Nyoka_mzee
JF-Expert Member
- Nov 26, 2016
- 3,695
- 5,515
umeona eeee acha tu babu wanakera sana hawa jamaa ,hawana utu wala ubinaadamuWalinikera sana waniandikia fani kwa SPD 55 hapo mbezi wakija kwenye fani yangu hasa hii ambayo kila MTU atakuja nitalipiza ndugu watabaki wakilia
Ndio mlipofika hapo 'professionals' wetu.Walinikera sana waniandikia fani kwa SPD 55 hapo mbezi wakija kwenye fani yangu hasa hii ambayo kila MTU atakuja nitalipiza ndugu watabaki wakilia
Mkuu nina uchungu sana maana mpaka sasa gari yangu inavyeti vitatu na sijalipa ,nimeandikiwa kwa sababu ya ujinga wao wala hayakuwa makosa ya kuandikiwa ,nimelipaki napanda daladala maana pesa ya kulipa sinaUmeongea kwa uchungu sana ..Naaminj watumiaji wa vyombo vya moto watakubaliana na hoja yako. Sio kila kosa linalostahili kuandikiwa faini, yapo makosa madogo madogo ambayo yanahitaji tu askari kutoa elimu badala ya kuandika faini lakini kwa sasa picha inayoonekana ni kama vike lengo ni kukusanya mapato zaidi. Sasa kwa mwendo huu ajali hazitapungua. Natamani sana kuona Risk management primciples zinatumika ili kuweka mkazo kwenye maeneo yenye hali hatarishi zaidi badala ya kuwa na malemgo tu ya kujusanya mapato
Yaan hawa jamaa hata kama ntakuwa na nyumba ya kupanga Simpangishi watu kama hawa madhwalimumaisha yanakaba kila mtu anavuta kamba upande wake, sawa inaruhusiwa! lakini sio kwa dhuruma na wizi wanaofanya polisi wa barabara..
kuchukua ela ya mtu alafu sio kwa haki itakutokea puani tu!
mkuu ndomana madereva wa daladala wanawapiga kwa uwonevu waoNdugu zangu askari usalama barabarani kuweni na huruma.
Mjue mna maadui wengi sana kama mnanibishia sawa. Mnajitafutia laana za bure.
haaha mkuu sikutaka kucheka kwa machungu niliokuwa nayo ,Dah ila mkuu anakosea sana kuwafanya hawa jamaa chanzo cha mapato,na ndo inanifanya nichukie utawala huuKuna watu wanamiliki daladala na bodaboda ili kuwaongezea kipato......
Kuna watu wanamiliki wavaa khaki na nyeupe ili kuwaongezea kipato, sasa ukiona hivi vyombo vyao vimeingia mtaani, usalama wa raia utatokana na muendeshaji!
Hawa mungu atawalaaani na kia siku nawaombea dua mbaya maana wamezidi dhulma ,hata kama ni inchi haiwezi kujengwa kwa dhulmaMkuu Jijini Fulani hapa wiki 2 zilizopita ili wiki ya kukamata bajaji uwe na kosa usiwe nalo zikaenda kulundikwa Police Central mpaka idadi yao ilipofika wanayoihitaji ndo wakaacha kuzikamata kilichofuata ni kutozwa faini kila bajaji
Sasa hawa jamaa kama hawana budget ya kutosha siwatufute njia nyingine na sio hii ya kudhulumu watu!!!
Utamkuta kasimama barabarani na kitambi kikubwa kumbe kinatokana na pesa za dhulma
Wewe utakuwa kanda ya ziwa. Niliwahi endesha huko, yaani traffic wa kanda ya ziwa hawafai, hasa Mwanza. Ni wababe, hawana lughaHawa police wa usalama barabarani bado ni kero kwa wenye magari. Wamekuwa si watu wa haki badala yale ni watu wa dhuluma na uonevu. Maana imekuwa sasa hivi ni mwendo wa cheti tu.
Gari ikiwa na mchubuko kidogo tu wa rangi basi jiandae 30,000, imetokea taa za brake zimekufa 30,000. Sasa mimi niko mbele ntaonaje? Na hata mkisema kwamba inanipasa kukagua, basi chukulia asubuhi nimefanya ukaguzi ikaungua njiani wakati natoka, napo hamlifikirii?
Imekuwa kero kwa hawa watu kupindukia. Zamani gari ikiwa ina vibali una uhakika wa kutembea kwa raha. Ila sasa hivi hata gari iwe na vibarl bado utasumbuliwa na kucheleweshwa unapokwenda. Na tena sio sehemu moja , unaweza jikuta umesimamishwa zaidi ya mara kumi.
Jambo hili limenifanya nimkumbuke sana mzee wangu Kikwete, maana usumbufu huu uliopitiliza ulikuwa hamna. Nimeshuhudia askari analifata gari na kuliandikia bila hata ya kosa au kumweleza mtu alichokosea tena mtaaani.
Wito kwenu nyinyi Askari, mkumbuke dhuluma na uonevu si jambo zuri na hamuwezi kufanikiwa kwa kuchukua hela ya mtu kwa uonevu. Kaeni mkijua watu wanasononeka kwenye nafsi zao na mtapata laana. Maisha hayaishii hapo ukijiona wewe mfalme barabarani basi kuna mwingine ni mfalme mahali fulani.
Siku ukimiliki gari ndo utaelewaKama umemkumbuka JK jiangalie "upstairs" kama uko fresh.
Nimeanza kumiliki gari kabla Stand ya watoka mikoani haijaletwa Ubungo.Siku ukimiliki gari ndo utaelewa
babu mimi siko kanda ya ziwa hapa hapa kwa mungu wa Dar kiama tunakipata na hasa njia ya tegeta ,Yaan ukitoka bagamoyo pale kizuiyani Askar,ukija bunju b Askar kwa baharia Askar ukija kiliani Askar ,ukija kwa mpemba Askar, Komando Askar ,Dawasco Askar,kibo Askar, ukija makonde Askar,pale bondeni Askar, hivi huku kote utanusurika ????Wewe utakuwa kanda ya ziwa. Niliwahi endesha huko, yaani traffic wa kanda ya ziwa hawafai, hasa Mwanza. Ni wababe, hawana lugha