sasa baad ya yote hayo bado anamsikiliza mumewe kweli? ni mume huyo sasa!??:angry:
Duh! Hii ni ngumu, wanaume wauza sura ni shida sana, anataka kulelewa na wanawake. Huyo dada ausikilize moyo wake tu, kama ana amani, amsamehe na aendelee kuishi na mumewe. Ndoa zina siri nyingi sana. Akumbuke pia - hakuna guarantee kama akimuacha mumewe ndio atapata furaha huko aendako lol!
Yaani ni ngumu sana ila kwa vile anawapenda wanae basi akae hapo kwa lengo kwamba "yuko hapo kwa faida ya watoto" yaani anawasindikiza watoto wakifika mahali watakapoweza kujitegemea wenyewe basi na yeye achukue ustaarabu wake.
hana kazi yyt..na mama yake saiv kastaaf..so anawaza namna ya kuwalea wanae pia..na pia ushauri huu alipewa siku nyng sn..haufanyii kazi
Yaani ni ngumu sana ila kwa vile anawapenda wanae basi akae hapo kwa lengo kwamba "yuko hapo kwa faida ya watoto" yaani anawasindikiza watoto wakifika mahali watakapoweza kujitegemea wenyewe basi na yeye achukue ustaarabu wake.
Kama haufanyii kazi kwa maana hawezi kubeba wanae na kukimbia nao mbali iwezekanavyo basi akae tu andelee kuwalea hapo hapo kwa title ya "maid". Ila asilalamike kwa ndugu wala marafiki kuhusu baba wa watoto wake.
yaan mpaka bs..ni vitu ving ashamfanyia huko nyumakuna wakat alimfumania na akiwa nyumba ya jiran na house girl wa apo kwa jirani,ila yy dada ndo aliambulia kipigo cha hali ya juu,akavuliwa nguo zote akabaki na nguo ya ndani tu..majirani ndo walikuja kumsitiri na kanga..wakamshaur akatoe taarifa polisi.. iyo kesi yy mwenyew dada aliifuta bila kujilisha ndg.
Basi akili yake imeganda. Angekuwa ndugu yangu ningemtandika vibao vya nguvu ili azinduke!apo ndo penye kaz tena..haish kulalamika..anasaidiwa kimawazo hafanyii kazi,kuna kipind alipewa mtaji,akaanza biashara ilipoanza kua imara akamkabidhi mumewe hela ya mtaji+ faida na bidhaa ili aendeleze biashara ile,ilipoishia,hakuna anaejua
ku run anasita.anaumia kuwaacha wanae..maana kaambiwa na mumewe uyo akitaka kuondka aondokepeke yake..
kwani alishajaribu kuondoka nao ikawaje? mana anamfanyia mwenzie unyama... sheria ya ndoa ya Tanzania inatambua kabisa ndoa za kimila angeweza kwenda mahakamani sema sasa huo upande wa pili kwa kuwa una mshiko inaweza chelewesha kupata haki yake si unajua tena mambo ya hapa kwetu... hapo kama anaweza kujisimamia mwenyewe anaweza kujisogeza tu akaangalia ustaarabu mwingine wa maisha mana magonjwa ndo hatari zaidi.