jamani wazima humu?labda tu napenda ieleweke kua si kila afisa maliasili ni afisa wanyamapori.sasa kwa jinsi nimeona hiyo taarifa (ingawa sifahamu undani wake) labda nitumie fursa hii tueleweshane juu ya tofauti ya kiutendaji kati ya idara ya wanyamapori na mamlaka ya huduma za misitu na ofisi ya maliasili na utalii katika halmashauri zetu.
1.idara ya wanyamapori
hii ni idara inayosimamia mapori yote ya akiba yaliyopo nchini ikiwa inatimiza majukumu yake chini ya sheria ya wanyamapori yaani wildlife conservation act no.9 of 2009.hiki ndo chombo kikuu cha usimamizi kilichopo cjhini ya serikali kuu (central government),sasa unapoona mtumishi anafanya kazi akiwa na kombati ndani ya pori lolote la akiba basi anajlikali kama ASKARI WA WANYAMAPORI.
2.huduma ya misitu tanzania(Tanzania Forestry Services Agency)
hii ilianzishwa kwa mujibu wa sheria ya uwakala cap.245 revised edition 2009),national forest and beekeeping policies adopted on march 1998 lakini ikawa administered kupitia sheria ya misitu no14 ya 2002 na sheria ya ufugaji nyuki no15 ya 2002.hawa wamepewa majukumu mengi lakini kati ya hayo ni pamoja kulinda hifadhi za misitu yetu yote.
NOTE
Askari wanyamapori kwa upande huu nahisi hawahusiki kwa mujibu wa majukumu ambayo kimsingi yanaainishwa na kutofautishwa na sheria hizo nlizozitaja,kwahvo nlikua najaribu kutoa angalizo tu kwa wanaotuma wajaribu kufatilia mambo kwa kina kabla ya kulaumu upande ambao kwa namna moja au nyingine unaweza ukawa offended na kutojua kwa mtoa habari ambae pengine kwa kua aliona mtu amevaa nguo zinazofanana na kada fulani basi aka conclude.ieleweke sijasema kwa ubaya lakini ni katika kuelimishana na pia niwape pole kwa hao waliopatwa na maswahibu haya.