Anguko La Gaddafi; Tafsiri Yangu

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

HAKUNA chenye mwanzo kisicho na mwisho. Na utawala wa Gaddafi umefikia ukomo. Libya haiwezi tena kurudi kama ilivyokuwa enzi za Gaddafi.


Gaddafi aliitawala Libya kwa ‘ mkono wa chuma’ kwa zaidi ya miaka 40. Aliitawala Libya kidikteta. Pamoja na utajiri mkubwa wa mafuta wa nchi hiyo, utawala wa Gaddafi uliminya uhuru wa fikra kwa watu wake. Kamwe Gaddafi hakuvumilia fikra za kipinzani.


Mwanzoni kabisa mwa harakati za kumwondoa Gaddafi madarakani , kuna kijana aliyepata kutamka haya; “ Tunachotaka ni kuishi maisha ya kawaida. Kuwa na uhuru wa mawazo kama vijana wengine duniani”. Alitamka kijana yule wa KiLibya kwa mwanahabari wa Kimagharibi.


Na hakika hicho ndicho kikubwa kilichokosekana chini ya utawala wa Gaddafi. Na siku zote, mwanadamu hata umpe nini, lakini ukimnyima uhuru wa kufikiri na kuchagua, basi, atajisikia mtumwa. Hatofurahi.


Na kwa Gaddafi, si tu aliitawala Libya kwa muda mrefu, lakini bado alikuwa na ndoto, kuwa akitoka madarakani , basi, familia yake iendelee kutawala. Na umma ukimchoka mtawala au chama cha siasa, basi, utaishi kwa matumaini, kuwa siku moja itafika, kuwa umma utaondokana nae, au kuondokana nacho, kama ni chama cha siasa. Ndio maana ya furaha kubwa ya wenye kutimiza ndoto zao za kujikomboa.


Ndio, kiongozi wa nchi haui watu wake, Moummar Gaddafi wa Libya alifanya hivyo. Aliwaua watu wake, tena mchana wa jua kali, na bado alisimama hadharani, akidai kuwa ni kiongozi wa WaLibya. Gaddafi hakuwa na aibu.


Hatukatai, kuwa Gaddafi alifanya mazuri kwa WaLibya, LAKINI, kosa kubwa kabisa alilofanya Gaddafi kwa WaLibya ni KUWAKANDAMIZA watu wake. Ndio, kuwanyima UHURU. Gaddafi aliwageuza WaLibya kama ng’ombe kwenye zizi. Waliotoa sauti kumpinga aliwakamata na ‘kuwachinja’, kimyakimya. Gadaffi aliifanya Libya kuwa ni mali ya Gaddafi na familia yake.




Ndugu zangu,



Gaddafi alipata kusimama hadharani na kuwaambia WaLibya waendelee kuimba na kucheza! Akatamka; “ WaLibya wote wananipenda!” Hakika, Gaddafi alikuwa amepoteza mwelekeo na mguso wa hali halisi. Alipitisha viwango vyote vya ulevi wa madaraka. Wakati mwingine Gaddafi alionekana kama mwehu fulani aliyeshika bunduki na kupita mitaani. Na kwa kuhofia maisha yao, kuna vijana wengi wasomi wa Libya walilazimika kuikimbia nchi yao wanayoipenda. Walikwenda kuishi uhamishoni.


Tunajifunza nini?

Kwamba Afrika bado ina viongozi wengi, ambao, hata hii leo, wameingiwa hofu kwa kile kilichomtokea mwenzao Gaddafi. Hofu hiyo ina tafsiri nyingi; moja kuu ni ukweli, kuwa kuna viongozi Afrika wanaofanana fanana na Gaddafi. Kwamba nao hawapendi na hawaamini katika demokrasia na uhuru wa watu kutoa mawazo yao, hata yenye kushutumu Serikali.


Hawapendi uwepo wa vyama vingi na dhana ya kugawana madaraka. Hawapendi uwepo wa chaguzi huru na za haki. Hawapendi Katiba ambazo, mbali ya mambo mengine, zinampunguzia madaraka Rais. Kwao, kumpunguzia Rais madaraka ni sawa na kumpunguzia nguvu mtawala. Kwao ni jambo lisilowezekana.

Na Afrika bado ina watawala ambao watafanya kila hila kuhakikisha chaguzi za kisiasa haziendeshwi na tume huru za uchaguzi, bali, zitaendeshwa kutoka Ikulu zao. Na watawala hawa wa Afrika, kama kuna wenye kuandamana mitaani kuwapinga, basi, nao kama alivyofanya Gaddafi, hawatasita kutumia nguvu za kijeshi kuzima maandamano ya wananchi, ikibidi kuwaua wananchi wao. Ndio, Watatafuta visingizio vya kuwatwanga risasi watu wao ili kuwatishia wengine.


Na hakika, kinachotokea Afrika ni hiki; kwanza, mtawala atawaita waandamanaji ‘ kuku’ na majina mengineyo. Kisha ataamrisha vikosi vyake vitumie risasi za moto kuwadhibiti ‘ kuku’ waandamanaji. Si tunajua, kuwa Afrika kuku hachimbiwi kaburi.


Viongozi Afrika watambue sasa, kuwa Afrika kuna kimbunga kimelipuka. Ni kimbunga kinachosambaa. Kimeanzia Tunisia, kikaenda Misri na kimetua Libya. Kinasambaa. Ni kimbunga cha mabadiliko. Waafrika wengi wanaokandamizwa na watawala au vyama tawala katika nchi zao, leo wana kiu kubwa ya kujikomboa.


Na kiongozi mzuri hujitambua na kutambua wakati unaomzunguka. Huwa na uwezo wa kusoma alama za nyakati. Kiongozi makini, mwenye busara na mapenzi ya dhati kwa nchi yake hatosubirii watu wake wafikie ukomo wa uvumilivu ili afanye mabadiliko hitajika na yenye kukidhi matakwa ya wakati husika.


Nimepata kuandika, kuwa katika nchi, mabadiliko ya amani yanawezekana, lakini, kwa anayejaribu kuyazuia, atambue, kuwa mabadiliko yenye vurugu hayaepukiki.

Waafrika wameamka usingizini. Wameshatambua, kuwa hakuna risasi au kombora la mtawala litakaloweza kushinda nguvu ya umma uliodhamiria kuleta mabadiliko. Yametokea Tunisia, Misri, Libya. Yanaweza kutokea popote pale Afrika.
Busara ni kuenenda na wakati uliobadilika. Nahitimisha.
Maggid,
Dar es Salaam.
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo


( Makala haya yamechapwa kwenye gazeti la Mwananci, leo Jumapili)
 
Viongozi wa afrika kusini mwa jangwa la sahara wanaona kinachoendelea kaskazini mwa afrika hakina uhusiano na wala hakitaathiri mwenendo wa kiharakati na kisiasa ndani ya nchi zao. Hakuna la kujifunza wanaloliona. Kwa ufupi wanajifariji "nchi yangu ni tofauti sana, watu wangu wananipenda" kama Gadafi alivokua akiwaza.
 
Ndugu zangu,

HAKUNA chenye mwanzo kisicho na mwisho. Na utawala wa Gaddafi umefikia ukomo. Libya haiwezi tena kurudi kama ilivyokuwa enzi za Gaddafi.


Gaddafi aliitawala Libya kwa  mkono wa chuma kwa zaidi ya miaka 40. Aliitawala Libya kidikteta. Pamoja na utajiri mkubwa wa mafuta wa nchi hiyo, utawala wa Gaddafi uliminya uhuru wa fikra kwa watu wake. Kamwe Gaddafi hakuvumilia fikra za kipinzani.


Mwanzoni kabisa mwa harakati za kumwondoa Gaddafi madarakani , kuna kijana aliyepata kutamka haya;  Tunachotaka ni kuishi maisha ya kawaida. Kuwa na uhuru wa mawazo kama vijana wengine duniani. Alitamka kijana yule wa KiLibya kwa mwanahabari wa Kimagharibi.


Na hakika hicho ndicho kikubwa kilichokosekana chini ya utawala wa Gaddafi. Na siku zote, mwanadamu hata umpe nini, lakini ukimnyima uhuru wa kufikiri na kuchagua, basi, atajisikia mtumwa. Hatofurahi.


Na kwa Gaddafi, si tu aliitawala Libya kwa muda mrefu, lakini bado alikuwa na ndoto, kuwa akitoka madarakani , basi, familia yake iendelee kutawala. Na umma ukimchoka mtawala au chama cha siasa, basi, utaishi kwa matumaini, kuwa siku moja itafika, kuwa umma utaondokana nae, au kuondokana nacho, kama ni chama cha siasa. Ndio maana ya furaha kubwa ya wenye kutimiza ndoto zao za kujikomboa.


Ndio, kiongozi wa nchi haui watu wake, Moummar Gaddafi wa Libya alifanya hivyo. Aliwaua watu wake, tena mchana wa jua kali, na bado alisimama hadharani, akidai kuwa ni kiongozi wa WaLibya. Gaddafi hakuwa na aibu.


Hatukatai, kuwa Gaddafi alifanya mazuri kwa WaLibya, LAKINI, kosa kubwa kabisa alilofanya Gaddafi kwa WaLibya ni KUWAKANDAMIZA watu wake. Ndio, kuwanyima UHURU. Gaddafi aliwageuza WaLibya kama ngombe kwenye zizi. Waliotoa sauti kumpinga aliwakamata na kuwachinja, kimyakimya. Gadaffi aliifanya Libya kuwa ni mali ya Gaddafi na familia yake.




Ndugu zangu,



Gaddafi alipata kusimama hadharani na kuwaambia WaLibya waendelee kuimba na kucheza! Akatamka;  WaLibya wote wananipenda! Hakika, Gaddafi alikuwa amepoteza mwelekeo na mguso wa hali halisi. Alipitisha viwango vyote vya ulevi wa madaraka. Wakati mwingine Gaddafi alionekana kama mwehu fulani aliyeshika bunduki na kupita mitaani. Na kwa kuhofia maisha yao, kuna vijana wengi wasomi wa Libya walilazimika kuikimbia nchi yao wanayoipenda. Walikwenda kuishi uhamishoni.


Tunajifunza nini?

Kwamba Afrika bado ina viongozi wengi, ambao, hata hii leo, wameingiwa hofu kwa kile kilichomtokea mwenzao Gaddafi. Hofu hiyo ina tafsiri nyingi; moja kuu ni ukweli, kuwa kuna viongozi Afrika wanaofanana fanana na Gaddafi. Kwamba nao hawapendi na hawaamini katika demokrasia na uhuru wa watu kutoa mawazo yao, hata yenye kushutumu Serikali.


Hawapendi uwepo wa vyama vingi na dhana ya kugawana madaraka. Hawapendi uwepo wa chaguzi huru na za haki. Hawapendi Katiba ambazo, mbali ya mambo mengine, zinampunguzia madaraka Rais. Kwao, kumpunguzia Rais madaraka ni sawa na kumpunguzia nguvu mtawala. Kwao ni jambo lisilowezekana.

Na Afrika bado ina watawala ambao watafanya kila hila kuhakikisha chaguzi za kisiasa haziendeshwi na tume huru za uchaguzi, bali, zitaendeshwa kutoka Ikulu zao. Na watawala hawa wa Afrika, kama kuna wenye kuandamana mitaani kuwapinga, basi, nao kama alivyofanya Gaddafi, hawatasita kutumia nguvu za kijeshi kuzima maandamano ya wananchi, ikibidi kuwaua wananchi wao. Ndio, Watatafuta visingizio vya kuwatwanga risasi watu wao ili kuwatishia wengine.


Na hakika, kinachotokea Afrika ni hiki; kwanza, mtawala atawaita waandamanaji  kuku na majina mengineyo. Kisha ataamrisha vikosi vyake vitumie risasi za moto kuwadhibiti  kuku waandamanaji. Si tunajua, kuwa Afrika kuku hachimbiwi kaburi.


Viongozi Afrika watambue sasa, kuwa Afrika kuna kimbunga kimelipuka. Ni kimbunga kinachosambaa. Kimeanzia Tunisia, kikaenda Misri na kimetua Libya. Kinasambaa. Ni kimbunga cha mabadiliko. Waafrika wengi wanaokandamizwa na watawala au vyama tawala katika nchi zao, leo wana kiu kubwa ya kujikomboa.


Na kiongozi mzuri hujitambua na kutambua wakati unaomzunguka. Huwa na uwezo wa kusoma alama za nyakati. Kiongozi makini, mwenye busara na mapenzi ya dhati kwa nchi yake hatosubirii watu wake wafikie ukomo wa uvumilivu ili afanye mabadiliko hitajika na yenye kukidhi matakwa ya wakati husika.


Nimepata kuandika, kuwa katika nchi, mabadiliko ya amani yanawezekana, lakini, kwa anayejaribu kuyazuia, atambue, kuwa mabadiliko yenye vurugu hayaepukiki.

Waafrika wameamka usingizini. Wameshatambua, kuwa hakuna risasi au kombora la mtawala litakaloweza kushinda nguvu ya umma uliodhamiria kuleta mabadiliko. Yametokea Tunisia, Misri, Libya. Yanaweza kutokea popote pale Afrika.
Busara ni kuenenda na wakati uliobadilika. Nahitimisha.
Maggid,
Dar es Salaam.
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo


( Makala haya yamechapwa kwenye gazeti la Mwananci, leo Jumapili)
I wish kwa mtizamo huu ulioutumia kuisema Afrika ungeandika version nyingine kuisema Tanzania! Tatizo waandishi kama wewe hamko aggressive moja kwa moja kwenye matatizo yetu ya msingi.najua ukiandika version nyingine kwaajili ya Tanzania kwa hoja hizi hizi lazima utafanya edit ya nguvu na kupunguza ukali wa maneno mfano chaguzi kuendeshwa kutokea ikulu!!! Ila kudos bro! kwa Afrika umeandika vizuri sana.
 
makala nzuri bwana maggij ila inabidi urudi upande wa pili wa makala na kuandika makala juu ya nchi yetu..............au unaogopa??????????
 
Nilifikifiri watu wameamka lakini nahofu kuwa Waafrika uafrika wetu utatumaliza. Kuna thread zingine mbili zinahusudu kweli Ghadafi na utawala wake wa kidikteta.
Eti Ghadafi anaitwa mzalendo. Mtu anayeuwa raia wake na kutawala kiimla ni mzalendo?
Kama vile Afrika ilivopata uhuru kabla ya wakati wake hivohivo imepata demokrasi kabla ya wakati wake. Wanaimba tu demokrasi wakati haki na utu habipo hata kwenye nywele zao.
 
Uchambuzi mzuri kaka Maggid, Handika na nyingine inayohusu Tanzania ili C.C.M wapate kujifunza.

Nchi za kusini mwa jangwa la sahara lina wanaichi weusi!! Msisahau wesuiz tangu mwanzo hawana guts kama za weupe na na hasa WAARABU ndiyo maana ukiziona nchi kama tunisia, Misri , Libya maisha ya wanchi wao na miundo mbinu za miji yao huwezi linganisha na nchi kama tanzania Uganda, Zimbabwe nk, Pia uchumi wa nnchi zao mali asili zao bado zinanufaisha nchi zaidi ukilinganisha na mali asili za nchi za kusini ambazo zinafanufaisha viongozi zaidi kuliko nchi miondo mbinu na maisha MABOVU LAINI WENYE RANGI NYEUSI WAMETULIA NA WATATULIA SIKU ZOTE HATA KAMA WAKIENDELEA KUUWANA NA POLISO KILA MARA KAMA TUNAVYOSHUHUDIA TANZANIA!!


NINACHSEMA NI KUWA VIONGOZI WA KUSINI ENDELEENI KUTESA TU NA KUANDAA VIJANA WENU KATIKA VYAMA ILI WATUTAWALALE MILELEE!! MSIWE NA WASI WASI TWNA WANACHI WENYE RANGI NYEUSI WALIOKUBALI KILAINI KUWA WATUMWA TOKA ENZI HIZO!!
 
Maggid nakubaliana na wewe. Hata hivyo inashangaza kusikia watu ambao siku zote wamekua wanapiga kelele kuhusu udikteta wa viongozi wa Kiafrika,leo wanamwita Gaddafi shujaa na mzalendo.
 
Tathmini nzuri sana Maggid. Bado tunao viongozi wengi sana Afrika na hata hapa kwetu Tanzania ambao hawataki kuelewa ukweli huo. Huwezi kumnyima mwanadamu uhuru wa kufikiri na kutoa maoni yake, na bado ukakaa na kujisifu kuwa unapendwa. Viongozi wa Afrika sasa ni wakati wa kuamka, ya kuwa siku za kumkandamiza mwafrika zimekwisha. Kuna waliodiriki hata hapa kwetu kutamka bila aibu wala woga ya kuwa Tanzania ni ya 'chama chao'. Huo ni ufinyu wa mawazo ambao haupaswi kukubalika mahali popote. Wakumbuke ya kuwa Afrika au Tanzania ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo hata baada ya wao kuondoka. Sote tunapita.

Ni kutokana na kukataa kwao kuukubali ukweli huo, ndipo tunapoona sasa wakitamka kwa jazba sana hadharani na kulaani yaliyotokea Libya. Hakuna jipya, nguvu ya umma imeongea. Ghadaffi likataa kuondoka kwa amani, ameondolewa kwa nguvu. Na wale wote wanaofikiri Tanzania ni nchi ya kisultani, ya kuandaa warithi wa uongozi kutoka kwenye familia 'zilizotukuka' wajue hawatafanikiwa. Ipo siku wananchi watazungumza.
 
Na hakika, kinachotokea Afrika ni hiki; kwanza, mtawala atawaita waandamanaji ‘ kuku’ na majina mengineyo. Kisha ataamrisha vikosi vyake vitumie risasi za moto kuwadhibiti ‘ kuku’ waandamanaji. Si tunajua, kuwa Afrika kuku hachimbiwi kaburi.
Sisi ni mbayuwayu!
 
makala nzuri bwana maggij ila inabidi urudi upande wa pili wa makala na kuandika makala juu ya nchi yetu..............au unaogopa??????????
Amesema viongozi wengi hawapendi katiba zinazompunguzia nguvu Raisi na kuruhusu uwepo wa tume huru za uchaguzi haya naamini ameyaona hata nchini Tanzania ambayo ulitaka aitaje.
 
Ninasikia Comdare Kagame wa Rwanda wananchi wanamuogopaKULIKO MUNGU JAPO ANAIJENGA NCHI KWA KASI ILA UHURU NI ALMOST ZERO WANANCHI NI WAOGA MNO, NI VIZURI ATOE UHURU na ajifunze kwa gadafi kuwa wanacni hawataki tu nchi ijengwe bali pia wanataka uhuru!!
 
Ndugu Maggid asante kwa tafsiri yako sahihi, fupi na fasaha. Umenipunguzia pressure kupanda na kushuka niliyokuwa nayo. Kila nilipokuwa ninasoma maoni ya wanaJF waliowengi hapa na kuona wanadai eti Kanali Gaddafi alikuwa "mzalendo, mtetezi wa raslimali za Afrika, amewapa wananchi wake nyumba bure pamoja na pesa za kuolea!", nk nilizidi kupata mshtuko mkubwa kwamba kama huo ndio mtazamo wa wasomi wa Tanzania, basi bado tunayo safari ndefu ya kujikomboa kutoka mikononi mwa mafisadi.
 
Kuna mfungwa mmoja nilikuwa nikimfaidi sana humu JF niliwasiliana naye na akanieleza kitu cha ajabu kidogo kuhusu kifo cha Gadafi, naomba nim-quote

" haya yote sept 11, Iraq, Tunisia, Misri, Osama, Gadafi n.k ni upande A wa New World Order, subiri wamalizie side A, kisha watakapogeuzia side B mtaelewa kinachoendelea, it will be too too late, especially for Tanzanians"

Nimeanza kuelewa alichoniambia mfungwa huyu wa gereza la JF.
 
I wish kwa mtizamo huu ulioutumia kuisema Afrika ungeandika version nyingine kuisema Tanzania! Tatizo waandishi kama wewe hamko aggressive moja kwa moja kwenye matatizo yetu ya msingi.najua ukiandika version nyingine kwaajili ya Tanzania kwa hoja hizi hizi lazima utafanya edit ya nguvu na kupunguza ukali wa maneno mfano chaguzi kuendeshwa kutokea ikulu!!! Ila kudos bro! kwa Afrika umeandika vizuri sana.
Na pia asingetaja "mabayu wayu" kama alivyotaja "kuku"
Wakiwa wanaitetea serikali ama mafisadi huwa wanaonekana kama wamechanganyikiwa hivi.Ila wakiongea ukweli basi hadi unafurahi.
 
Back
Top Bottom