Hii Comment nadhani imetulia, sasa tuhitimishe mijadala ya maisha binafsi na kuangalia masuala ya mustakabali wa TAIFA! Tujibu hoja za manufaa kwa wananchi!
------------------------------------------------------------
Kwa watanzania wote wenye mapenzi mema na hata wale walioathirika vibaya na kimeta cha CCM wasome ujumbe huu. Ni bure, hakuna kulipia!
Inatia huruma sana kwa vile wakati huu wa kampeni CCM wamebanwa mbavu kiasi kwamba hakuna anayethubutu kujibu hoja nzito kuhusu ufisadi. Wamebanwa sawasawa! Sasa wanatafuta pa kutokea! Wanachokifanya sasa ni kujaribu kuhadaa wananchi na hoja za maisha ya ndoa ya Dr Slaa. Hoja zenyewe, ukiziweka katika mizani moja na zile za ufisadi, utaona mwenyewe uzito unaangukia wapi.
Kuoa na kuolewa na kuzaliana ni jambo la kawaida katika maisha ya wanadamu na wanyama, na wadudu pia. Hata panya wanaoana na kuzaliana. Na kunguni pia. Hiyo ndiyo hulka ya viumbe vyote! Na wala ngono haimuathiri panya katika uwezo wake wa kuchimba mashimo!
Na wanadamu ni vivyo hivyo. Ngono haina madhara yoyote bali huburudisha na kuchangamsha. Historia inaonyesha kuwa wapo hata wafalme katika biblia waliokuwa na wanawake wengi. Lakini uwezo wao wa kiutawala unasifika hadi leo. Nani asiyemjua mfalme Daudi katika biblia? Huyu alikuwa wa wanawake wanane waliotajwa, na vimada kadhaa ambao hawakutajwa. Na Mfalme Solomon je? Naye hamumfahamu? Haya, huyu alikuwa na wanawake 700 na vimada 300. Dr Slaa ana mmoja!
Baadhi ya marais mashuhuri waliokwisha kusifika duniani, walitokea kuwa na vimada! Rais Franklin Roosevert wa Marekani alikuwa na mke wa ndoa, Eleonor. Lakini kwa pembeni alikuwa na wa moyo wake, Lucy Mercer. Mwaka 1918 Eleonor alipogundua mahusiano hayo, Roosevert alimuacha Lucy. Lakini miaka michache baadaye Roosevert alipokuwa rais, Mapenzi na Lucy yakanoga kuliko hata mwanzoni. Roosevert alipofariki mwaka 1945 huko Georgia, kimada Lucy Mercer, alilia hadi akazimia. Roosevert anasifika hadi leo kwa uongozi wake uliotukuka. Ngono haikumuathiri!
John F. Kennedy hadi leo wamarekani wanamjua kama "Ladies man"- Bwana wa mabibi. Huyu alikuwa mtaalam wa ngono! Pamoja na kwamba alikuwa na mke wake wa ndoa aliyejulikana kwa jina la Jacquiline, alikuwa pia na vimada wengine kibao akina Judith Exner na Marilyn Monroe. Na mara nyingi alitumbukia nao White House. Pamoja na ngono, anajulikana kwa utendaji wake mzuri, hadi uwanja wa ndege wa Kimataifa huko New York unajulikana kwa jina lake, J. F Kennedy International Air Port. Huyu naye, ngono haikumuathiri.
Bill Clinton na Monica Lewinsky wanajulikana sana kwa mahusiano yao ya ngono. Lakini ni nani asiyemjua Clinton na utendaji wake wa kazi? Na huyu naye, ngono haikumzuia asifanye kazi zake.
Jacob Zuma, rais wa Africa ya kusini, anao wanawake watatu. Na wote wanajulikana kama first ladies. Na bado kwa pembeni, anazo nyumba nyingine ndogo nne. Jumla wanawake saba. Dr Slaa ana mmoja..
Nani asiyemjua mzee Nelson Mandela? Huyu alimwacha mke wake wa ndoa, akaoa mke wa mtu mwingine. Alimuoa mke wa Samora Mashel. Wala sifa ya Mandela haijapungua mpaka leo, mpaka kesho. Sasa sijui ninyi CCM mnatuletea utumbo gani! Hoja za kuacha mke na kuoa mwingine wala hata hazina mvuto zikilinganishwa na hoja za wizi na ufisadi! Poleni sana kwa kutapatapa!
Watanzania ni wa kuhurumiwa. Ni rahisi kurubuniwa hata na hoja ambazo hazina kichwa wala miguu. Ukimdondoshea kuku vipande wiwili vya almasi na punje mbili za mahindi, ni wazi atashambulia punje za mahindi na kuiacha almasi. Atafanya hivyo kwa vile akili yake imeishia hapo. Hana la ziada. Hana habari na thamani ya almasi!
Ndivyo watanzania wengi wanavofanywa na CCM. Uwezo wao wa mang'amuzi ya mambo umedumaa. Na CCM inatumia mwanya huo kuwarubuni. Waakati tunahangaika kujaribu kutupa macho huku na kule ili kujaribu kupeana mawazo juu ya maendeleo ya kiuchumi ya nchi yetu, na ni nani mzalendo wa kweli atakayetuvusha katika lindi la umaskini, CCM wanatupotezea lengo na kutuletea habari ya maisha ya mtu binafsi. Hawataki tuongelee almasi na dhahabu zetu zinazokwapuliwa . Wanataka uwezo wetu wa kufikiri uishie kwenye ngono.
CCM wamekuwa wakimtuhumu Dr Slaa kwamba ana kimada. Hii ni hoja finyu sasa ukiilinganisha na hoja za ufisadi zinazotolewa, ambazo zinahitaji majibu. Wanachokifanya ni kujaribu kukwepa kujibu maswali na hoja za msingi kuhusu ufisadi. Baadala ya wananchi kufikiri na kujadili mambo yanayohusu uchumi wa taifa lao, waanze kufikiri na kujadili juu ya maisha ya mtu binafsi.
Iwapo Dr Slaa ana mwanamke, shida iko wapi? Mbona ni ishara nzuri kwamba, walau ni mwanamme, tena dume la mbegu! Na hata ukimtazama Dr. Slaa usoni, unaona ana sura ya kiume! Anao uwezo wa kuoa! Na hilo haliwezi kuathiri uwezo wake wa utendaji kazi. Rais wa Afrika ya kusini anao saba. Dr Slaa anaye mmoja! Sijui iwapo Makamba ulikwishafika Swaziland. Kama hajafika namshauri ufunge safari ukajionee mfalme Muswati ana wanawake wangapi. Yeye binafsi, hatuna sababu ya kumchunguza, anajijua mwenyewe!
Sasa tukianza kuchunguza maisha ya ndoa ya kila mtu, ni mwanamme gani atasimama? Wenye vimada ni wengi, hadi wanatia kinyaa. Viongozi wakuu wa CCM ndio wenyeviti wa ngono! Tuongelee dira na mwelekeo wa kiuchumi wa nchi yetu. Maswali muhimu yajibiwe, kuliko kukurupukia maisha binafsi ya mtu.
Tunataka mtu wa kutuonyesha dira za kimaendeleo. CCM isituyumbishe na hoja za ngono ambazo hazimjengi mtanzania. Baadala ya kujibu maswali ya msingi kuhusu ufisadi, mnatupachika tongotongo za ngono ili kutupotezea lengo. Tunataka kupata majibu ya kufaa juu ya maswali kuhusu ufisadi unaofanywa na watu wachache, huku mamilioni ya watanzania wakihangaika kila kukicha. Ee Mungu inasue nchi yetu katika mikono ya mafisadi!
Wewe mtanzania uliyeathiriwa na aina hii ya kimeta cha CCM, amka kumepambazuka! Achana na longolongo za CCM. Achana na akili za kuku kuishia katika punje za mahindi. Kura yako mpe Dr Slaa! Mwambie na mke wako, kura yake Chadema inaihitaji.
Usisahau kumpasha habari na mama yako kule kijijini. Mwambie kura yake ni muhimu sana kwa Chadema. Kila la heri. Ubarikiwe sana!
Mwenye maoni awasiliane nami kwa e-mail hii: mak.ralph
yahoo.com
Source: Coment in Mwananchi, 2010-9-6
------------------------------------------------------------
Kwa watanzania wote wenye mapenzi mema na hata wale walioathirika vibaya na kimeta cha CCM wasome ujumbe huu. Ni bure, hakuna kulipia!
Inatia huruma sana kwa vile wakati huu wa kampeni CCM wamebanwa mbavu kiasi kwamba hakuna anayethubutu kujibu hoja nzito kuhusu ufisadi. Wamebanwa sawasawa! Sasa wanatafuta pa kutokea! Wanachokifanya sasa ni kujaribu kuhadaa wananchi na hoja za maisha ya ndoa ya Dr Slaa. Hoja zenyewe, ukiziweka katika mizani moja na zile za ufisadi, utaona mwenyewe uzito unaangukia wapi.
Kuoa na kuolewa na kuzaliana ni jambo la kawaida katika maisha ya wanadamu na wanyama, na wadudu pia. Hata panya wanaoana na kuzaliana. Na kunguni pia. Hiyo ndiyo hulka ya viumbe vyote! Na wala ngono haimuathiri panya katika uwezo wake wa kuchimba mashimo!
Na wanadamu ni vivyo hivyo. Ngono haina madhara yoyote bali huburudisha na kuchangamsha. Historia inaonyesha kuwa wapo hata wafalme katika biblia waliokuwa na wanawake wengi. Lakini uwezo wao wa kiutawala unasifika hadi leo. Nani asiyemjua mfalme Daudi katika biblia? Huyu alikuwa wa wanawake wanane waliotajwa, na vimada kadhaa ambao hawakutajwa. Na Mfalme Solomon je? Naye hamumfahamu? Haya, huyu alikuwa na wanawake 700 na vimada 300. Dr Slaa ana mmoja!
Baadhi ya marais mashuhuri waliokwisha kusifika duniani, walitokea kuwa na vimada! Rais Franklin Roosevert wa Marekani alikuwa na mke wa ndoa, Eleonor. Lakini kwa pembeni alikuwa na wa moyo wake, Lucy Mercer. Mwaka 1918 Eleonor alipogundua mahusiano hayo, Roosevert alimuacha Lucy. Lakini miaka michache baadaye Roosevert alipokuwa rais, Mapenzi na Lucy yakanoga kuliko hata mwanzoni. Roosevert alipofariki mwaka 1945 huko Georgia, kimada Lucy Mercer, alilia hadi akazimia. Roosevert anasifika hadi leo kwa uongozi wake uliotukuka. Ngono haikumuathiri!
John F. Kennedy hadi leo wamarekani wanamjua kama "Ladies man"- Bwana wa mabibi. Huyu alikuwa mtaalam wa ngono! Pamoja na kwamba alikuwa na mke wake wa ndoa aliyejulikana kwa jina la Jacquiline, alikuwa pia na vimada wengine kibao akina Judith Exner na Marilyn Monroe. Na mara nyingi alitumbukia nao White House. Pamoja na ngono, anajulikana kwa utendaji wake mzuri, hadi uwanja wa ndege wa Kimataifa huko New York unajulikana kwa jina lake, J. F Kennedy International Air Port. Huyu naye, ngono haikumuathiri.
Bill Clinton na Monica Lewinsky wanajulikana sana kwa mahusiano yao ya ngono. Lakini ni nani asiyemjua Clinton na utendaji wake wa kazi? Na huyu naye, ngono haikumzuia asifanye kazi zake.
Jacob Zuma, rais wa Africa ya kusini, anao wanawake watatu. Na wote wanajulikana kama first ladies. Na bado kwa pembeni, anazo nyumba nyingine ndogo nne. Jumla wanawake saba. Dr Slaa ana mmoja..
Nani asiyemjua mzee Nelson Mandela? Huyu alimwacha mke wake wa ndoa, akaoa mke wa mtu mwingine. Alimuoa mke wa Samora Mashel. Wala sifa ya Mandela haijapungua mpaka leo, mpaka kesho. Sasa sijui ninyi CCM mnatuletea utumbo gani! Hoja za kuacha mke na kuoa mwingine wala hata hazina mvuto zikilinganishwa na hoja za wizi na ufisadi! Poleni sana kwa kutapatapa!
Watanzania ni wa kuhurumiwa. Ni rahisi kurubuniwa hata na hoja ambazo hazina kichwa wala miguu. Ukimdondoshea kuku vipande wiwili vya almasi na punje mbili za mahindi, ni wazi atashambulia punje za mahindi na kuiacha almasi. Atafanya hivyo kwa vile akili yake imeishia hapo. Hana la ziada. Hana habari na thamani ya almasi!
Ndivyo watanzania wengi wanavofanywa na CCM. Uwezo wao wa mang'amuzi ya mambo umedumaa. Na CCM inatumia mwanya huo kuwarubuni. Waakati tunahangaika kujaribu kutupa macho huku na kule ili kujaribu kupeana mawazo juu ya maendeleo ya kiuchumi ya nchi yetu, na ni nani mzalendo wa kweli atakayetuvusha katika lindi la umaskini, CCM wanatupotezea lengo na kutuletea habari ya maisha ya mtu binafsi. Hawataki tuongelee almasi na dhahabu zetu zinazokwapuliwa . Wanataka uwezo wetu wa kufikiri uishie kwenye ngono.
CCM wamekuwa wakimtuhumu Dr Slaa kwamba ana kimada. Hii ni hoja finyu sasa ukiilinganisha na hoja za ufisadi zinazotolewa, ambazo zinahitaji majibu. Wanachokifanya ni kujaribu kukwepa kujibu maswali na hoja za msingi kuhusu ufisadi. Baadala ya wananchi kufikiri na kujadili mambo yanayohusu uchumi wa taifa lao, waanze kufikiri na kujadili juu ya maisha ya mtu binafsi.
Iwapo Dr Slaa ana mwanamke, shida iko wapi? Mbona ni ishara nzuri kwamba, walau ni mwanamme, tena dume la mbegu! Na hata ukimtazama Dr. Slaa usoni, unaona ana sura ya kiume! Anao uwezo wa kuoa! Na hilo haliwezi kuathiri uwezo wake wa utendaji kazi. Rais wa Afrika ya kusini anao saba. Dr Slaa anaye mmoja! Sijui iwapo Makamba ulikwishafika Swaziland. Kama hajafika namshauri ufunge safari ukajionee mfalme Muswati ana wanawake wangapi. Yeye binafsi, hatuna sababu ya kumchunguza, anajijua mwenyewe!
Sasa tukianza kuchunguza maisha ya ndoa ya kila mtu, ni mwanamme gani atasimama? Wenye vimada ni wengi, hadi wanatia kinyaa. Viongozi wakuu wa CCM ndio wenyeviti wa ngono! Tuongelee dira na mwelekeo wa kiuchumi wa nchi yetu. Maswali muhimu yajibiwe, kuliko kukurupukia maisha binafsi ya mtu.
Tunataka mtu wa kutuonyesha dira za kimaendeleo. CCM isituyumbishe na hoja za ngono ambazo hazimjengi mtanzania. Baadala ya kujibu maswali ya msingi kuhusu ufisadi, mnatupachika tongotongo za ngono ili kutupotezea lengo. Tunataka kupata majibu ya kufaa juu ya maswali kuhusu ufisadi unaofanywa na watu wachache, huku mamilioni ya watanzania wakihangaika kila kukicha. Ee Mungu inasue nchi yetu katika mikono ya mafisadi!
Wewe mtanzania uliyeathiriwa na aina hii ya kimeta cha CCM, amka kumepambazuka! Achana na longolongo za CCM. Achana na akili za kuku kuishia katika punje za mahindi. Kura yako mpe Dr Slaa! Mwambie na mke wako, kura yake Chadema inaihitaji.
Usisahau kumpasha habari na mama yako kule kijijini. Mwambie kura yake ni muhimu sana kwa Chadema. Kila la heri. Ubarikiwe sana!
Mwenye maoni awasiliane nami kwa e-mail hii: mak.ralph
Source: Coment in Mwananchi, 2010-9-6