Askari aliyepiga picha na Lema atokomea

Askari aliyepiga picha na Lema atokomea

Mhhhhh! Kumbe kule JWTZ kuna sheria za aina mbili!!!! Baadhi ya wanajeshi wanaruhusiwa kujihusisha na mambo ya siasa na baadhi hawaruhusiwi!!! sasa sijui ni vigezo vipi vinavyotumika katika kuamua mjeshi huyu anaruhusiwa na yule haruhusiwi!!!! Kazi Kweli kweli!!!! Hili Jeshi Magamba bado lina safari ndefu sana ya kujiweka mbali na magamba.

Huyo mjeshi inayedaiwa katoroka asiwe kapelekwa Mabwepande kufanyiwa kitu mbaya.




Alipoulizwa kama kuna tofauti gani kati ya mwanajeshi kuingia kwenye mikutano ya wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kisiasa kama wakuu wa wilaya na mikoa, Kanali Mgawe alijibu:" Wanajeshi wanaofanya kazi za U-DC au RC, wanaruhusiwa kisheria."


 
Makubwa hayo. Ukivua magwanda ya jeshi ruksa kuwa gamba, ukivaa gwanda unakuwa afande!?
 
Katika katib a mpya kuna ulazima wa kuwa na kipengele kitakacho tambua uhuru wa mtu binafsi mbali na kufungwa na sheria za kazi ambazo zinamfanya mtu kukosa uhuru wa kufanya kile anacho guswa nacho moyoni ili watu wawe na uhuru wa kuonesha hisia zao kama huyo mjeshi alivyo kuwa uameguswa na kuamua kuweka hadharani hisia zake za moyoniiiiiiiiiiiiiiii
 
Leo ndo nimeelewa kumbe mwanajeshi anaruhusiwa kufanya kazi za ccm kama DC au RC na kuwa mjumbe wa kamati za siasa za wilaya au mkoa.Sasa ndipo ukweli umeanikwa kwamba bado JWTZ lipo kwenye mfumo wa chama kimoja.
 
ubabaishaji tu.... huyo msemaji kajichanganya kwenye statement yake.
labda wewe ndo hujamuelewa! anachosema hapa kanali ni kwamba ukiwa mwanajeshi Tanzania unaruhusiwa kufanya siasa za ccm na sio against ccm! well said mgawe,kidumu chama cha Mapinduzi kanali!
ndo maana kila siku huwa nasema it will take us the hard way kujikomboa, lakini kwa kura za kwenye makaratasi tutakesha kwa kujua hilo ndo maana sisi wengine tunajiandaa kwa yote kwamba ikiwa ardhini,angani au majini poa tu!
 
Huyu Mgawe kwa ufafanuzi alioufanya ameiacha uchi JWTZ na kuonyesha jinsi inavyotumika na magamba ili kutimiza mradi wake wa kutawala Tanzania milele.

Leo ndo nimeelewa kumbe mwanajeshi anaruhusiwa kufanya kazi za ccm kama DC au RC na kuwa mjumbe wa kamati za siasa za wilaya au mkoa.Sasa ndipo ukweli umeanikwa kwamba bado JWTZ lipo kwenye mfumo wa chama kimoja.
 
Kumbe bora ilikua kunyamaza tu,hii jambo lina implication mbaya sana!
 
Vague, Pasco.
CHADEMA "wamkabidhi".....? Wao kama nani? Je unaweza kuthibitisha hizo tuhuma zako za CHADEMA kumpandikiza huyo mjeshi?

Ndio maana taaluma ya uandishi habari inapuuzwa na kununuliwa kwa bei chee na wenye fedha nchini.

Eti huyu nae ni mwandishi wa habari, tena na shahada ya sheria juu!!

Ameshindwa hata kusaidia kuhoji yafuatayo:
1. Kama CCM wanaweza kuchukua wanajeshi kwa kile Msemaji wa jeshi kaita secondment, je ni lini hao wanaokuwa seconded walijiunga na CCM na kukubali itikadi na sera za CCM to the extent wakaaminiwa kuwa wanaweza kuwa ma-DC/RC?

2. Je, ikiwa chama kingine kitashinda uchaguzi na kuunda serikali, wataweza vipi kupata wanajeshi wa kuwa-second kwenye shughuli nyingine za kisiasa iwapo kwa sasa tunaambiwa kuwa hakuna mwanajeshi anayeruhusiwa kujiunga na vyama vya siasa akiwa jeshini? (na CCM wao wanawapataje hao wanaowapa u-DC/RC iwapo siasa hairuhusiwi jeshini? Waliwarecruit lini mpaka wakaiva kiasi cha kwenda kuwa makada wao kwenye ngazi kubwa hivyo?)

Msigwa (mbunge wa Iringa mjini) aliwahi kusema kuwa kuna tatizo la watu kuwa wamesoma vizuri kidogo na wanategemewa kutoa michango yao in a positive way kusaidia jamii, lakini wanaamua kuweka maarifa na ujuzi wao mfukoni na kuanza kujipendekeza kwa makubwa wao kwa kuhubiri hata wasichokiamini (hapa alikuwa anam-refer Mwigulu). Nadhani Pasco nwe ni mmoja wao.

So disgusting!
 
Maskini kijana wa watu alishindwa kuzuia hisia zake
 
Ukiniita kwenye kikao cha kutoa maoni ya katiba mpya nitasema " wanajeshi usiwe ni kuvaa au vuvua magwanda bali uwe ni utumishi tukuka wa mtu na mwanajeshi awe amevaa au kuvua magwanda asijihusishe na siasa" Mgawe atanisaidia
 
CCM wanatamani Lema naye ashitakiwe kwa kupiga picha na mwanajeshi ah aha a haa ?? !!!
 
Wajibu wa serikali kulinda raia wake, tunataka jibu ameyowekea wapi?
 
ama kweli kwa tafsiri hii ya jeshi inaonekana hata baba akitoka chumbani na kukakaa sebuleni anakuwa mjomba akirudi chumbani anakuwa baba tena
 
Kila mahali,kila sekta, na kila kitu kina taratibu na sheria zake, alichofanya huyo aliyejiita Mwanajeshi hakipo katika taratibu zao, kwani hata wao ukiwauliza hakuna aliyefurahiwa na kitendo hicho, huo ni ulimbukeni wa kutokujua mambo. Hata kingeongoza chama gani, bado taratibu za chombo hicho na miiko yake lazima ifuatwe, msishabikie vitu ambavyo hamvijui. Hebu jiulize itakuwaje, kila mwanajeshi ashabikie chama chake halafu wote wanamiliki silaha.
 
Back
Top Bottom