Askari aliyepiga picha na Lema atokomea

Askari aliyepiga picha na Lema atokomea

kumbe kuwa mwanajeshi ni kuvaa magwanda ukishavua wewe sio mwanajeshi. hapo nimezielewa akili za jeshiccm. mia
 
kumbe ccm inachagua wakuu wa wilaya ambao si wanaccm!ile hazina ya wanachama milioni 5 haitoshi kupata wakuu wa wilaya?!lini hawa wanajeshi hupewa kadi za ccm na lini huzirudisha?
Naona wanaibua hoja juu ya hoja!
Kumbe siasa ni kazi eh?kwa minajili hii kanali ameruhusu wanajeshi wetu kuvua kombati halafu wavae magwanda na magamba kwa muda flani wapige siasa halafu warudi jeshini...hii haki inaeleweka kwa wajeda wote?
 
Umeshaambiwa yeye alisha pitia JKT unamtakia nini zaidi eleza ili aweze kujitokeza.

:violin:
 
Wanajeshi kulingana na katiba ya sasa hawaruhusiwi kufanya kazi za kisiasa isipokuwa tu wamejiuzuru kwanza kazi yao ya awali na siyo secondiment, na hii tabia ya kujaza wanajeshi maDC na Rcs inaanzaje kama siyo kupeana chakula tu, kwani hakuna raia wazuri katika utawala wanaoweza kufanya kazi hizo, watupe bwana mbona tupo na tunaweza tu hata kuliko wao, tumewaona wengi tu wakichemsha sana tu.
 
Maelezo ya huyo msemaji wa jeshi yameniacha hoi!
1: Uanajeshi wa mtu ni magwanda. Hii ina maana ''ukivua'' magwanda basi wewe sio mwanajeshi tena na ukivaa unarudia uanajeshi wako. Ndio maana watu wanaweza kuwa ma-DC just kwa kuvua magwanda na wanapoacha u-DC wanarudia uanajeshi just kwa kuvaa magwanda)
2:Jeshi halijui wanajeshi wake, wako wapi na wanafanya kazi gani. Hii ni kwa sababu kama ni mwanajeshi/sio mwanajeshi angeshatambulika siku nyingi na haihitaji uchunguzi hata wa zaidi ya siku moja kujua kama mtu fulani ni mwanajeshi au sio mwanajeshi.
 
Sikutegemea kama na intelijensia ya JESHI ni dhaifu kiasi hiki.
 
Kuwa mwanajeshi c sababu kuwa huna haki ya kushirki kama mtu mwingine kawaida lah! Suala tunalotakiwa kuelewa hapa ni wakat gan unatakiwa kushirk kama taratibu za nchi zinavyoeleza ndilo suala kamanda mgawe analolieleza, tuache ushabk kabla ya kujua taratib za sehem husika (nchi)
Mkuu unaonekana huelewi unachokitetea hapo hujagundua kama Majibu ya Mgawe yanaacha maswali kuliko majibu?? labda wewe ndiye Kapambala ebu tusaidie
1. Ili uwe DC au RC kwa sasa lazima uwe kada mtiifu sana wa CCM, au ulipwe kama fadhila kwa kufanya kazi fualani itakayo wafurahisha CCM; Je hao wanajeshi wanapewaje UDC au RC kama si makada wa CCM.
2. Wakiwa katika Madaraka hayo mapya wanakuwa Member wa CCM (Huwezi kuwa mkuu wa wilaya kwa sasa bila kuwa Member wa ccm, Je huo uanachama wanakuwa wameupata lini?
3. Pindi wanapomaliza vipindi (ambavyo pia huweza kuendelea to infinity) wanarudi Jeshini kisha uanachama unakoma? au unabakia kama akiba? au what????

 
Anatafutwa kwa kuvaa sare za jeshi na kupiga nazo picha, tena na mbunge wa chama cha Upinzani. Hili ni kosa sana bora hata angekuwa amepiga na mbunge wa chama Tawala.. Duh, siasa za Bongo hizi....!!! nashauri JWTZ waache huu ijinga waendelee na kazi zao.. hii ni siasa tu!!!
ni kweli mkuu tanzania ukiwa upinzani unahitaji ngozi ngumu!
 
“Huyu kijana inasemekana alishawahi kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), lakini wakati
tunaendelea na uchunguzi alitoroka katika nyumba aliyokuwa amepanga bila ya taarifa kwa baba mwenye nyumba,” alisema Kanali Mgawe na kuongeza:


hizi sarakasi mpaka lini?

kuna siku zitawavunja migongo hawa watu
 
Tangu day one nilisema yule sio mjeda bali ni imposter tuu!, nikawashauri Chadema wamkabidhi kunakohusika ili kuilinda hadhi ya chama kisiwe an "accessory before the fact", na kusingiziwa ndio wali mplant huyo mjeda fake ili kuwathibitishia wajeda na wananchi kwa ujumla kuwa baadhi ya wajeda wameshaanza kujiandaa kisaikolojia kumpokea the next CIC kutoka upande wa CDM!.
P.
 
Aisee Kamanda anazidi kuibua mjadala mzito mkubwa zaidi
Nahitaji kujua iyo sheria ya secondment tu-construe.

mada hii inanikumbusha shutuma alizozitoa yule waziri wa uingereza bi Claire Short ndani ya bunge lao akiishutumu serikali ya tz kuwa na mfumo wa black dictatorship na kuiomba uingereza kuinyima misaada.na ile ishu ya acc ya jwtz nje kukutwa na pesa nyingi kiasi cha wahisani kushangaa ni kwa vipi tz bado ni ombaomba mnaikumbuka?nisonge nguna yangu nile miee.!
 
Tangu day one nilisema yule sio mjeda bali ni imposter tuu!, nikawashauri Chadema wamkabidhi kunakohusika ili kuilinda hadhi ya chama kisiwe an "accessory before the fact", na kusingiziwa ndio wali mplant huyo mjeda fake ili kuwathibitishia wajeda na wananchi kwa ujumla kuwa baadhi ya wajeda wameshaanza kujiandaa kisaikolojia kumpokea the next CIC kutoka upande wa CDM!.
P.

Vague, Pasco.
CHADEMA "wamkabidhi".....? Wao kama nani? Je unaweza kuthibitisha hizo tuhuma zako za CHADEMA kumpandikiza huyo mjeshi?

Ndio maana taaluma ya uandishi habari inapuuzwa na kununuliwa kwa bei chee na wenye fedha nchini.
 
Haya msemaj wa geshi we jkanyage2 cdm wapo makin utajalia cku1 ;(
 
Nimekubali jf kumbe kuna vichwa kazi. Nimefurahi sana kwa michango yenu, mungu nijalie niwe nbusara kama zenu. Afande katupatia hoja tuijafili asnteni sana wadau.
 
Back
Top Bottom