Asante A-G Werema kwa kuturejeshea Tanganyika yetu

Asante A-G Werema kwa kuturejeshea Tanganyika yetu

Hoja aliyokuwa anaiwasilisha Mnyaa ilikuwa mahsusi kwa Zanzibar na ndo maana akaambiwa akaulize huko kwao

Sasa hapa unakubaliana ya kuwa Tanganyika imevaa koti la muungano. Kama maswala ya Zanzibar ambayo si ya muungano hayapaswi kujadiliwa/kufafanuliwa katika BUNGE la JAMUHURI, Je maswala ya Tanzania Bara (Tanganyika) ambayo si ya muungano huwa yanajadiliwa wapi?
 
Hoja aliyokuwa anaiwasilisha Mnyaa ilikuwa mahsusi kwa Zanzibar na ndo maana akaambiwa akaulize huko kwao

Kwa hiyo ingekuwa ni mtoa wa mada wa Kagera kwa mfano, angeambiwa kaulize huko kwenu?!
 
huu muungano kisheria haufuction,
umekaa ki yakhe yakhe salama tu bwana.
werema n mwanasheria, hivyo amemjibu kisheria.
hivyo kama huyo mbunge anaona amedharirishwa aombe wanasheria wamfafanulie.
 
Hoja aliyokuwa anaiwasilisha Mnyaa ilikuwa mahsusi kwa Zanzibar na ndo maana akaambiwa akaulize huko kwao

We kweli hamnazo,sasa mbona aliomba msamaha kama alichoongea ni sahihi?
 
Huyu WEREMA sijui ni ushamba au ndo Cheo kimemlevya... Yuko arrogant sana... Kwa kweli jinsi anavyojibu maswali huwa anakera maana dharau na kiburi imemjaa..

Nitashangaa Sana Wazanzibar wengine wakizidi kumkumbatia... Huu Muungano ulishakufa na kama walivyosema Jini lake limeshatoka kwenye chupa haliwezi kurudi
Kauli ya Werema ilitosha kuwaput off wazanzibar wote ndani ya bunge lile! Lakini unafiki wa kura ya wazi unawatafuna hasa wale wa CCM. Wanajua kuwa wanabaguliwa, wanaibiwa kama Lissu alivyobainisha, na wanaonekana majuha lakini kura ya wazi inawatesa! " Nisije nikaonekana!"
 
CCM hatuna tena sababu za kupinga kurudi kwa Tanganyika. CCM hatuna haja tena ya kupinga Serikali tatu. Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Mwita Werema amenena.Amenena kwa ufupi lakini katika ujumbe mkubwa sana. Ya kwamba, Dodoma ni Tanganyika na si Zanzibar. Tumemsikia akimwambia Mbunge Habib Mnyaa "kaulize huko huko kwenu Zanzibar.....hapa kwetu".

Haya si maneno ya mzaha. Haya si maneno ya kuyapuuza. Aliyeyasema;alipoyasemea;na alichomaanisha ni vitu 'serious' sana. Mwanasheria Mkuu wa nchi amesema...mnataka aseme nani tena kurudi wka Tanganyika? Ni huyu huyu Werema ndiye aliyedai mwanzoni kabisa kuwa Tanzania haihitaji Katiba mpya. Sasa anaitaka na Tanganyika.Yuko kinyume na CCM yetu.Yuko kinyume na Serikali mbili.

Jaji Werema lakini ni mbaguzi na aliyejaa kiburi cha madaraka. Hata kama kutakuwa na Serikali tatu kama anavyotaka,bado Wazanzibari wataendelea kuwa ndugu zetu. Halafu, ina maan Jaji Werema hajui kuwa Dodoma kuna Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? Mambo ya kwenu na kwetu yanatoka wapi? Asante A-G Werema kwa kuirejesha Tanganyika lakini ubaguzi haufai.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Siku zote njia ya mwongo huwa ni fupi, na mwishoni ukweli unaonekana.
Wanajua wazi ya kwamba Muungano walishauvunja, hauna uhalali, na bado wanang'ang'ania ya kwamba Muungano uwe wa serikali mbili na yeyote anayeuliza ama kudai serikali tatu basi ni muasi, anayetaka kuuvunja Muungano. Lakini kwenye ufanyaji kazi wao na utekelezaji wa majukumu yao wanafahamu wazi ya kuwa hawataweza kuendelea na mfumo huu uliopo wa Muungano. Matokeo yake ndiyo hayo ya kuropoka hasa wanapobanwa na kujikuta wameongea 'ukweli hadharani'!
Hakika, Tanganyika yetu inarudi. Asanteni sana UKAWA, endeleeni kukoleza moto!!!
 
Back
Top Bottom