ScreenMaster
Member
- Nov 26, 2011
- 12
- 4
Wakuu,
Leo hii JK alikuwa huko Monduli Arusha kutunuku kamisheni za Maafisa wa Jeshi.
Taarifa za kuwasili kwa JK Arusha zilianza ziku chache zilizopita ambapo ilikuwa apitie uwanja wa ndege wa KIA, ndipo aingie kwenye msafara wa magari hadi Arusha, kutokana na sababu kuwa kiwanja cha ndege cha Arusha kipo matengenezoni, na njia ya kurukia ndege imefupishwa.
Lakini wasaidizi wake walistukia mpango huo, ambao ungemlazimu JK kupitia Arusha mjini ili aende Wilayani Monduli, na wakatumia nguvu ya dola kuepusha JK kupita Arusha mjini kwa kulazimisha wajenzi wa kiwanja cha ndege cha Arusha kuondoa makatapila ya ujenzi kwenye njia ya kurukia, na wakatakiwa kushindilia njia ya kurukia japo temporarily, ili mzee apitie uwanjani hapo, na kwa jinsi hiyo kuepuka kabisa kupita Arusha mjini.
Hakika Arusha ni tishio kabisa kwa mkuu huyu!
Leo hii JK alikuwa huko Monduli Arusha kutunuku kamisheni za Maafisa wa Jeshi.
Taarifa za kuwasili kwa JK Arusha zilianza ziku chache zilizopita ambapo ilikuwa apitie uwanja wa ndege wa KIA, ndipo aingie kwenye msafara wa magari hadi Arusha, kutokana na sababu kuwa kiwanja cha ndege cha Arusha kipo matengenezoni, na njia ya kurukia ndege imefupishwa.
Lakini wasaidizi wake walistukia mpango huo, ambao ungemlazimu JK kupitia Arusha mjini ili aende Wilayani Monduli, na wakatumia nguvu ya dola kuepusha JK kupita Arusha mjini kwa kulazimisha wajenzi wa kiwanja cha ndege cha Arusha kuondoa makatapila ya ujenzi kwenye njia ya kurukia, na wakatakiwa kushindilia njia ya kurukia japo temporarily, ili mzee apitie uwanjani hapo, na kwa jinsi hiyo kuepuka kabisa kupita Arusha mjini.
Hakika Arusha ni tishio kabisa kwa mkuu huyu!