Nilikuwa napinga sana ujio wa ndege, nikatoa hoja kedekede kwamba si kipaumbele.
Lakini baada ya mimi mwenyewe kuonja unafuu wa usafiri huu, nimesema asante mheshimiwa Raisi kwa uamuzi wa kishujaa kutuletea ndege.
Nimesafiri kutoka Bukoba kuja Dar kwa kutumia ndege yetu ya Bombadia kwa shilingi 325000, Japo bado ni nyingi sana lakini ni unafuu kuliko ile kampuni inayoanza na herufi P ambao wao ni zaidi ya shilingi 600,000, lakini pia ni nafuu kuliko kuunganisha ndege ya Auric +Fastjet.
Mheshimiwa Raisi, japo kuna unafuu ninakuomba juhudi ziendelee ili bei iweze kushuka zaidi na Watanzania wengi wanufaike na usafiri huu.
Pia nimegundua kuwa kwa sisi kuwa na shirika letu bora la ndege na la kisasa itarahisisha movement ya Watalii ndani ya nchi, Ifahamike kuwa Utalii ni sekta inayoongoza kutupatia fedha za kigeni, kwa hiyo ni muhimu sana kuwa na shirika la ndege imara ili kuhudumia sekta hii.
Zidumu Bombadia, na Zidumu juhudi sahihi za mheshimiwa Raisi wetu!