Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya msingi Oldonyo Sambu Wilayani Arumeru Mkoani Arusha, wanadaiwa kudondoka darasani kutokana na kushinda na njaa kwa muda mrefu.
Mtendaji wa Kijiji cha Lemanda Bw. Gaspar Lembris amesema adha hiyo inatokana na Wananchi kushindwa kuwalipia watoto wao ili wapate mlo shuleni.
Aidha, Wananchi wamesema kutokana na madadiliko ya hali ya hewa kwa msimu wa mwaka huu wa 2021 hawajapata mavuno yeyote mpaka sasa hivyo mbali na kushindwa kuwalipia watoto wao chakula shuleni pia wao binafsi wanaomba Serikali iweze kuwasaidia chakula kwakua wanakosa hadi mlo mmoja kwa siku.
Mtendaji huyo ameieleza kuwa mwanafunzi akidondoka anapewa soda na biskuti ndipo anapata nguvu, lakini wakati mwingine walimu hulazimika kwenda kuchukua chakula majumbani mwao na kuwapa pindi tatizo hilo linapotokea.
"nimeshashuhudia watoto wanne na mara nyingi ni matukio yamekuwa yakitokea ndani ya wiki, ukweli ni kwamba pia kwa walimu imekuwa ni kazi kwasababu baada ya saa nne ufundishaji kwa walimu unakuwa ni mgumu kwa sababu watoto unakuta wameishiwa na wengine kutoroka" Mtendaji, Gaspa Lembris.
Mtendaji wa Kijiji cha Lemanda Bw. Gaspar Lembris amesema adha hiyo inatokana na Wananchi kushindwa kuwalipia watoto wao ili wapate mlo shuleni.
Aidha, Wananchi wamesema kutokana na madadiliko ya hali ya hewa kwa msimu wa mwaka huu wa 2021 hawajapata mavuno yeyote mpaka sasa hivyo mbali na kushindwa kuwalipia watoto wao chakula shuleni pia wao binafsi wanaomba Serikali iweze kuwasaidia chakula kwakua wanakosa hadi mlo mmoja kwa siku.
Mtendaji huyo ameieleza kuwa mwanafunzi akidondoka anapewa soda na biskuti ndipo anapata nguvu, lakini wakati mwingine walimu hulazimika kwenda kuchukua chakula majumbani mwao na kuwapa pindi tatizo hilo linapotokea.
"nimeshashuhudia watoto wanne na mara nyingi ni matukio yamekuwa yakitokea ndani ya wiki, ukweli ni kwamba pia kwa walimu imekuwa ni kazi kwasababu baada ya saa nne ufundishaji kwa walimu unakuwa ni mgumu kwa sababu watoto unakuta wameishiwa na wengine kutoroka" Mtendaji, Gaspa Lembris.