Wewe tulia ukae kwa Amani kwani ukithubutu kugusa masilahi ya Maliyamungu Bashite ujue yatakukuta kama ya Lisu kule Dodoma alipogusa masilahi ya 10% ununuzi wa ndege na Siri za kuikomboa ndege kwa Siri kimya kimya apate kupiga cha kingine, tulia usiguse Dili za Naibu Rais Maliyamungu idd Amin Bashite utaishi kwa Amani na Heri Kisanduku makapero hatakaa apajue kwako.Mkuu Mwanahabari huru, kumbe upo?, kwa vile Ngurumo mwenyewe ameishaingia humu mazima in person akiwa ni verified, nakushauri sasa pumzika, acha mwenyewe aje, tubanane nae humu humu.
Ni kweli kuna kitu nimeona hapo sio tuu ni hatari kweli bali kinatisha, sisi ambao hatuna mahali pa kukimbilia, kuna wakati, unapaswa kufunga tuu mdomo na kushangaa, kama mimi ninavyoshangaa kwenye bandiko hili na haswa the authenticity of the story, ikizingatiwa imeripotiwa na mhariri wa kuaminika, ila pia inaweza kabisa kuwa ni concoction kwa sababu hata waandishi wakubwa na wahariri kama kina Salva, na Mtanzania, waliwahi ku concoct na kushuka na concoction kumhusu Dr. Salim Ahmed Salim.
This is something serious, something big, something very dangerous, mpaka sasa mimi bado siamini!.
Tusubiri.
P
Maliyamungu idd Amin Bashite ni hatari kuliko marehemu Babu yake colonel Maliyamungu wa enzi za marehemu idd Amin dada kule uganda.Hii habari ni kweli kabisa,Maliyamungu ni tishio
Mtakimbiana mwaka huu, mkuu kumbe Mtulia yuko hoi?? Ila dua aliyoomba Mwalimu Salum pale viwanja vya buibui mwananyamala kinondoni, aliapa na kujiapiza atakaeshiriki kwa namna yoyote kudhulm nafsi, uhai, damu na ushindi wa mtu atateketea yeye na ukoo wake. Mtulia tayari hatujui ukoo wake, vipi wsle polisi walioua Aquilina? Vipi Makonda na timu yake?Mwanahabari Huru naona sasa umebobea kuleta taarifa za uchochezi hapa JF na Moderator wamekuacha tu!! Sina uhakika kama unaweza kutudhibitishia taarifa hii kama ni ya kweli kwa kuwa wewe ndiyo unaisambaza!!
Kufuatana na sheria za kikimbizi mkimbizi haruhusiwi kutumia nchi alipo kimbilia kuanza kuichokoza nchi yake alipotokea. - Ansbert jiongeze -Hakuna siri tena. Leo tarehe 30:03:2018, saa tisa kamili (9:00) alasiri, saa ambayo Bwana Yesu Kristo alikata roho msalabani, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, katika muda ule ule, Paul Makonda, alikuwa anafungua kikao maalumu cha kupanga mambo maovu dhidi ya viongozi waandamizi wa Chadema na wakosoaji wengine wa serikali. Kikao hicho, ambacho alikiita kikao cha “ulinzi na usalama,” katika ukumbi wa polisi Kurasini, kiliahirishwa saa moja kamili (1:00) usiku.
Katika kikao hicho, yalijadiliwa mambo mengi mazito.
Nimechagua machache tu yafuatayo, ndiyo nitaweka bayana, ili kuonyesha dunia jinsi kiburi, jeuri, sifa na madaraka ya watu wawili (JPM na Makonda) vinavyohatarisha usalama wa taifa letu. Mengine yanafanyiwa kazi na vyombo muhimu.
1. Mbali na Freeman Mbowe na viongozi wenzake walio gerezani Segerea, wengine waliojadiliwa na kikao hiki, ambao watakamatwa muda wowote kuanzia sasa ni wabunge: Godbless Lema (Arusha), Halima Mdee (Kawe), John Heche (Tarime Vijijini), Esther Bulaya (Bunda), Joseph Selasini (Rombo), na kiongozi wa Jumuiya za Kiislamu, Ustadhi Rajab Katimba. Eti hawa ni "majasusi wa Chadema!"
2. Miongoni mwa waliohudhuria kikao hicho ni Bw. Cyprian Musiba, ambaye amekuwa anakutana na waandishi wa habari na kutoa matamko ya shari na tuhuma kali dhidi ya watu wanaokosoa serikali. Alikuwa kikaoni - kikao cha “ulinzi na usalama” mkoa wa Dar es Salaam. Katika moja ya hoja zake, alisema Ansbert Ngurumo anachafua serikali akiwa huko Ulaya; na kwamba ingekuwa vema serikali iweke utaratibu wa kumfuatilia huko aliko na kumdhibiti. Baadhi ya wajumbe walisema hakuna haja, bali serikali ibane hawa hawa waliopo nchini, hasa Heche na Lema. Hasira dhidi ya Lema zilitokana zaidi na kauli yake kutaja Dk. Modestus Kipilimba kwamba anashinikizwa na kushirikishwa katika kupanga mateso dhidi ya wapinzani. Mbali na kusaka fursa ya kumtesa, wanatengeneza “mabomu” dhidi ya mbunge huyo wa Arusha.
3. Wamekerwa na suala la ugonjwa wa Abdallah Mtulia (mbunge wa Kinondoni) kujulikana, wakadai kwamba ugonjwa wake umesababishwa na Chadema. Mtulia ana hali mbaya hospitalini. Makonda na Musiba wamejiapiza kuwa watapambana na Chadema kwa mbinu zote kwa kutumia dola na "uchawi."
4. Kesi ya Mbowe inawapasua kichwa, inawatia hofu (kwa sababu ni ya kubumba); hata mawakili wa serikali wamesema wanalinda hadhi ya taaluma yao, hawataki kuchafuka au kuchafua taaluma zao kwa kesi za kubumba za polisi.
5. Serikali inakerwa mno na taarifa za vikao vyao vya siri kuvuja, na jambo hili linawafanya wachelewe kutekeleza uovu wao wanaopanga dhidi ya Mbowe. Wamesema zamu hii watakuwa makini zaidi.
Yapo mengi, lakini haya ndiyo nimeona vema niyaanike hapa, ili Watanzania na dunia nzima ijue kinachoendelea nyuma ya pazia, wajue aina ya “viongozi” walionao, na wajue nani anahatarisha usalama wa nchi. Hivi ndivyo Bashite na kikosi chake walivyoadhimisha Ijumaa Kuu – kwa kumkejeli Mungu!
MASWALI MAGUMU:
a) Bado Watanzania mnajiuliza nani anamtuma Musiba kufanya press conferences na kutoa matamko ya kushambulia watu kwa tuhuma za ajabu ajabu?
b) Bado mnataka kujua mamlaka inayomlinda Musiba?
c) Idara ya Usalama wa Taifa haijui haya au imenyosha mikono, inafuata maagizo, na imeamua kuacha hatima ya usalama wa nchi hii mikononi mwa watu wawili?
d) Kuna mtu anadhani Makonda anafanya haya kwa hiari yake tu, bila idhini na baraka za Rais Magufuli anayesema maneno ya ajabu dhidi ya wapinzani na wakosoaji wake, hadharani bila aibu, kwamba, “sijaribiwi…. nitawavunja miguu?”
e) Kwa mikakati hii, kwa kuhatarisha badala ya kulinda uhai na usalama wetu, rais anadhani nchi iko salama, na yeye mwenyewe yuko salama?
f) Wakati uovu huu unapangwa rasmi, Rais Magufuli alikuwa kanisani kwenye ibada ya Ijumaa Kuu, “anasali.” Je, naye alibusu msalaba? Kama ndiyo, busu lake lina tofauti gani na busu la Yuda kwa Bwana Yesu – busu la usaliti kwa Watanzania alioapa kuwalinda?
g) Mateso na vifo vya wapinzani na wakosoaji wake ndiyo zawadi ya Pasaka ambayo rais anaandalia Watanzania mwaka huu 2018?
h) Kama utawala wa Kaisari uliangukwa kwa sababu ya kiburi, jeuri na ulevi wa madaraka, utawala wa Magufuli utanusurika vipi ukiwa na sifa zile zile?
Mengine nabaki nayo. Tuendelee kutafakari haya.
Ansbert Ngurumo
MHARIRI BILA MIPAKA (MBM)
Unaamini kuwa unaweza, jaribu.Acha vitisho we bua, unajifanya anajiweza, tena wewe kwako tunapajua endelea kutuudhi tutaanza na wewe.
Mayala, hata swali ulilouliza rais kuhusu kuvunja katiba ulikuwa kazini? Hata kama raisni msukuma ndo mmeamua kutuuua? Kutuonea? Ni dhambi ipi kuwa upinzani? Halafu huu urais wa wasukuma hautaisha? Mmeamua kuvuruga nchi na kutesa watanzania? Haya ni wakati wenu.Duh!.
Ngurumo, Ngurumo, Ngurumo...
Hii kali...
Kwanza kwaheri
kisha karibu
Hii ya kwako Ngurumo kali!, yaani wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Dar es Salaam wanaripoti kwako Ngurumo!...
bora umekimbia! maana...
Hata hivyo, kwenye tasnia ya media, hakuna kitu kama MBM, kilichopo ni waandishi wasio ma mipaka, Journalists San Frontiers
P
Umewafuatilia Edward Snowden na Julian Assange wanadili vipi na nchi zao wakiwa huko ukimbizini?Kufuatana na sheria za kikimbizi mkimbizi haruhusiwi kutumia nchi alipo kimbilia kuanza kuichokoza nchi yake alipotokea. - Ansbert jiongeze -
mange kimambi huwa anazipata vipi? kikubwa hapa kuna wau wengi tu walioko kwenye system hawapendi na hawafurahii yanayoendelea ila tu hawana pa kuongelea. So kweu sisi watu kama kimangi na hata hyu Ngurumo ni muhimu sana kwa jamii yetu kwa sasa.Inamaana amezipata hizi taarifa akiwa huko ugaibuni? Kama ni hivyo sasa nihatari,nani amemfikishia taarifa za kikao hicho? Kwa kifupi kuna uvujaji mwingi sana wa taarifa kama ni hivyo,haiwezekani mtu yuko ugaibuni akaqeza kudukua siri za vikao hapa kwetuu
Kweli mkuu.Comrade Mayalla
Mi siamini kama Nchi yetu imefika huko...
Haya yakiachwa yaendelee, kuna siku Viongozi na Wananchi tutavuna mabua
Kama Marekani alidai uchaguzi wake umedukuliwa na Mrusi sembuse nchi masikini na hisiyo na teknolojia kama ya kwetu!!!?Inamaana amezipata hizi taarifa akiwa huko ugaibuni? Kama ni hivyo sasa nihatari,nani amemfikishia taarifa za kikao hicho? Kwa kifupi kuna uvujaji mwingi sana wa taarifa kama ni hivyo,haiwezekani mtu yuko ugaibuni akaqeza kudukua siri za vikao hapa kwetuu
Wewe acha ufala utumbo mnaongea nyie vilaza wa Le mutuz na Boss wenu Maliyamungu Bashite, akiongea Msiba ujinga mnaomtuma mbona hamuombi ushahidi wowote? Ya msiba hatahitaji ushahidi lakini ya chadema kuwajibu CCM mnataka ushahidi? Tambua kuwa watanzania si wajinga kiasi mnachofikiria wanajua kutafakari ni yupi kati ya CCM na chadema anayewahadaa watanzania.Duh. Huu upotoshaji wa CHADEMA, wanaongea lolote ili kujihami na maovu yao wanayoyafanya kila siku.
Yaani wao ni kubashiri lolote jf ili kulinda maovu yao. Mmeongea utumbo mwingi wa vikao bila ushahidi wowote.
Naibu Rais ndugu Maliyamungu Bashite na kikundi chake saa 24 wanashinda na waganga wa kienyeji wanaishi kwa wasiwasi hawajiaminiMtakimbiana mwaka huu, mkuu kumbe Mtulia yuko hoi?? Ila dua aliyoomba Mwalimu Salum pale viwanja vya buibui mwananyamala kinondoni, aliapa na kujiapiza atakaeshiriki kwa namna yoyote kudhulm nafsi, uhai, damu na ushindi wa mtu atateketea yeye na ukoo wake. Mtulia tayari hatujui ukoo wake, vipi wsle polisi walioua Aquilina? Vipi Makonda na timu yake?
Aaah wapi......this is just a guessing
Kuna baadhi ya mambo ni ya kufikirika unaweza kuyaweka kwenye maandishi yakaonekana ni ukweli kutokana na wakati tuliopo
Mfano
kama ambavyo wengi wetu tunajaribu kumhusisha MBOWE na UPOTEVU wa SAANANE...
Au kuwahusisha CHADEMA NA BAADHI YA MAUAJI
Wakati uovu huu unapangwa rasmi, Rais Magufuli alikuwa kanisani kwenye ibada ya Ijumaa Kuu, “anasali.” Je, naye alibusu msalaba? Kama ndiyo, busu lake lina tofauti gani na busu la Yuda kwa Bwana Yesu – busu la usaliti kwa Watanzania alioapa kuwalinda?
WHAT IF IKITHIBITIKA HUU MUDA PIA MAKONDA ALIKUWA KANISANI?
Me naomba tufatilie ni wapi jana MAKONDA ALISALI...hili tuthibutishe hiki