Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 19,151
- 43,102
Ng’ombe wakiwa wamewasili katika kiwanda cha Tanganyika Packers Kawe tayari kwa kuchinjwa na baadaye nyama kusindikwa na ngozi kuandaliwa kwa matumizi mengine.
Kisha baadaye mambo yakaw yale yaleeeee...kiwanda kikajifia zake tu, sababu hazijatajwa.....😃
Mji wa Kawe ulianza tangu miaka ya 1908. Kipindi hicho mji ulikuwa lilipo eneo la Makaburi ya Mzimuni (Mwai Kibaki road). Kufikia miaka ya 1960 baada ya kuanzishwa kwa kiwanda cha Tanganyika Packers palikuwa na njia ya kupeleka ng'ombe kiwandani, ambayo wazungu waliita "cow way" wakimaanisha njia ya ng'ombe. Wamatumbi wakashindwa kulitamka neno hilo na badala yake wakatamka KAWE.
Vitongoji vilivyokuwa vinapakana na Kawe kwa kipindi hicho vingi vilitokana na wakazi mashuhuri wa maeneo hayo, ikiwa ni pamoja na Kwa Mussa Hassan ambako ni Msasani, Michael Chain ambako sasa ni Mikocheni. Umbwelani ambako sasa ni pahala ilipo hosteli ya JWTZ, pia kwa Wakwama ambako sasa ni Ukwamani na upande wa Kaskazini walipakana na mashamba ya mkonge ya Asamali ambako sasa ni Mbezi Beach.
