AseeLindi ni kijijini wazee

AseeLindi ni kijijini wazee

Ujiji
Lindi ni sawa na Bagamoyo, Tabora, Ujiji, Zanzibar, Pemba, Tanga. Uislam na umwinyi umekuharibu mno, mtu anaona ufahari kushinda kavaa shuka tu akizunguka mitaani kusengenyana, hana kabisa wazo la kutafuta ama kufanya kazi.
Ujiji ni zaidi ya Lindi pa kijinga sana
 
Mkuu ulikua bweni gani? Mwongozo? Fidel Castro? Utawala Bora, etc. Unanikumbusha mbali sana.... Kila siku jioni kwenda beach
 
Yaani, ikitokea advance amepigwa kiboko hata kimoja basi utachekwa na kudharaulika miaka yote. Mambo yamebadilika, siku hizi hata kwenda beach ni kwa ruhusa......viboko kama vyote.
Ooh kumbe. Sisi paredi tulikua hatuendi, darasani pia ukipenda. Ni miaka mingi kidogo. Nilimaliza pale 19 years ago.
 
Ila watu wa pale wanaheshimu sana wanafunzi, unaweza ukapishwa seat na mtu size ya dingi yako, kisa tu umevaa t-shirt la lindi seko.

Lindi seko ilikuaga poa sana, ni bweni lakini ukiwa mzembe unapangishwa kitanda 😄

Pale wanafunzi wameacha sana watoto, maeneo yanayoizunguka shule.

Watoto wa maeneo yale wanakujaga sana kula pale shuleni, na mara nyingi hawakatazwi kwa sababu ni watoto walioachwa/waliotelekezwa na wanafunzi.

Lindi seko kuna wanafunzi wengine walishalowea pale pale shule, unakutana na li dingi saizi ya baba ako mnalala nalo bwenini.

Mengine ni malima mchicha, unaweza kudhani labda ni ticha kumbe mkaazi mwenzio 🤣

Asubuhi nyie mkiamka kwenda darasani na lenyewe linaamka kwenda kwenye harakati zake, usiku mnakutana bwenini, mnapiga stori, wewe unalipa za darasani lenyewe linakupa stori za mtaa 😄 🤣

Yalikujaga kusoma hapo kitambo, baada ya kumaliza shule yakaamua kubaki pale pale shule miaka na miaka(haya ndio ma ving'ang'a sasa 😄)

Mie niliendaga pale kikomando sababu O- Level nilisoma boarding ya kibabe vile vile.

Nimefika pale na kibegi na ndoo ndogo ya lita kumi, mpaka patroni akashangaa akasema "ulivyokuja hivyo utalalia chaga?
nikamjibu sijaja kulala nimekuja kusoma.

alivyonionesha kitanda changu akashangaa natoa godoro na ndala kwenye ndoo ndogo(kupeki hivi walinifundisha wanyasa/watu wa Malawi)

Kuna dogo usiku ametoka darasani kuingia bwenini anakuta mtu kalala kitandani kwake kajifunika gubigubi, dogo kuona hivyo akawa mbogo, akaanza kukitikisa kitanda anamwambia jamaa toka kwenye kitanda changu, tooookaaa.

Ile kufunua shuka akakutana na dingi lina ndevu kama zoote, ikabidi aamkie kwanza, halafu jamaa likamwambia nenda nje kaangalie namba ya bweni, dogo alipotoka anaangalia kumbe amekosea bweni, kilichofuata 😄

Kuona nyoka ni kila siku mpaka unazoea

Watu walimchoma spoku iliyowekwa kwenye moto ng'ombe wa shule ili wale nyama.

Nashangaa eti watu wanataka kuandamana ng'ombe wa shule achinjwe kwa sababu wameona anaumwa na ameanza kudhoofu,

kumbe mijamaa imeshamchoma spoku inajua iwe isiwe ni lazima aliwe.

Lindi na kahama ni masai na samaki, tofaaauti kabisa.

Ikitokea Watu wooote wa pale lindi mjini wakahamishiwa kahama mjini watatoshea pale kahama stendi tu, kahama nyingine yoote inabaki tupu.

Ukisimama katikati ya lindi, ukirusha jiwe kuelekea upande wowote ule linadondokea mpakani.

Lindi ni ndogo kama mchanga asee!!!

Hata mzunguko wa pesa ni pale pale, ndio maana noti za lindi zimechakaa.

Noti atakayoikataa konda wa daladala dar, ukiipeleka lindi dukani inapokelewa.

Ukitaka kufilisika, nenda kaanzishe biashara ya pesa chakavu lindi.

Sema ni miaka mingi imepiga patakua labda pamebadilika
Wewe unaizungumzia lindi gani?

Huwezi kusema lindi ndogo wakati Lindi ni miongoni mwa mikoa mikubwa kwa neo hapa Tanzania

Wewe umeenda Lindi sekondari halafu unajifanya unaijua Lindi

Halafu ukisema Lindi ni Chaka inategemea unafanisha na wapi, Kuna mikoa ipo Chaka bora ya mkoa wa Lindi
 
Lindi ni sawa na Bagamoyo, Tabora, Ujiji, Zanzibar, Pemba, Tanga. Uislam na umwinyi umekuharibu mno, mtu anaona ufahari kushinda kavaa shuka tu akizunguka mitaani kusengenyana, hana kabisa wazo la kutafuta ama kufanya kazi.
Dodoma kakuharibu nani?

Maana ukiachana na pale mjini mkoa wote wa hovyo

Kule Kuna waislamu wengi??
 
Wewe unaizungumzia lindi gani?

Huwezi kusema lindi ndogo wakati Lindi ni miongoni mwa mikoa mikubwa kwa neo hapa Tanzania

Wewe umeenda Lindi sekondari halafu unajifanya unaijua Lindi

Halafu ukisema Lindi ni Chaka inategemea unafanisha na wapi, Kuna mikoa ipo Chaka bora ya mkoa wa Lindi
Lindi ni kijiji mzee nimeishi miaka 5
 
Lindi ni ndogo sana, maeneo mengine ni pori na bahari
Lindi unazungumzia Lindi unayoisema, RUANGWA, Nachingwea, Liwale,

Hata Tabora ambao ni mkoa mkubwa Tanzania ni pori kwa sehemu kubwa

Unatoka Tabora mjini unaenda katavi, unaonaje ule msitu mkubwa
Hamna mkoa mkubwa uliokuwa hauna mapori

Pwani yenyewe tu ina mapori kibao ambao ndio mkoa umepakana na mjini DSM
 
Back
Top Bottom