Wakuu nimekuwa msafiri wa mara nyingi hasa nikitokea Dar kwenda Mikoani.
Mara ZOTE tunapofika Kibaha huwa naona makondakta wanashuka na kadi ya TLB ikiwa wameifinya na kati ya Shs 1000 hadi 5000 na kuwapa askari.
Askari huzugazuga kuwa wanasoma kadi hizo na kukagua gari ilihali wakisunda fedha mifukoni.
Aidha miaka ya nyuma palikuwapo na banda la mbao hapo hapo stendi ambalo lililazimika kuondolewa kwa kuhusika sana na rushwa, hali ambayo nadhani haijakoma.
Najiuliza sana, Pesa hizo ni za nini? na ili iweje?
CC:- IGP na Kamanda MPINGA.
Mara ZOTE tunapofika Kibaha huwa naona makondakta wanashuka na kadi ya TLB ikiwa wameifinya na kati ya Shs 1000 hadi 5000 na kuwapa askari.
Askari huzugazuga kuwa wanasoma kadi hizo na kukagua gari ilihali wakisunda fedha mifukoni.
Aidha miaka ya nyuma palikuwapo na banda la mbao hapo hapo stendi ambalo lililazimika kuondolewa kwa kuhusika sana na rushwa, hali ambayo nadhani haijakoma.
Najiuliza sana, Pesa hizo ni za nini? na ili iweje?
CC:- IGP na Kamanda MPINGA.