Arusha hakuna Dola kabisa!

Arusha hakuna Dola kabisa!

Niko hapa arusha kikazi kama wiki sasa!

Kilicho nishangaza ni kwamba USD hakuna kabisa, yani kuanzia maduka ya kubadili fedha mpaka benki zote hakuna!

Sasa najiuliza, je hii ni kawaida?
Si tulisikia wamerudishiwa hela zao!!? Sasa wamepeleka wapi??? Kwanini mlimtukana JPM?

Ha ha haaa wahuni siyo watu
 
Ina maanisha utalii Arusha imeshuka Sana kwasababu ya propaganda za utalii wa Zanzibar....it doesn't make sense brother
Yaani inashangaza kabisa, ni uongo wa dhahiri uliopikwa kimajungu majungu
 
Mama amefungua uchumi sasa dolla kwanini hazipo?wakati WA dictiteta watalii hawakuwepo na COVID na miaada na mikopo ikakatwa lakini dolla zilikuwrpo.Nini kimetikea wakati kila kitu Hali ni nzuri
Akili zako ni ndogo sawa na Mwandazake
 
Alafu Mwigulu Nchemba aliwalipa wafanyabiashara wa Arusha dola za kutosha, kwa kisingizio kwamba walinyang'anywa na Magufuli
Kama kweli aliwapa basi alifanya jambo zuri, kwani yule muovu Jiwe aliwatenda vibaya sana
 
Nikajua dola serikali kumbe dollar USD ya mabeberu. Hiyo sio Arusha pekee hata huku Dar ukienda hata $500 kupata ni mzozo.

N:B watanzania tumieni madafu achaneni na dollar
Unaweza kuagiza machines za kufanyia kazi zako kutoka China kwa madafu?? watu wanataka dollar kwa ajiri ya importation sio kununua kilo ya nyama, nchi haina mafuta tatizo ni hilo hilo hatuna dollar, bila dollar uchumi utaanguka vibaya sana
 
Ina maanisha utalii Arusha imeshuka Sana kwasababu ya propaganda za utalii wa Zanzibar....it doesn't make sense brother
Basi hizi ndege ziache kufaulisha kutoka Zanzibar to Arusha or kwenye parks and safari en route same day tuone kama wageni watalala hapo airport ili kesho waanze safari asubuhi kwa utulivu!
Ratiba ya hizi domestic flights sio rafiki kwa uchumi wa utalii kwa mzawa wa chini!
Flights zote zitoke jioni ama sivyo muundo wa itineraries uanze na layover kesho safari zianze sio tua dandia gari kimbia ruka haifai hii inamnyima mtalii kuifurahia na kuijua nchi!
 
Ubinafsi wa kuwaficha watalii zanzibar na kuongezeka kwa hizi ndege ndogo zinazo faulisha wageni kutoka zanzibar hadi hifadhini zimegeuza hifadhi za kaskazini kuwa za day trips! Mahoteli na lodges zoote mijini Arusha wanalalamika hawana wageni tena! Kwanza huko maporini zinatusumbua nimakelele mtindo mmoja, haka kanatua haka kana paa mara haka kana onyesha views yaani pollution of noises kwa wanyama na inaondoa hadhi ya kuwa sasa huko hifadhini!
Zipangieni plan rafiki
Miji ya kaskazini haina tena mafuriko ya wageni kama zamani na matamasha hakuna tena!
Mfumo wa marketing wa TTB hauonekani ukibalansi hii biashara!
Mgeni mathalani anakuja na budget ya shopping na kuspend $25,000!
Unamlazimisha akazitumie zoote Zanzibar kiuhalisia hawezi kuzimaliza!
Kwanza hizi rizki haziendi kwa watu wa chini kama zamani! Maana humo humo mahotelini mnapowalazimisha wakae ndio huko huko huuziwa vitu vyoote mahotelini nakumnyima mjasiria mali wa chini kupata rizki!
Malipo mengi ni online transactions! Wengi hulipia hukohuko nje so zinazokuja hapa ni peanuts moja tu ya ku run safari!
Ni aibu kwa taifa hatutaki wageni waijue nchi , wajichanganye na jamii, watu wazawa wanufaike kwa mantiki hii utali hauna faida kwa mzawa!
Bara bara ndani ya parks zinahariba , ajali ni nyingi lakini ukiangalia kinachosababisha ni mafuriko ya wageni yaliyopangiwa itineraries zisizo rafiki na muda wa kutalii kwa kutulia, ni haraka haraka kukimbia kimbia ilimradi tu mtalii awahi ndege kurudi zanzibar! Ukweli watalii wanauchukia huu mfumo!
Zamani mgeni anasafiri 14 days anaifurahia nchi! Sasa hivi nikimbia kimbia ameona wildlife hajaona ruka eudi Zanzibar!
Sio lazima waziri atafute plans ningeshauri wizara ikutane mapema na waongoza watalii maana wanalalamika na kunakuwa na exchanging words kati ya mgeni na muongoza watalii na kibaya zaidi travel agents wa zanzibar kuwapa wageni wrong informations hususani kuhusu Tanzania mainland sio professional! Unapomwambia mgeni unaenda nchi ya Tanzania uwe makini ni wezi hivyo usinunue chochote uje ununue huku nchi ya Zanzibar hii is very primitive and shallow mind conversation! Zanzibar hamna ebony tree kule na sisi tukianza kuwaambia mnawauzia vifuu na dating palm tree products itakuwaje!!?
Please, Minister shufhulikia hili na mkihitaji ushauri kutana na WAONGOZA WATALII hawa ndio wanai market nchi achana na hawa wa maofisini!
$$ kwa wote
Kuna mambo umeyaandika, ni ya kweli na nipoambiwa yalinikera sana.

Hii swala la watalii kuvutwa Zenji na kuambiwa Bara ni hovyo ni la kulipigia kelele kwa kweli.

Kaskazini hatukuzoea "excursionists" kama ilivyo sasa.

Yale yale ya South Africa kumarket tourism attractions zao kupitia Mt. Kilimanjaro kama " ukitaka kuupanda Mlima Kilimanjaro ni masaa matatu tuu kutoka Kruger National Park" huko Thailand,Malaysia,Singapore,Taiwan na Hong Kong.
 
Kuna mambo umeyaandika, ni ya kweli na nipoambiwa yalinikera sana.

Hii swala la watalii kuvutwa Zenji na kuambiwa Bara ni hovyo ni la kulipigia kelele kwa kweli.

Kaskazini hatukuzoea "excursionists" kama ilivyo sasa.

Yale yale ya South Africa kumarket tourism attractions zao kupitia Mt. Kilimanjaro kama " ukitaka kuupanda Mlima Kilimanjaro ni masaa matatu tuu kutoka Kruger National Park" huko Thailand,Malaysia,Singapore,Taiwan na Hong Kong.
Yaani inakera!
Sijui kwanini hatutaki kutumia akili mpya katika kubuni aina za marketing!
I'm pretty sure ikitokea tuwafanyie interviews ya kushitukiza hapo wizarani japo ya kuandika itinerary ya siku nne nights tatu nauhakika hakuna atakaye faulu!
 
Back
Top Bottom