Asemavyo Mkapa Kupitia BBC

Hii nchi ni bola iuzwe tugawane kila mtu achukue chake,anayetaka kubaki awe mtumwa abaki , anayetake akawekeze nchi nyingie poa, maana kila kukicha hakuishi vituko.
 
Pia ndiye aliyeweka ripoti ya Mzee Paul Sozigwa kapuni kama alivyosema EL hayo yote yanayofanyika sasa yasingekuwepo kama ile ripoti ingetumika.

Pia ndie alimbeba EL kwa kumpa unaibu Waziri wa Ardhi wakati anajulikana ni mpenda rushwa (na hakuchukua muda mrefu EL akataka kufanya maujanja na kiwanja kile cha shule ya chekechea kilicho karibu na CMC motors opp na Maktabu Kuu bahati Mzee Sabodo ambaye nafikiri alikuwa mwenyekiti wa hiyo shule alipinga kwa nguvu zote.

Bila hivyo hapo sasa pangekuwa ofisi za CMC), akadai eti ni wazeee wamshinikize na hata kusema chaguo ni Kikwete ni huyo huyo baada ya kutishwa.

Sasa mtu kama huyo ANAYETISHWA NYAU na akina EL na wazee hana ujasiri wa kusema ukweli si ajabu kuna wazee wammtisha na kumwambia kasema hayo aliyoyasema, kwanza hana hadhi ya kuwazungumzia Watanzania ni MCHAFU

Anafikiri watanzania wameshamsahau?


US embassy cables: BAE's 'dirty deal' to sell radar to Tanzania revealed

Tuesday, 24 July 2007, 14:06
C O N F I D E N T I A L DAR ES SALAAM 001037
SIPDIS
SIPDIS
AF/E FOR B YODER AND D MALAC
MCC FOR G BREVNOV AND M KAVANAGH
EO 12958 DECL: 07/23/2012
TAGS PREL, PGOV, ECON, EAID, KMCA, PINR, TZ
SUBJECT: BIG FISH STILL RISKY CATCH IN TANZANIA
REF: A. A. DAR ES SALAAM 1009 B. B. DAR ES SALAAM 00085
Classified By: D. Purnell Delly, Deputy Chief of Mission, for reasons 1 .4(b and d).
1. (C) SUMMARY. Tanzania's Prevention of Corruption Bureau (PCB) has never successfully prosecuted a high-level
corruption case involving either the private or public sector. On July 14, the Director General of the PCB, Edward Hoseah, assured the DCM that the PCB was now prepared to prosecute a milestone corruption case: the U.K.-Tanzanian BAE radar deal. Beyond plans to prosecute the BAE case, Hoseah painted a mixed picture regarding the Government of Tanzania's (GOT's) progress toward addressing the country's endemic corruption problem. On one hand, Hoseah highlighted recent legal reforms and the increasing willingness of both Parliament and press to level corruption charges against the government. On the other hand, he noted the unabated corruption in Zanzibar, weak capacity of his bureau, and President Kikwete's reluctance to implicate former President Benjamin Mkapa or members of Mkapa's inner circle in corruption scandals. Finally, Hoseah reiterated deep concern about his personal safety, explaining that he frequently received threatening letters. In the event of increasing threats to his life, Hoseah said he would not hesitate to seek refuge in another country. END SUMMARY.
PCB: Ready to Prosecute the BAE Radar Deal
 
Mkapa ni kama nguo chakavu,hana issue BBC walikosa kabisa mtu wa kumhoji hadi wakaamua kumhoji Fisadi walitegemea atasapoti upinzani?????lazima asifie chama kilichomlea hadi ameondoka ikulu akiwa ana kampuni wewe uliona wapi hiyo????kama ingewezekana Nyerere afufuke leo huyu atakimbia hadi afe,alinadiwa kwa kuambiwa yeye ni mr clear kaondoka ikulu akiwa mchafu na aibu tupu anapata wapi ujasiri wa kuvisema vyama vya siasa nje ya ccm.
 
Kweli la kuvunda halina ubani. HIvi mtu na akili yake anaweza kuanzisha kampuni halafu akaiita kwa majina yake na mkewe tena akiwa madarakani? Afu anwani yake anaandika IKULU. Tena kampuni hiyo hiyo ilisajiliwa silu ya tarehe 1/5 ambayo kwa kawaida ni sikukuu. Sasa mtu kama huyo anaweza kusema nini wakati huu. Mi ningekuwa yeye ningekaa kimya ana nisingependa kuonekana popote au kusema chchote.

yani jina lako kwa kihaya ni mkwaju..!banza ojajure mkapa. Kwanza wanauita mkapa mzee wanakosea.mzee ni mtu mhadirifu,mwenye staha,heshima nk. Ndo maana sehemu nyingne ata uwe mtu mzima ukifamble hakuna atakaekuita mzee. Huyu ni mwizi tu.
 
Huyu ni mchumia tumbo,hafahamu kuwa dunia ya leo haihitaji siasa uchwara na za kibabe.Asamehewe kwasababu ya umri wake.
 
lazima atetee katiba mbovu maana anajua katiba mpya itakua kitanzi kwake. Kwani kilicho mkuta chiluba hakijui? Lakini waache warukeruke muda ukifika hiyo katiba mbovu ndiyo kitanzi chao.Kumbuka hata zambia watawala walikuwa wanapiga chenga kuhusu katiba.Lakini upepo wa nguvu ya umma ukavuma,sote tunajua kinachoendelea zambia.Ila wakifanya kichwa ngumu tutawaonyesha nini maana ya nguvu ya umma .
 
Mkapa acha kudanganya ulimwengu. Unajua fika mwaka jana 2010 ni chama gani ilishinda. Kwanza ushukuru jinsi mnavyoendeleza wizi wa kura kwa sababu bila ivyo wengi mngekuwa ndani. Huwezi sema kuwa ccm hawawezi kushindwa katika chaguzi, Ni uongo ambao mmezoea ili kuwapumbaza walimwengu na wananchi ijulikane kuwa ccm inakubalika sana.

Wekeni tume huru uone ngoma yake. Mfano wenyewe umeona Igunga bila wizi ungeadhirika kwa kukipigia debe, ilibidi wizi lifanyike ili ccm ishinde, kukulindia heshima yako.

Ila kwa mawazo haya ustahili heshima hata kidogo ngoja tuone kama hutahama nchi hapo badae, kwa ajili ya matumizi mabaya ya madaraka. Ccm wazee wamezidi ili kulindana bora kuwachia vijana pia wakaongoza.

Vijana wenyewe kama ndio akina Ngereja, Nape, Malima, Masha and the like basi bora waendelee wazee tuu
 
kashaanza kuweweseka na midhambi aliyofanya. ngoja tu lazima ataionja joto ya jiwe maana wanajua upinzani ukishinda wao wanakesi nyigi za kuzima. Anayepiga kura si yeye bwana ni watanzania. Na kusema kwamba upinzani hauwezi kushinda wakati wanaiba kura na kwenye kampani wanaongozana NEC nzima nadhani lile gamba lake ni gumu kama la kobe. Hivi hawajamvua tu gamba huyu mzee?

Naye ameshaanza kupoteza heshima yake kwa watzanznia bila kujuwa kama alivyofanya mwenzake six. Ukianza kuusema upinzani vibaya wakati huu unatafuta kuchukiwa tu ndo maana wanamzomeaga kila anakokwenda hiloooooo
 
nimemsikia pia. Naheshimu sana mchango wake kwa nchi hii maana aliwezesha hataa sehemu watu walikuwa wamekata tamaa wakazinduka!
Lakini sisi sio malaika, baadae alichafuka! Sasa anajua fika kuwa ikija serikari nyingine nje na 'mitandao' yao waliyojijengea itakuwa ngumu kwake na anajua katiba mpya na hasa iliyokamilika lazima imsulubu tu!
Nashauri badala ya viongozi (hasa wastaafu kama Mkapa) kukalia porojo na unafiki, ingeundwa tume ya maridhiano ili kama wana nia ya kweli wajisafishe then twende mbele badala ya kung'ang'ania vitu visivyo na tija na manufaa yoyote kwa taifa hili masikini
 
Huyu mzee kwanza akae kimya maana hatujasahau alivofanya biashara akiwa ikulu kinyume na katiba!! halafu bila aibu ansema watu hawawezi kueleza kwa nini tume sio huru?? Alimuuliza nani akashindwa simply tume inayoteuliwa na rais wa jamhuri ambaye pia ni mwenyeketi wa CCM na mgombea urais kwenye uchaguzi utakaosimamiwa na tume aliyoteua, tume hiyo itakuwaje huru??

Katiba inasema matokeo ya urais yakishatangazwa na tume hakuna mahali au taasisi yoyote inayoweza kuyahoji hata mahakama, tume ipo juu ya mahakama?? huko nako ni kuvunja katiba maana katiba hiyohiyo inasema mahakama ndicho chombo pekee cha kusimamia na kutoa haki!!

Mzee anatetea katiba mbovu na CCM maana anajua siku ikiondoka madarakani lazima afikishwe mahakamani kujibu tuhuma za ANBEM, EPA, RADA, KIWIRA n.k kweli sasa amekuwa mvivu wa kufikiri!!


Kwanza Mzee Nkapa alishinda mara moja tu , mwaka 1995 alibwagwa na Mhehimiwa Mrema lakini NEC wakachakachua alipata ushindi kuptia katiba mboyo iliyokataza kuoji uhalali wa kura za rais akiwepo mapungufu, kwastail hii ni kama enzi zakupigia giza
 
Hivi BBC walikosa mtu wa kuhojiana nae mpaka wakaamua kumhoji huyo babu?kuna watu wengi wa kuwahoji wenye timam sio wezi kama Makapa.
 
huyu mzee kwanza akae kimya maana hatujasahau alivofanya biashara akiwa ikulu kinyume na katiba!! Halafu bila aibu ansema watu hawawezi kueleza kwa nini tume sio huru?? Alimuuliza nani akashindwa simply tume inayoteuliwa na rais wa jamhuri ambaye pia ni mwenyeketi wa ccm na mgombea urais kwenye uchaguzi utakaosimamiwa na tume aliyoteua, tume hiyo itakuwaje huru??

Katiba inasema matokeo ya urais yakishatangazwa na tume hakuna mahali au taasisi yoyote inayoweza kuyahoji hata mahakama, tume ipo juu ya mahakama?? Huko nako ni kuvunja katiba maana katiba hiyohiyo inasema mahakama ndicho chombo pekee cha kusimamia na kutoa haki!!

Mzee anatetea katiba mbovu na ccm maana anajua siku ikiondoka madarakani lazima afikishwe mahakamani kujibu tuhuma za anbem, epa, rada, kiwira n.k kweli sasa amekuwa mvivu wa kufikiri!!

kweli kabisa, huyu mzee anakera sana! Na akae kimya. Anafikiri watz wa leo ni wale wa enzi zao!
 
Mtu aliyehalalisha rushwa ya mahindi Igunga mbele ya hadhara na vyombo vya dola,hatutegemei asema cha maana.
 
Hivi alishatupa faida ya kufanya biashara ktk ikulu yetu?alisharudisha kiwira?alishatuomba radhi kwa kutuambia tuna wivu wa kike?anatuambiaje kuhusu radar na chenji imerudishwa?tumeshakula nyasi na ndege ya raisi imenunuliwa je inaleta mapato kwa kuwa tuliambiwa itakodishwa!huyu mzee akae kimya tu aache kutudhihaki
 
Mkapa naona amevimba kichwa watu wanaposema heri ya enzi za Mkapa. Ni dhahiri anaanza kujisahau, inafaa tumgeuzie kibao sasa.
 
Back
Top Bottom