tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Askari wa Majeshi mbalimbali mkoani Morogoro wamefanya mazoezi ya pamoja ikiwemo Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Jeshi la Uhamiaji pamoja na Jeshi la Uhifadhi.
Mazoezi hayo yamelenga kuimarisha umoja katika majeshi hayo, Askari ambao wameshiriki zoezi hilo wameshuhudiwa wakipita maeneo mbalimbali Mjini Morogoro.
Soma pia: Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro laungana na majeshi mengine kufanya mazoezi ya pamoja
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama amesema zoezi la kuimarisha afya kwa majeshi hayo ni endelevu na kwamba linajimuisha nyimbo za kizalendo zenye kuleta mshikamano wa pamoja, hivyo wananchi hawapaswi kuwa na hofu.
Naye Captain Yona Mtaita amesema mazoezi yanawaimarisha kufikia lengo.
Mazoezi hayo yamelenga kuimarisha umoja katika majeshi hayo, Askari ambao wameshiriki zoezi hilo wameshuhudiwa wakipita maeneo mbalimbali Mjini Morogoro.
Soma pia: Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro laungana na majeshi mengine kufanya mazoezi ya pamoja
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama amesema zoezi la kuimarisha afya kwa majeshi hayo ni endelevu na kwamba linajimuisha nyimbo za kizalendo zenye kuleta mshikamano wa pamoja, hivyo wananchi hawapaswi kuwa na hofu.
Naye Captain Yona Mtaita amesema mazoezi yanawaimarisha kufikia lengo.