i411
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 906
- 297
Haya jama wabongo apple app store ndo hiyo imetia nanga sasa wale wanaofanya uzinduzi wa mambo ya apps haraka haraka tuanze kutengeneza tuiweke Tanzania kwenye rada ya apple. Kitu kingine sasa tufanye mpango tumuandikie steve jobs na vigogo wa apple watufungulia duka kabisa hapa bongo. Tusiendelee kununua bizaa zao kwa bei ya kifisadi. Wakitufungulia duka hapa Tanzania litakuwa la kwanza east Africa na litakuwa kivutio pia. Sasa tuanze hii kampeni apple fungua duka Tanzania. Juzi tumeweza pata ukurasa wetu wenyewe kwenye forum ya kimataifa skyscrapercity lolote lawezekana. Na mwenye namba ya JK amwambie safari nyingine akienda US aongee na mzee steve job alete duka bongo. Sent from Iphone