Arfi anaiua CHADEMA wilayani Mpanda

Arfi anaiua CHADEMA wilayani Mpanda

Mambo mengine tuweke ushabiki nyuma na tuwe tayari kuongea na kusimamia ukweli. Mimi ni mwana chama hai wa CHADEMA. Mara ya kwanza nilipotoka chuoni, mwezi Juni mwaka jana nilikuta mji umebadirika kabisa. Zile bendera nzuri za CHADEMA ambazo zilikuwa zinaupendezesha mji, hazikuonekana tena. Maeneo mengi ambayo kulikuwa na Bendera za CHADEMA, nafasi yake ilikuwa imechukuliwa na bendera za ccm. Nilishangaa sana, na ikabidi niwaulize wenyeji niliowakuta. Jibu ambalo lilipata kutoka kwa wengi, walisema, bendera siyo issue, issue in mioyo ya watu, watu wako CHADEMA japo mashina yao yamewekwa bendera za ccm! Ilinichukua muda mrefu kidogo kuamini.

Najua wengi tunapenda kusikia mazuri tu kutoka CHADEMA, hata mimi ni mmoja wao, lakini kwenye ukweli lazima tuseme. Kama sijakosea, Said Arf alishinda kwa tofauti ya kura 47 katika uchaguzi uliopita, tofauti sana na uchaguzi wa 2005 ambapo alipata kura nyingi sana. Hili pekee linaonesha kukubalika kwake kumepungua sana. Japo anafanya kazi nzuri, lakini mvuto wake umepungua kwa wananchi na nafikiri ameshindwa kuwa na techniques za kuwavuta watu na kukubali sera za chama. Tusifarijiane, huyu Mzee atakiacha chama cha CHADEMA katika hali mbaya sana. Na anaposema kuwa haogombei tena, siyo kwamba hapendi, lakini ameshaupima upepo na ameona kuwa kukubalika kwake kunashuka kwa nguvu sana hapa Mpanda mjini na hivyo anataka amuachie mwingine aibu ya kushindwa ili yeye ajisifu kuwa ndiye alikuwa anaibeba CHADEMA MPANDA MJINI.

Tusibishane, ukweli daima utasimama, mimi binafsi nilisikitishwa sana na huyu Mzee kutupa kadi ya chama, eti kwa sababu alikasirishwa na vijana. Ina maana siyo mvumilivu kiasi hicho? Kuitupa kadi ya chama ni kukidhalilisha chama. Nilisikitika sana, na hata leo hii siamini kama kweli alifanya kitendo kile.

Hili suala la chama kukosa ofisi ya maana hapa Mpanda Mjini, nilizungumzwa sana, japo kwenye mikutano ya siasa tunafarijiana na kupeana moyo kuwa tuna mkakati wa kujenga ofisi kubwa ya mkoa. Lakini hiyo itachukua muda sana, kwa nini tusiwe na ofisi at least yenye hadhi kwa sasa wakati tunashughulikia hiyo ya mKoa? Huyu Mzee kweli amefanya mengi, lakini nafikiri kuwa atamaliza vibaya sana ubunge wake hapa Mpanda Mjini.

Kuna hii case ya gari la AMBULANCE kukaa nyumbani kwa mbunge. Mimi bado sijajua, ila nilisikia tetesi kuwa hizi gari zilitolewa na CHADEMA MAKAO MAKUU kwa kila jimbo ambalo lilikuwa na mbunge wa CHADEMA, na kwamba kwa mujibu wa maelekezo ya CHADEMA MAKAO MAKUU, ilitakiwa hizi gari zikabidhiwe kwa uongozi wa hospitali za mkoa au wilaya. Nasikia Ndesambulo na wengine walizikabidhi gari hizo kwa serikali kupitia uongozi wa hospitali husika, huku kwetu gari linakaa kwa mbunge. Mimi hofu yangu, jamaa anaweza akafuta yale maandishi "MBUNGE MPANDA MJINI CHADEMA" kama hatogombea tena uchaguzi ujao, na kama atagombea mwingine akashindwa, je itaendelea kuwa ambulance?

Lisemwalo lipo, kama halipo linakuja. Nafikiri tunahitaji kuwa na kikao cha vijana mkoa wa Katavi kwa ajili ya kujadili mustakabali wa chama hapa mkoani, vinginevyo, tutarudi nyuma ambako binafsi sipendi. Ni hayo tu!!!!

Huo ndio ukweli ila hawataki tuseme ukweli eti ukisema unitwa gamba.Hawa wenzetu wanaupofu sijui limbwata la Josephina linatudhuru wote?Wanani criticise bila point hawajibu hoja na kusema kama mi naongea majungu na uongo.Je ukweli upo wapi?bora wewe umeliona hili.
 
Hakuna gamba wala anayetumika na ccm hii kitu ndio itatuangusha chadema inabidi tukubali ukweli iki tujipange na si kupinga kila kitu na mtu anayesema ukweli unaitwa gamba.je ukweli ni upi kama mimi nadanganya?
Siku hizi majungu na unafiki vinaitwa ukweli?
 
Makam mwenyekiti anakipenda sana chama chake usimchafue labda ukiweka picha tutakuelewa kidogo
 
Makam mwenyekiti anakipenda sana chama chake usimchafue labda ukiweka picha tutakuelewa kidogo

Nimejaribu kuapload picha toka jana unajua mi natumia simu so inasumbua kuapload ila huo ndio ukweli huyo jamaa anaiua cdm hapa mpanda
 
Hata kama mtu amekaa uchi hakuna apendaye kuambiwa kuwa yu uchi!!! Achilia mbali mtu ajaribuye kusema kuwa "mfalme" yu uchi!!!
Soma nilichoandika uelewe a center of my point.. Kuleta hapa JF itasaidia vp ku-solve tatizo kama lipo..?
 
Hatimaye leo chadema mpanda wamefungua ofisi yao na kulipa kodi ya miezi 6 waliyokuwa wanadaiwa na hii ni baada ya kuandika humu jf jana,je tutafika kwa hali hii?je wapo wapi wale waliokuwa wananisema mi muongo,mnafiki na ninajenga chuki?
 
Aaah dogo kwani kujiumga jf siku za karibuni inamfanya mtu ashindwe kufikiri?majungu yapo wapi?naomba uniambie ukweli pia mbona ndani ya chama hamtaki ambiwa ukweli?kama kujiunga jf mapema ndio kigezo mbona umejiunga jf kitambo lakini akili yako ni kama ya gift binti yangu?jifunze kuheshimu watu huna ulichoandika wewe dada

Narudia tena, JF sio ofisi ya CHADEMA, malalamiko kama haya yaende kwenye chama. Huu ni utoto na ujinga, nadhani una akili kamasi zinakusumbua.
 
Narudia tena, JF sio ofisi ya CHADEMA, malalamiko kama haya yaende kwenye chama. Huu ni utoto na ujinga, nadhani una akili kamasi zinakusumbua.

Ofisi gani ambayo nitaenda kutolea maoni haya?kumbe ofisi wamenyang'anywa na imechukulia na dogo mmoja hivi muuza asali pia mzee hayo si majungu ni ukweli kabisa
 
Toa majungu humu kwani ofisi za chadema unazijua peleka huko mnafiki mkubwa wewe
 
Mzee mpaka nimeamua kuandika hapa sikuwa na jinsi kumbuka nipo mpanda pia hapa hakuna ofisi nitatoa maoni wapi?tulimwambia ukweli kwenye kikao akatupa kadi.je ungekuwa wewe ungefanya nini?
wewe kweli GAMBA..sababu iliyoelezwa ya mh arfi kutupa kadi ni kakijana flani kasiko kua na adabu kumtuhumu kwamba amenunuliwa na pinda..NA kwa kumbukumbu yangu mh.Arfi tulisha kaa nae kikao sisi vijana kabla ya kwenda bungeni..nakumbuka ili kuwa mwezi wa kwanza..Vijana wa chadema mpanda tulimaliza tofauti zetu na mh.arfi na kuahidi kukijenga chama upya.
 
mimi nipo mpanda....HUO NI UONGO MTUPU....Au na wewe ushanunuliwa na kevi mbogo coz vjana wengi wa mpanda walishanunuliwa na chama chenye pesa...
 
Narudia tena, JF sio ofisi ya CHADEMA, malalamiko kama haya yaende kwenye chama. Huu ni utoto na ujinga, nadhani una akili kamasi zinakusumbua.[/QU
ila ofisi ya ccm? Kwamba myalete hapa na kuyatilia majungu mtakavyo ila maovu ya cdm yawekwe kapuni kwakuwa yakijadiliwa hapa yanawaumbua.mnakera...
 
Hatimaye leo chadema mpanda wamefungua ofisi yao na kulipa kodi ya miezi 6 waliyokuwa wanadaiwa na hii ni baada ya kuandika humu jf jana,je tutafika kwa hali hii?je wapo wapi wale waliokuwa wananisema mi muongo,mnafiki na ninajenga chuki?
It was just a coincidence, who are you by the way?
 
Back
Top Bottom