Anza Leo, Acha Kuahirisha

Anza Leo, Acha Kuahirisha

BUSARA ZANGU

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2013
Posts
778
Reaction score
1,269
Wakuu Habari za Asubuhi

Kuna mambo mengi ambayo huwa yanakwama kwasababu ya kushindwa kuanza leo, watu wengi wamekuwa pale pale, miaka nenda rudi sababu ya kuahirisha kufanya mambo ambayo pengine yangewasogeza mbele kama Wangeanza kufanya jambo kwa wakati.

Watu wanaahirisha kuoa, watu wanaahirisha kusoma, watu wanaahirisha kujenga, watu wanaahirisha mambo mengi ambapo baadae wanakuja kujilaumu kwanini hawakufanya. Huu ni ugonjwa mkubwa.

Umewahi kuwaza ungeanza kutunza Tsh 100,000/= au 200,000/= au 300,000/= kila mwezi kwa miaka 5 iliyopita leo ungekuwa wapi? Vipi ukianza leo, baada ya miaka 5 ijayo utakuwa wapi kiuchumi. Achana na kiasi cha fedha, embu chukulia ungeanza leo kutunza/ku save angalau 15%/20% ya pato lako mwaka 2023 utakuwa na fedha kiasi gani? Anza Leo.

Anza Leo, panda miti leo kwenye shamba lako, ili miaka kadhaa upige hela. Najua ukiwaza mpaka mwaka 2025 ndio uvune miti yako utaona mbali sana. Lakini je, mwaka 2010 ungeambiwa panda miti yako ili uje uvune 2017,si ungeona ni mbali sana. Lakini huu ndio mwaka 2017. Kwa aliyekuwa na spirit kama hii mwaka 2010,leo anakula matunda.

Anza Leo kulima, Anza Leo kufuga, Anza Leo biashara, usiahirishe. Watu wengi wapo pale pale sababu ya kuahirisha.

Tarehe 30/11/2018 utajiuliza kwanini hukufanya leo, utajilaumu kwanini hukuanza leo.
 
Hesabu za darasa LA pili
Ukitunza shilingi 500 kila siku kwa Mwaka [HASHTAG]#500[/HASHTAG] mara siku 360 utakuwa na 180000* sasa kazi kwako
 
Hizo za kutunza mkuu si mpaka ziwepo? Au unazani tunavipato sawa?
Ila ngoja waje wenye ajira na mishahara minono
Mkuu za kutunza huwa zipo tu. Lakini pia za kutunza huwa hazipo tu. Inategemeana na utayari wako.

Unafahamu kuna watu wanapata milioni kwa mwezi, lakini mwisho wa mwezi anaishiwa na kubaki na madeni? Unafahamu kuna watu wanapata 150,000/= kwa mwezi lakini wanaweka akiba. Tofauti inayoweza kujitokeza kati ya mwenye pato kubwa na dogo katika kuweka akiba ni kiasi cha fedha, mmoja anaweza tunza kiasi kikubwa, mwingine ni kidogo.

Kuna mtu anaamini hawezi kuishi kwa laki mbili kwa mwezi kwakuwa leo anaishi kwa laki 5 kwa mwezi. Je akifilisika na aanze kuingiza laki na nusu kwa mwezi atakufa? La hasha.
 
Somo Zuri Shida Ipo Hv Unaweka Akiba Then Kibarua Kinagoma Kwa Cku Kadhaa Unachokifanya Unachukua Ile Akiba Uloweka Unaitikita ,then Una Anza Upya
 
Mada nzuri sana. Asilimia 95 au zaidi ya watu wanaona pesa hazitoshi. Akiwa na mshahara laki tano hautoshi. Akipandishiwa ukafika milioni hautoshi pia. Akifikisha milioni mbili bado ataona hautoshi. Kisa? Kila kipato kikiongezeka matumizi yanaongezeka. Mtu pekee atakayeweza kuweka akiba kama mtoa mada anavyosema ni mtu mwenye NIDHAMU YA PESA ya hali ya juu. Hao ni wachache sana. Nidhamu hiyo unaikuta kwa matajiri tu. Ndio maana watu wengi wa kawaida wanawaona matajiri kama watu bahili. Kumbe sio ubahili bali ni nidhamu ya pesa
 
Mada nzuri sana. Asilimia 95 au zaidi ya watu wanaona pesa hazitoshi. Akiwa na mshahara laki tano hautoshi. Akipandishiwa ukafika milioni hautoshi pia. Akifikisha milioni mbili bado ataona hautoshi. Kisa? Kila kipato kikiongezeka matumizi yanaongezeka. Mtu pekee atakayeweza kuweka akiba kama mtoa mada anavyosema ni mtu mwenye NIDHAMU YA PESA ya hali ya juu. Hao ni wachache sana. Nidhamu hiyo unaikuta kwa matajiri tu. Ndio maana watu wengi wa kawaida wanawaona matajiri kama watu bahili. Kumbe sio ubahili bali ni nidhamu ya pesa
Kwa mfano utasikia wanasema jamaa ana hela lakini nguo zake ni zile zile, au jamaa ana hela lakini mchoyo.

Wanasahau Warren Buffet tajiri wa pili duniani, anaishi kwenye nyumba ya vyumba vitano ambayo alikuwa anaishi humo tangu mwaka 1958
 
Kwa mfano utasikia wanasema jamaa ana hela lakini nguo zake ni zile zile, au jamaa ana hela lakini mchoyo.

Wanasahau Warren Buffet tajiri wa pili duniani, anaishi kwenye nyumba ya vyumba vitano ambayo alikuwa anaishi humo tangu mwaka 1958

Warren Buffet ni tajiri wa nne duniani na siyo wa pili. Nafasi ya pili anaishikilia Gates, ya tatu Ortega na ya kwanza yupo Bezos wa Amazon.
 
Wakuu Habari za Asubuhi

Kuna mambo mengi ambayo huwa yanakwama kwasababu ya kushindwa kuanza leo, watu wengi wamekuwa pale pale, miaka nenda rudi sababu ya kuahirisha kufanya mambo ambayo pengine yangewasogeza mbele kama Wangeanza kufanya jambo kwa wakati.

Watu wanaahirisha kuoa, watu wanaahirisha kusoma, watu wanaahirisha kujenga, watu wanaahirisha mambo mengi ambapo baadae wanakuja kujilaumu kwanini hawakufanya. Huu ni ugonjwa mkubwa.

Umewahi kuwaza ungeanza kutunza Tsh 100,000/= au 200,000/= au 300,000/= kila mwezi kwa miaka 5 iliyopita leo ungekuwa wapi? Vipi ukianza leo, baada ya miaka 5 ijayo utakuwa wapi kiuchumi. Achana na kiasi cha fedha, embu chukulia ungeanza leo kutunza/ku save angalau 15%/20% ya pato lako mwaka 2023 utakuwa na fedha kiasi gani? Anza Leo.

Anza Leo, panda miti leo kwenye shamba lako, ili miaka kadhaa upige hela. Najua ukiwaza mpaka mwaka 2025 ndio uvune miti yako utaona mbali sana. Lakini je, mwaka 2010 ungeambiwa panda miti yako ili uje uvune 2017,si ungeona ni mbali sana. Lakini huu ndio mwaka 2017. Kwa aliyekuwa na spirit kama hii mwaka 2010,leo anakula matunda.

Anza Leo kulima, Anza Leo kufuga, Anza Leo biashara, usiahirishe. Watu wengi wapo pale pale sababu ya kuahirisha.

Tarehe 30/11/2018 utajiuliza kwanini hukufanya leo, utajilaumu kwanini hukuanza leo.
100 mkuu
 
Warren Buffet ni tajiri wa nne duniani na siyo wa pili. Nafasi ya pili anaishikilia Gates, ya tatu Ortega na ya kwanza yupo Bezos wa Amazon.
Sawa mkuu. Orodha imekuwa ikibadilika mara kwa mara. Nina imani hiyo haijapoteza msingi wa hoja yangu.
 
Somo Zuri Shida Ipo Hv Unaweka Akiba Then Kibarua Kinagoma Kwa Cku Kadhaa Unachokifanya Unachukua Ile Akiba Uloweka Unaitikita ,then Una Anza Upya
Mkuu ni kweli hizo changamoto huwa zinajitokeza, cha msingi ni kuwa na malengo.

Nakuhakikishia wewe hutakuwa mtu wa kwanza kutoka chini na kutusua kimaisha, kama ukiwa na malengo.
 
Dah! umenikosha mara zote nimekuwa nikiwaza hilo lkn nimekuwa mtumwa mno wa mikopo hadi naishi kwa shida! maskini mm! labda ntaanza mwakani.
wadau fikiri suppose napata take home sh. let's say 900,0000 (i.e kwa wale wenye mapato hayo and above)
nikaamua kusave 500,000 kila mwezi(NB; kwa yule anayeweza)
kwa mwaka utakuwa na 6,000, 000.
hatupaswi kusema kuwa hatuwezi kuweka, shida ni discipline ya kujinyima na kujikubali kuishi kwa salio dogo. but if you can, unaweza kufanya wonders!!! karibuni wadau. Haya ni mawazo yangu waweza kuwa na mawazo yako pia
 
Back
Top Bottom