Kabende Msakila
JF-Expert Member
- Oct 7, 2020
- 1,398
- 1,264
WanaJF
Salaam!
Maji hufuata mkondo wake - Rais wa awamu ya pili wa JMT alijizaa mfano wake. Hussein Ally Hassan Mwinyi (Rais wa sasa wa nchi ya Zanzibar) ni kiongozi shupavu na mwadilifu sana!
Chini ya uongozi wake naiona Zanzibar inayofunguka - naiona Zanzibar inayobadilika - naiona Zanzibar inayokua.
Aidha, rekodi zake akiwa Waziri wa Serikali ktk JMT kwa nafasi ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa sikuwahi kusikia, kuona ama kupata taarifa inayomtuhumu na ufisadi wa mali na rasilimali za taifa. Hii inanisukuma kumpa "BIG Up". Mengine nayompongeza ni:-
(a). Kukubali maridhiano kati ya Serikali yake na upinzani hususan ACT Wazalendo. Kwa utamaduni wa CCM si rahisi kukubali kufanya kazi ya ujenzi wa taifa kwa kushare madaraka!
(b). Miradi ya mikakati ya utafiti na uchimbaji mafuta, ujenzi wa barabara au daraja toka Zanzibar mkp Dar, ujenzi wa barabara za mitaani, utoaji mikopo kwa Jamii ya wazanzibar, uwajibishaji viongozi wazembe - kama aliyepata ajari tz akaachwa tu nk hivi ni baadhi ya vitu vinavyovutia sana.
(c). Kutopenda kutukuzwa - wapo viongozi wanapenda utukifu uliopitiliza, wanaofumbia uovu hasa ufujaji mali za umma (rejea taarifa za CAG) zinavyofunikwa na baadhi ya viongozi.
Nasema, Hussein Ally Hassan Mwinyi hongera sana kwa kazi na utumishi uliotukuka.
Msakila Kabende
Kakonko
Salaam!
Maji hufuata mkondo wake - Rais wa awamu ya pili wa JMT alijizaa mfano wake. Hussein Ally Hassan Mwinyi (Rais wa sasa wa nchi ya Zanzibar) ni kiongozi shupavu na mwadilifu sana!
Chini ya uongozi wake naiona Zanzibar inayofunguka - naiona Zanzibar inayobadilika - naiona Zanzibar inayokua.
Aidha, rekodi zake akiwa Waziri wa Serikali ktk JMT kwa nafasi ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa sikuwahi kusikia, kuona ama kupata taarifa inayomtuhumu na ufisadi wa mali na rasilimali za taifa. Hii inanisukuma kumpa "BIG Up". Mengine nayompongeza ni:-
(a). Kukubali maridhiano kati ya Serikali yake na upinzani hususan ACT Wazalendo. Kwa utamaduni wa CCM si rahisi kukubali kufanya kazi ya ujenzi wa taifa kwa kushare madaraka!
(b). Miradi ya mikakati ya utafiti na uchimbaji mafuta, ujenzi wa barabara au daraja toka Zanzibar mkp Dar, ujenzi wa barabara za mitaani, utoaji mikopo kwa Jamii ya wazanzibar, uwajibishaji viongozi wazembe - kama aliyepata ajari tz akaachwa tu nk hivi ni baadhi ya vitu vinavyovutia sana.
(c). Kutopenda kutukuzwa - wapo viongozi wanapenda utukifu uliopitiliza, wanaofumbia uovu hasa ufujaji mali za umma (rejea taarifa za CAG) zinavyofunikwa na baadhi ya viongozi.
Nasema, Hussein Ally Hassan Mwinyi hongera sana kwa kazi na utumishi uliotukuka.
Msakila Kabende
Kakonko