:
1. Baadhi ya mapadre kugoma kufungua makanisa ili kuwahifadhi waliokuwa wakiwakimbia wauaji.
2. Baadhi ya mapadre kuwahifadhi wakimbizi kisha wakapigia simu wauaji ili waje kuwaua wakimbizi waliojificha ndani ya kanisa.
3. Baadhi ya mapadre na maaskofu kusifu, kupongeza, na kuunga mkono juhudi za Rais Habyarimana kabla ya mauaji ya kimbari.
4. Baadhi ya mapadre na maaskofu kukaa kimya kabla ya mauaji, wakati wa mauaji na baada ya mauaji.
Haya hayakufanywa na Kanisa Katoliki peke yake tu, bali makanisa mengi nchini humo. Kanisa Katoliki linaonekana kwa sababu ya ukubwa wake, lakini viongozi wa makanisa mengine wanapaswa pia kuomba msamaha.
TUNAJIFUNZA NINI?
Kimya kinaua
Kuunga mkono kunaua
Kukaa katikati kunaua
Kwa hiyo, kusema inapotakiwa ni bora kuliko kukaa kimya inapotakiwa. Kukemea vibaya ni bora kuliko kupongeza vibaya.!
Askofu Bagonza: Wakimaliza ya kwenye simu, watahamia Hospitali, Mikopo yetu. Toba zetu na vitubio havitakuwa siri tena
Ameandika Asikofu Dr Kalikawe Lwakalinda Bagonza PHD TUAZIME TENA HEKIMA YA WANYAMBO "Nyani asiyekomaa bado (mchanga), huangua kicheko aonapo msitu ukiteketea". Kwa uchanga wake huwa hajiulizi usiku atalala wapi? "Mtoto mtundu aliyezoea kutukana watu wazima, huwa haishii kwa mmoja"...
www.jamiiforums.com
Maswali matatu ya Askofu Bagonza kuhusu CHADEMA kujitoa uchaguzi serikali za mitaa
Askofu Benson Bagonza KKKT Dayosisi ya Karagwe ametoa maoni yake kuhusu kinachoendelea katika uchaguzi wa Serikali za mitaa baada ya Chadema na baadhi ya vyama vya Upinzani kutangaza kujitoa katika uchaguzi huo wakilalamikia kutokutendewa haki kwa wagombea wao. TUJIULIZE ZAIDI 1. Hivi CHADEMA...
www.jamiiforums.com