Anguko la Kasri ya Mbinguni ya Wachina April 2018

Anguko la Kasri ya Mbinguni ya Wachina April 2018

Cesar Saint

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2016
Posts
423
Reaction score
727
Habari zenu wanaJamvi
Ni wendelezo wa habari za anga za juu (Space) Tiangong-1 neno lenye maana ya "Heavenly Palace" kwa tafsiri isiyo rasmi yaani kasri ya mbinguni ina uzito unaokadiriwa wa 8.5 metric tons na urefu wa futi 34 na upana wa futi 11 (10.4m kwa 3.4m)
Kituo hiki cha anga kinajumuisha kitengi ya mafunzo na majaribio ambapo wana-anga wanaweza kufanyia shughuli zao na sehemu ya pili yenye matenki propellant na injini za roketi.

IMG_4225.JPG


Tiangong-1 ni kituo cha anga kilichopo kwenye mfumo wa single-module kinachosimamiwa na China National Space Administration kilichorushwa mwishoni mwa mwaka 2011 kikiwa kimehudumia na wana-anga wawili wa kichina (taikonauts) mwaka 2012 na 2013. Kutokana na usiri mkubwa wa CNSA taarifa juu ya mission na habari kuhusu Tiangong-1 zimekuwa hazipatikani kwa urahisi.

IMG_4226.JPG

IMG_4227.JPG
IMG_4228.JPG


Tiangong-1 iliwekwa kwenye mzunguko wa karibu na dunia takribani maili 217(350km) na katika mwinuko wa chini kidogo ukilinganisha International space station . Mashine zake zinapewa nguvu na “arrays” mbili za jua na inauwezo wa kutunza na kuhudumia mwana-anga watatu .

Msingi mkubwa wa kujenga module hii ilikuwa ni kusaidia China katika kuendeleza shughuli hizi za uchunguzi wa anga ya juu kuwa endelevu kwa kuweza kufanya “space docking” na kuweza kutengeneza kituo kikubwa kitakachoweza kupokea spacecrafts nyingi zaidi na kwenda Mars na sehemu nyingine za mfumo wa jua .

IMG_4213.JPG


Mara baada ya kufanikiwa kwa mpango huu China walifanya mission mbalimbali kwa kutumia Shenzou 8,9,10 hii ilitokana na hapo mwanzo kwa Tiangong-1 ilitazamiwa kudumu kwa kipindi cha miaka miwili na hivyo ndio ikapelekea kurushwa kwa mfululizo wa Shenzhou 8 hii ilikuwa haijabeba mtu October 2011, Shenzhou 9 mwaka 2012 ikiwa na watu watatu ambayo iliweka historia ya kupeleka mwanamke wa kwanza wa kichina kwenye Space na June 2013 wakarusha Shenzhou 10 iliyobeba watu taikonauts watatu.

IMG_4218.JPG


Baada ya kupoteza uongozi wa Tiangong-1 hatimaye September 2016 China wakarusha Tiangong -2 na ikafanikiwa kupokea mwendelezo wa Shenzhou 11 na ilipofika November 2016 likafanyika jaribio la “docking and refueling” ya Tianzhou-1 na ilifanya hivyo tena April,June na September 2017 na tofauti na matarajio ya kufanya hivyo kwa siku mbili docking hii ilidumu kwa masaa 6.5

IMG_4220.JPG


Kitendo cha kuharibika kwa mzunguko wa Tiangong-1 na kupoteza kwa mawasiliano ya usimamizi wa Tiangong-1 mwaka 2016 kunaweka wazi uwezekano mkubwa wa vipande vya spacecraft hii kuingia katika anga la dunia mnamo March 30 mpaka April 2018

IMG_4217.JPG

IMG_4219.JPG



Hakuna wana-anga waliotembelea Tiangong-1 tokea mwaka 2013 lakini taarifa zinazokusanywa kupitia kituo hiki kimewezesha uchina kugundua uwepo wa madini na kupata taarifa za hali ya hewa ambapo inasadikika mwaka 2013 wakati wa mafuriko ya Yuyao na mnamo March 2016 zoezi la ukusanyaji taarifa likasimamishwa bila taarifa zaidi.

IMG_4222.JPG

IMG_4223.JPG


Bado haijawekwa wazi hasa kama China imeweza kufanya mahesabu ya kuingia kwa chombo hiki katika anga la dunia kama ilivyokuwa kwa MIR au kitakuja kama Nyati aliyejeruhiwa kama ilivyokuwa kwa Skylab mwaka 1978 na kudondokea maeneo yenye watu huko Australia
IMG_4221.JPG


IMG_4212.JPG


Maeneo ambayo inaweza kuangukia ni

IMG_4224.JPG



Asante
 
Kuna 85% ya kusababisha madhara kwa RAIA
Lakini kama chombo hiki kingewekwa ktk mzunguko wa nguvu ya uvutani hata kama kingepoteza nguvu bado kingeendelea kuvutwa na nguvu ya uvutani sijui kwa nini China wamefanya kitu cha hatari namna hii au labda huenda uwezo wao wa teknolojia ni mdogo walishindwa kukiweka sehemu ambayo kitatumia nguvu ya uvutani ya jua na Dunia
 
Hiki chombo watu waliokuwemo wamepoteza maisha au kuna njia ya kuwaokoa?
 
Kuna 85% ya kusababisha madhara kwa RAIA
Lakini kama chombo hiki kingewekwa ktk mzunguko wa nguvu ya uvutani hata kama kingepoteza nguvu bado kingeendelea kuvutwa na nguvu ya uvutani sijui kwa nini China wamefanya kitu cha hatari namna hii au labda huenda uwezo wao wa teknolojia ni mdogo walishindwa kukiweka sehemu ambayo kitatumia nguvu ya uvutani ya jua na Dunia

Walikuwa na mipango ya kutaka kuendelea kukitumia zaidi kama kituo cha safari za Space
 
Halafu ni chepesi sana kwa aajili ya kuhimili uelekeo mchongoko na upepo kinzani na urukaji uwezo himili, ole wake kikutane na radi kwenye anga lile breki ya kwanza Chato
 
Mmmmh kingeangukia pale kwa yule kaka asiependa tarehe 26............mweee
 
Back
Top Bottom