Arusha haikulengwa dini...

Status
Not open for further replies.

Mkuu hapa hakuna uchochezi huo ndo ukweli ninachoamini mimi ni kuwa si waislam wote wana chuki dhidi ya ukristo ila ni waislam wachache wanaofadhili na kutekeleza unyama huu,Tatizo linakuja pale waislam wanapoungana kupinga haya madai,Tukiungana kwa pamoja kila mmoja kwa imani yake kuvikataa vitendo hivi Tanzania itakuwa salama.
 

Mficha uchi hazai na mficha maradhi kifo umuumbua tafakari izo methari halafu urudi umu utuambie umeelewa nini...kama umeanza VILOBA mapema acha nenda kapumzike.
 

'mbona wanaotajwa kulipua bomu ni wakisto victor, jeseph n.k'
 

Taaabu ya baadhi ya watu ni urahisi wao wa kurubuniwa na kuaminishwa kwao kuwa kila kitu kinachovumishwa na watu wa mlengo wake...

hawatumii akili zao. Wala hawana haja ya kudadisi ama kufanya tafakuri ya kina na ya kimantiki kuhusu matukio yanayojiri nchini na duniani kote.

Ni wavivu wa kufikiri kwa vichwa vyao; na kwa sababu hiyo wamebaki kuwa wa kulalamika na kuamini hoja nyepesi nyepesi zinazopenyezwa na wajanja ambao kutokana na uzuzu wetu wanaweza kuusambaratisha umoja na mshikamano wetu kwa kutumia chambo maarufu ya siasa na udini...Halafu eti tunajifanya wajanja!!!!.....
 
Ni kweli lile shambulia halikuwalenga Wakristo lililenga wafanyabiashara maana ndiyo wanamgogoro mkubwa na hawa watu walio muua mchungaji kule Zanzibar
 
Kweli mkuu wanaoua mapadri na wachungaji na kuchoma makanisa na leo wametupa au kutega bomu kanisani tuseme na kuamini ni siasa tu si udini?HIZO NI FIKRA MGANDO !
 

una uhakika waislam hawana shda na wakiristo? Hzo chuk mnahubr za nin?
 
Hata kama tunatakiwa kuheshimu uhuru wa kutoa maoni, kwa hili acha tusivumilie
 

kwanini hawakulenga soko kuu au ngarenaro.

kumbuka: hakuna ban kwa wasioanzisha uzi ama kuchangia - unaweza ukawa msomaji kama mimi
 
Af wewe usinitie hasira nakwambia, tena acha kutuzingua.Tunauchungu wenzio.Ficha upumbavu wako
 

umepewa makuzi ya kinafiki
 

Sasa wewe unaposema upotoshaji, unamanisha unachosema wewe ni ukweli?
Naomba unijibu swali hili
Nini motivation ya mlipuaji/ walipuaji katika jumuiya wa wakatoliki tena siku ya tukio kubwa kama hilo wakati mikusanyiko ya CDM na CCM ni mikubwa kuliko ya kanisa?
Kama amewalipua wakatoliki huoni kwamba dhehebu moja limeathirika bila kujali mlipuaji/walipuaji walilenga udini au kitu gani?
 

Huoni aibi?
 
Mkuu Petro E. Mselewa

Nimekusoma vyema imenibidi nirudie mara mbili ili kujiaminisha kile ninanchokisoma ni sahihi au ni mauza uza ya hivi mvua zinazonyesha Arusha bila mpangilio.

Umedai shambulio la Arusha halikulenga UKRISTO/UKATOLIKI.Sawa pengine ungetueleza sababu za kutuaminisha ningekuelewa.Wahusika wakuu ni waSaudia Arabia ambao ni waIslamu wamemtumia muendesha boda boda masikini asiyekuwa na uhakika wa mlo wa siku kwenda kurusha bomu kwenye Ibada KANISANI halafu unatuambia halikulenga wakatoliki/wakristo.Baada ya shambulio haukufanyika wizi wa sadaka,wizi wa kitu chochote bali wapangaji wa shambulizi walikuwa wanatimkia Kenya baada ya kufanyakazi nzuri ya kua,kujerui na kuharibu mali za KANISA.

Najua huu ni msimamo wa serekali yetu ambayo imeshindwa kutuambia mpaka leo watesaji halisi wa Dr Ulimboka,wameshindwa kuwakamata mpaka leo washambuliaji wa nyumba za IBADA [MAKANISA] ambayo yamekuwa ni sehemu ya malengo ya mashambulizi kuanzia ZANZIBAR,TANGA,DAR na sasa ARUSHA.

Viongozi wa wakuu wa makanisa Tanzania wanatakiwa kuanzia sasa wawatangazie waumini wao kwamba serekali imeshindwa kuwalinda dhidi ya maadui wanaofahamika,wawatangazie kwamba serekali imekuwa ikiwadanganya mara zote inapenda amani lakini imeshindwa kuwakata na kuwafungulia mashtaka wasamabazaji wa kanda zenye mihadhara ya kashfa,imeshindwa kumkamata Ilunga na genge lake la magaidi.
 
Last edited by a moderator:
sio kusema ni uchochezi bali nikujiuliza swala muhimu....kwanini kanisa lishambuliwe??
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…