Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,930
- 31,170
Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wa Dar es Salaam, wameeleza kukerwa na uongozi wa Kampuni ya Huduma za Maji Safi na Maji Taka Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASCO) kwa kutangaza na kukata maji katika kambi zao. Sambamba na hilo, wamewaonya wakataji maji hao kuwa kitendo cha kukata maji na kuingia kambini bila kuutaarifu uongozi wa kambi husika, ni kukiuka sheria za uingiaji kambini na ipo siku watakamatwa na kuchukuliwa hatua kali.
Kwa mujibu wa taarifa ya onyo ya wanajeshi hao, Mkurugenzi Mkuu wa Dawasco, Alex Kaaya na watendaji wenzake, wanalaumiwa kuwa na ajenda ya siri yenye kutaka kulitikisa Jeshi na kuwakasirisha askari ili wafanye fujo. Wanajeshi hao walisema serikali ilikwishawaagiza Dawasco na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuacha kulikatia Jeshi huduma hizo kwa kisingizio cha madeni na kuongeza: Hivi wanatangaza madeni hayo wanalitangazia Jeshi au serikali? Waelewe Jeshi halina vyanzo vya mapato ya kulipia ankara ya maji, ni serikali ndiyo yenye jukumu la kulipa.
Hata hivyo, taarifa ilisema wamefuatilia na kubaini kuwa fedha zinazotolewa na serikali kulipia huduma hizo, zinalipwa zote kwa taasisi hizo na wao ndio wanaolipa fedha nyingi zaidi kuliko wateja wote, na hata bili za kubambikizwa, hivyo waache kuwanyanyasa na kutamba. Sisi tunapenda kumhakikishia Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Jakaya Kikwete na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange, kuwa pamoja na vitendo hivyo vyote vya kulihujumu jeshi tuko imara na tutaendelea kutekeleza majukumu na wajibu wetu kwa uadilifu na nidhamu ya hali ya juu, ilisema taarifa.
Akitoa maelezo kuhusu malalamiko hayo, Mkuu wa Idara ya Operesheni wa Dawasco, Jackson Mibala, alisema wamekubaliana na uongozi wa JWTZ kuwa watamaliza kulipa deni lao lote. Kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita walikuwa wakidaiwa Sh milioni 860 na hadi sasa wamelipa Sh milioni 150. Alisema: Rais hakusema wasikatiwe, ila alisema watulipe na wasiolipa wakatiwe maji nasi muda tuliokubaliana ukipita kabla hawajalipa kama tulivyokubaliana, tutakata maji, sisi tusipolipa umeme tunakatiwa, hivyo nasi tutawakatia wasipolipia huduma. Alisema wao wanaingia kwenye kambi kwa utaratibu unaotakiwa na hakuna wa kuwazuia kukata maji iwapo watakuwa hawajalipa.
Kwa mujibu wa taarifa ya onyo ya wanajeshi hao, Mkurugenzi Mkuu wa Dawasco, Alex Kaaya na watendaji wenzake, wanalaumiwa kuwa na ajenda ya siri yenye kutaka kulitikisa Jeshi na kuwakasirisha askari ili wafanye fujo. Wanajeshi hao walisema serikali ilikwishawaagiza Dawasco na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuacha kulikatia Jeshi huduma hizo kwa kisingizio cha madeni na kuongeza: Hivi wanatangaza madeni hayo wanalitangazia Jeshi au serikali? Waelewe Jeshi halina vyanzo vya mapato ya kulipia ankara ya maji, ni serikali ndiyo yenye jukumu la kulipa.
Hata hivyo, taarifa ilisema wamefuatilia na kubaini kuwa fedha zinazotolewa na serikali kulipia huduma hizo, zinalipwa zote kwa taasisi hizo na wao ndio wanaolipa fedha nyingi zaidi kuliko wateja wote, na hata bili za kubambikizwa, hivyo waache kuwanyanyasa na kutamba. Sisi tunapenda kumhakikishia Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Jakaya Kikwete na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange, kuwa pamoja na vitendo hivyo vyote vya kulihujumu jeshi tuko imara na tutaendelea kutekeleza majukumu na wajibu wetu kwa uadilifu na nidhamu ya hali ya juu, ilisema taarifa.
Akitoa maelezo kuhusu malalamiko hayo, Mkuu wa Idara ya Operesheni wa Dawasco, Jackson Mibala, alisema wamekubaliana na uongozi wa JWTZ kuwa watamaliza kulipa deni lao lote. Kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita walikuwa wakidaiwa Sh milioni 860 na hadi sasa wamelipa Sh milioni 150. Alisema: Rais hakusema wasikatiwe, ila alisema watulipe na wasiolipa wakatiwe maji nasi muda tuliokubaliana ukipita kabla hawajalipa kama tulivyokubaliana, tutakata maji, sisi tusipolipa umeme tunakatiwa, hivyo nasi tutawakatia wasipolipia huduma. Alisema wao wanaingia kwenye kambi kwa utaratibu unaotakiwa na hakuna wa kuwazuia kukata maji iwapo watakuwa hawajalipa.