Nilifurahi na kuwapongeza sana traffic police kwa kuamua kukaa eneo hilo.Yaani hiyo sehemu waenda kwa miguu wakitaka kuvuka barabara lazima wakimbie kama wezi! kuna Zebra,mabango makubwa ya kuwaambia madereva kuhusu kupunguza mwendo lakini wapi! binafsi hujisikia vibaya sana nikiwa naendesha nikikaribia Zebra halafu mwenda kwa miguu anavuka barabara kwa kukimbia. Madereva wa Tanzania tustaarabike,kwa nini nchi hii ina matuta ya barabarani mengi kuliko nchi yeyote ile Afrika Mashariki na Kati?