Askari JWTZ waionya Dawasco

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,930
31,170
Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa Dar es Salaam, wameeleza kukerwa na uongozi wa Kampuni ya Huduma za Maji Safi na Maji Taka Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASCO) kwa kutangaza na kukata maji katika kambi zao. Sambamba na hilo, wamewaonya wakataji maji hao kuwa kitendo cha kukata maji na kuingia kambini bila kuutaarifu uongozi wa kambi husika, ni kukiuka sheria za uingiaji kambini na ipo siku watakamatwa na kuchukuliwa hatua kali.

Kwa mujibu wa taarifa ya onyo ya wanajeshi hao, Mkurugenzi Mkuu wa Dawasco, Alex Kaaya na watendaji wenzake, wanalaumiwa kuwa na ajenda ya siri yenye kutaka kulitikisa Jeshi na kuwakasirisha askari ili wafanye fujo. Wanajeshi hao walisema serikali ilikwishawaagiza Dawasco na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuacha kulikatia Jeshi huduma hizo kwa kisingizio cha madeni na kuongeza: “Hivi wanatangaza madeni hayo wanalitangazia Jeshi au serikali? Waelewe Jeshi halina vyanzo vya mapato ya kulipia ankara ya maji, ni serikali ndiyo yenye jukumu la kulipa.”

Hata hivyo, taarifa ilisema wamefuatilia na kubaini kuwa fedha zinazotolewa na serikali kulipia huduma hizo, zinalipwa zote kwa taasisi hizo na wao ndio wanaolipa fedha nyingi zaidi kuliko wateja wote, na hata bili za kubambikizwa, hivyo waache kuwanyanyasa na kutamba. “Sisi tunapenda kumhakikishia Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Jakaya Kikwete na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange, kuwa pamoja na vitendo hivyo vyote vya kulihujumu jeshi tuko imara na tutaendelea kutekeleza majukumu na wajibu wetu kwa uadilifu na nidhamu ya hali ya juu,” ilisema taarifa.

Akitoa maelezo kuhusu malalamiko hayo, Mkuu wa Idara ya Operesheni wa Dawasco, Jackson Mibala, alisema wamekubaliana na uongozi wa JWTZ kuwa watamaliza kulipa deni lao lote. Kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita walikuwa wakidaiwa Sh milioni 860 na hadi sasa wamelipa Sh milioni 150. Alisema: “Rais hakusema wasikatiwe, ila alisema watulipe na wasiolipa wakatiwe maji nasi muda tuliokubaliana ukipita kabla hawajalipa kama tulivyokubaliana, tutakata maji, sisi tusipolipa umeme tunakatiwa, hivyo nasi tutawakatia wasipolipia huduma.” Alisema wao wanaingia kwenye kambi kwa utaratibu unaotakiwa na hakuna wa kuwazuia kukata maji iwapo watakuwa hawajalipa.
 
This is stupid, if they are not paying why not? if not who actually ought to pay? why should they react against the one who is not paying for their bills. Rubbish!!!
 
Military junta mentality. Mkuu wa nchi na wengi tu wanaomzunguka ni wanajeshi - ni rahisi kwao kujisahau kwa sababu ni kama tu vile tuna a government ruled by a committee of military leaders.
 
Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa Dar es Salaam, wameeleza kukerwa na uongozi wa Kampuni ya Huduma za Maji Safi na Maji Taka Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASCO) kwa kutangaza na kukata maji katika kambi zao. Sambamba na hilo, wamewaonya wakataji maji hao kuwa kitendo cha kukata maji na kuingia kambini bila kuutaarifu uongozi wa kambi husika, ni kukiuka sheria za uingiaji kambini na ipo siku watakamatwa na kuchukuliwa hatua kali.

Kwa mujibu wa taarifa ya onyo ya wanajeshi hao, Mkurugenzi Mkuu wa Dawasco, Alex Kaaya na watendaji wenzake, wanalaumiwa kuwa na ajenda ya siri yenye kutaka kulitikisa Jeshi na kuwakasirisha askari ili wafanye fujo. Wanajeshi hao walisema serikali ilikwishawaagiza Dawasco na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuacha kulikatia Jeshi huduma hizo kwa kisingizio cha madeni na kuongeza: “Hivi wanatangaza madeni hayo wanalitangazia Jeshi au serikali? Waelewe Jeshi halina vyanzo vya mapato ya kulipia ankara ya maji, ni serikali ndiyo yenye jukumu la kulipa.”

Hata hivyo, taarifa ilisema wamefuatilia na kubaini kuwa fedha zinazotolewa na serikali kulipia huduma hizo, zinalipwa zote kwa taasisi hizo na wao ndio wanaolipa fedha nyingi zaidi kuliko wateja wote, na hata bili za kubambikizwa, hivyo waache kuwanyanyasa na kutamba. “Sisi tunapenda kumhakikishia Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Jakaya Kikwete na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange, kuwa pamoja na vitendo hivyo vyote vya kulihujumu jeshi tuko imara na tutaendelea kutekeleza majukumu na wajibu wetu kwa uadilifu na nidhamu ya hali ya juu,” ilisema taarifa.

Akitoa maelezo kuhusu malalamiko hayo, Mkuu wa Idara ya Operesheni wa Dawasco, Jackson Mibala, alisema wamekubaliana na uongozi wa JWTZ kuwa watamaliza kulipa deni lao lote. Kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita walikuwa wakidaiwa Sh milioni 860 na hadi sasa wamelipa Sh milioni 150. Alisema: “Rais hakusema wasikatiwe, ila alisema watulipe na wasiolipa wakatiwe maji nasi muda tuliokubaliana ukipita kabla hawajalipa kama tulivyokubaliana, tutakata maji, sisi tusipolipa umeme tunakatiwa, hivyo nasi tutawakatia wasipolipia huduma.” Alisema wao wanaingia kwenye kambi kwa utaratibu unaotakiwa na hakuna wa kuwazuia kukata maji iwapo watakuwa hawajalipa.

Wakulaumiwa ni wao JWTZ. Hivi wanataka wawe wanatumia maji bila kulipia na kama watafanya fujo watakuwa wamedhamiria tu. Walipe bills na tuone kama DAWASCO watawakatia maji. Mimi nadhani JWTZ linataka kutumia mabavu kwa hili.
 
Kwa nini zisikatwe huku huko hazina..yaani mgawo wa pesa wa JW na Polisi ikawa minus pesa ya umeme na maji. Hazina ikalipa TANESCO na DAWASCO directly??

This way kulumbana kungeisha..maana hii pesa wakipewa wanafanyia mambo mengine au zinaliwa!
 
Kwa nini zisikatwe huku huko hazina..yaani mgawo wa pesa wa JW na Polisi ikawa minus pesa ya umeme na maji. Hazina ikalipa TANESCO na DAWASCO directly??

This way kulumbana kungeisha..maana hii pesa wakipewa wanafanyia mambo mengine au zinaliwa!

Lakini si wanapewa hizo fedha? Swali ni je, pesa zinaenda wapi? Na ujue hizi ni pesa za walipa kodi na siyo zawadi kuwa watumie wanavyotaka. Sasa wanaposhindwa kuwajibika wanataka kutumia vitisho. Tuwe wastaarabu na tuwajibike kila mmoja sehemu yake.
 
Kwa nini zisikatwe huku huko hazina..yaani mgawo wa pesa wa JW na Polisi ikawa minus pesa ya umeme na maji. Hazina ikalipa TANESCO na DAWASCO directly??

This way kulumbana kungeisha..maana hii pesa wakipewa wanafanyia mambo mengine au zinaliwa!

JWTZ sio wastaarabu naunga mkono hoja yako wapewe net of electricity and water bills
 
Hii ni kuwatafutia manundu hao wakata maji, Mkuu wa operesheni yeye atakuwa yuko ofisini anakenua tu wakati vijana wake wakitolewa baru!
 
Waachieni DAWASCO wawakatie maji wanajeshi, wanajeshi wachukue nchi kama Madagascar.

Labda tunaweza kuwa na afadhali.
 
Wakichukua nchi kwa sababu wamekatiwa maji hapatakuwa na afadhali yeyote,it will be a disaster!After all jeshi la Tanzania lina tofauti gani na mafisadi tunaowaona mitaani,mbona na wao wameshafisadishwa.

Waachieni DAWASCO wawakatie maji wanajeshi, wanajeshi wachukue nchi kama Madagascar.

Labda tunaweza kuwa na afadhali.
 
Back
Top Bottom