BIN BOR
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 1,013
- 407
Mama mmoja alikuwa anagombana na mumewe kabla ya kulala.
"Mke wangu vipi, mbona mkali"
"Nimekuta hiki kikaratasi kwenye mfuko wa kaptula yako kimeandikwa Annie Louis. Nataka uniambie ni nani huyu Annie Louis?"
"Aaagh mke wangu kwa wivu tu. Umesahau leo pale leader's club kulikuwa na mbio za mbuzi? Sasa mbuzi niliyetabiri angeshinda ndio jina lake Annie Louis"
"Sasa alishinda?"
"Bahati mbaya hakushinda" mume akamridhisha mkewe, wakalala.
Saa tisa usiku wakati jamaa anakoroma mke akamtikisa kwa nguvu hadi jamaa akadondoka chini. Kwa hasira jamaa akauliza.
"Mke wangu mbona unaniamsha kwa fujo, kuna nini?"
"Chukua simu yako uone. Mbuzi amekutumia meseji, tena kwa kizungu"
"Mke wangu vipi, mbona mkali"
"Nimekuta hiki kikaratasi kwenye mfuko wa kaptula yako kimeandikwa Annie Louis. Nataka uniambie ni nani huyu Annie Louis?"
"Aaagh mke wangu kwa wivu tu. Umesahau leo pale leader's club kulikuwa na mbio za mbuzi? Sasa mbuzi niliyetabiri angeshinda ndio jina lake Annie Louis"
"Sasa alishinda?"
"Bahati mbaya hakushinda" mume akamridhisha mkewe, wakalala.
Saa tisa usiku wakati jamaa anakoroma mke akamtikisa kwa nguvu hadi jamaa akadondoka chini. Kwa hasira jamaa akauliza.
"Mke wangu mbona unaniamsha kwa fujo, kuna nini?"
"Chukua simu yako uone. Mbuzi amekutumia meseji, tena kwa kizungu"