Unatakiwa kuwa na uwezo wa kusoma na kuelewa kilichoandikwa;siyo kutembeza uswahili wala kutanguliza hisia kali. Nimekushauri usome mkakati wa shule. Tatizo lako na watu waaina yako mnajadili pesa badala ya kufahamu na kujadili masuala makuuyanayobeba mjadala (debate).
Kiongozi wa serikali hatakiwi kupokea kiasi kikubwa cha pesa kwa sababu yoyote ile, iwe msaada au zawadi,KUNA VIWANGO vya mwisho, kama huvijui kasome tena waraka wa tume ya maadili.
Huwezi kupokea $1M kwa sababu yoyote ile ukaitetea. $1M ni faida ambayo mfanyabiashara anaipata kwa kuwa na mapato yasiyopungua $5M. Na ukichangia corporate tax, ya hiyo profit, basi ni zaidi ya hapo.Ni ngumu sana mfanyabiashara anayefanya biashara kihalali kugawa pesa hiyo bila sababu ya msingi.Tena kwa makumi ya watu,kwa kipindi cha siku kadhaa.Sheria za kodi haziruhusu kiwango cha aina hii kulipwa bila ushahidi wa invoice, au mkataba unaoonesha sababu ya kulipwa kiwango hicho cha pesa. Kwa kuwa mwenye benki(Kilaini) alishalainishwa basi ma-teller wanafanya tu transaction kama machizi, BOT nao kwa kuwa wameshapokea maagizo kutoka Juu wanaruhusu tu transaction fraudulent kupita bila sababu ya msingi.Only in TZ mambo ya kipuuzi kama haya yanafanyika.
Kama hujui mkakati wa maendeleo wa asasi husika usijiingizekwenye mjadala kuhusu maendeleo ya asasi hiyo.
Kupata wazo na kubadilisha wazo kuwa bankable project, ku-developplan, kuandaa design ya kutekeleza mpango, kuanzisha asasi yenye malego namajukumu ya kutekeleza shughuli wakilishi ya wazo la awali la maendeleo Fulani (sema shule) siyo jambo la mzaa wala eneo la kila mtu kuweza kufanya, achiliambali kufahamu. Na hili ndilo tatizo la nchi maskini na fursa kwa asasi zakimataifa kama benki ya Dunia, IMF, Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya nakadhalika, kuingilia na kuchagiza mipango ya maendeleo ya nchi maskini, ikiwani pamoja na Tanzania. Hali hii inaitwa poor public policy understanding,design, execution/implementation and analysis of underdeveloped countries.
Unachanganya mambo hapa, wizi/Ufisadi wa Tibaijuka na kazi alizowahi fanya ni mutually exclusive, hazina uhusiano. Mahakama haitazami uliwahi kuwa mtakatifu huko nyuma, zina-angaliwa facts za kosa ulilofanya. Facts zinaonesha tuko na waziri ambaye yuko very well compromised.
Kama asasi (shule) husika huzijui usijiingize kwenye mjadala kwa hoja za kufikirika bila rejea ya nadharia au taarifa za tafiti.
Aliyeiingiza asasi ni Tibaijuka mwenyewe kwa kuweka utetezi wa kishamba kuwa amepokea fedha kwa ajili ya shule, yani anatufanya watanzania ni mabwege sana, muda si mrefu kila mwizi ataanda kutoa sababu kama hizo kutetea wizi wake,hata zile bilioni 73 za standbic tutaambiwa zilienda kujenga makanisa. Kama hiyo ni asasi kama anavyotanabahisha, basi pesa zilitakiwa zipelekwe kwenye account ya shule na si vinginevyo.
Kwanza nataka ufahamu kuwa binafsi sina uhusiano wowote nashule za Tibaijuka zaidi ya watoto wangu kusoma pale na ninalipa karo kiasichote cha Tzs. 4.5m/- kwa kila mtoto. Hivyo I am an impartial, civilised andresponsible citizen nisiyependa uswahili na ubabaishaji katika maendeleo kuanziangazi ya mtu mmoja, kaya na asasi rasmi (kitaifa, kimataifa, serikali, isiyo yaserikali, biashara au huduma).
Watoto wako wanasoma wapi ni irrelevant, unalipa ada kiasi gani hapo shuleni hakusaidii kwenye kujenga hoja ya kuwa wewe ni civilized and responsible. Hata hao wezi kina chenge wamesomesha watoto wao Redbricks universities, lakini hakuna asiyejua Chenge ni sawa na shetani aliyekosa mbuyu.
Kukweiba mabilioni kuyapeleka kwenye miradi binafsi, sio maendeleo ni uhayawani na ufisadi, ndio maana Africa inaendelea kubaki nyuma, kwa kuwa viongozi ni wabinafsi. Fedha za Escrow, za umeme, za watanzania, hawa washenzi wachache wanagawana kwenye mifuko ya saflet, yani ni waroho hadi wanapindukia. kesho ukiwakuta kwenye mashangingi na suti zao unataka tuwaite civilised?kwa kuwa wamevaa suti?sidhani.
Ukiwa mwananchi unayewajibika unajukumu la kushinikizaserikali ya CCM iboreshe shule za umma (walimu, vifaa, miundombinu, usimamizi) ili watoto wako, na pengine waWatanzania wengine wa aina yako, waweze kunufaika na elimu bora badala yakuchukia wadau wa harakati binafsi za kuwekeza kwenye elimu.
Subjectively viwango vya elimu vimechangiwa kudorora na hawa watendaji wa serikali wenye kumiliki shule binafsi, huu uwekezaji mshenzi kwenye elimu, si kila mtanzania anaufurahia. Hivi unategemea Elimu ibrosheke vipi wakati ili kuipata elimu bora bei yake inaanzia 4.5M?wakati wastani wa pato la mtanzania kwa mwaka ni chini ya $1000?hivi ni vichekesho.
Usibeze watu wasio na uwezo wa kupeleka watoto kwenye private schools,kwani haziwezi kuboresheka kama mawaziri kama tibaijuka wako mstari wa mbele kukwapua kila fedha iliyoko BOT na Hazina kuzipeleka kwenye mambo yao binafsi.
Unaweza kumwajibisha Tibaijuka kwa namna yoyote unayowezalakini siyo ku-launch unduly accusations and uninformed arguments.
Tibaijuka ameshawajibishwa, hivyo sentensi yako haina mashiko. Accusations sio uninformed, kwani timing na coincidence yake ilisababisha parliamentary probe na yeye Tibaijuka amekiri kuandika barua ya kujieleza kwa kamati ya PAC.
Acha kutetea wizi wa mchana kama huu, hakuna hata mtu mmoja aliyekana kupokea fedha za Rugemarila.sababu ziko wazi. it was a payday, all was good UNTIL shit hit the fans