Chillipo
Member
- Mar 27, 2012
- 37
- 6
Katika hatua nyingine, Shahidi wa 14 wa upande wa wadaiwa katika kesi ya Uchaguzi Jimbo la Segerea, Samuel Bubegwa amekiri mahakamani kuwa matokeo yaliyompa ushindi Mbunge wa jimbo hilo, Dk Makongoro Mahanga wa CCM, yalitangazwa bila kura zenye migogoro kutatuliwa.
Bubegwa ambaye ni Mkuu wa Idara ya Usafishaji wa Manispaa ya Ilala na ambaye pia alikuwa Msimamizi Msaidizi Ngazi ya Jimbo hilo (ARO), alisema hayo jana alipohojiwa na na Wakili wa upande wa madai, Peter Kibatala.
Kesi hiyo namba 98 ya 2011 inasikilizwa na Jaji Profesa Ibrahim Juma na ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea nafasi hiyo kupitia Chadema, Fred akipinga matokeo yaliyompa ushindi Dk Mahanga, akidai kuwa sheria na taribu za uchaguzi zilikiukwa.
Dk Mahanga anatetewa na Mawakili Jerome Msemwa na Aliko Mwanamanenge na washtakiwa wengine, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala wakitetewa na Mawakili wa Serikali , David Kakwaya na Seith Mkemwa.
Akiongozwa na Wakili Mkemwa, shahidi huyo alidai kuwa walipokea fomu za matokeo ya ubunge kutoka katika vituo vyote 749 na kwamba baada ya kufanya uhakiki, hawakuona kura zenye migogoro.
Alidai kuwa baada ya uhakiki walianza kujumlisha matokeo kwa kusoma matokeo ya kila kituo kwa kila mgombea kuanzia saa nne usiku na kumaliza saa nane.
"Baada ya kumaliza kujumlisha tulimwita msimamizi (wa uchaguzi wa jimbo) ambaye alifika na kusaini fomu za matokeo na kisha akaenda kutangaza matokeo," alidai shahidi huyo.
Alisema wakati wote wa mchakato huo tangu kuanza majumuisho hadi kutangazwa matokeo, Mpendazoe hakuwepo wala wakala wake na badala yake walikuwapo mawakala wawili tu wa CCM na CUF pamoja na Dk Mahanga.
Akihojiwa na Wakili Kibatala ambaye alimuonyesha baadhi ya Fomu namba 21B za matokeo ya kura za ubunge kutoka vituoni alikiri kuwepo kwa kura zenye migogoro na kudai kuwa hajui kura hizo zilikopotelea na kukiri kuwa majumuisho ya kura ambazo Dk Makongoro alitangazwa mshindi, yalifanyika bila kura zenye migogoro kutatuliwa.
Lakini wakati akihojiwa na Mawakili Mwamanenge na Kakwaya, shahidi huyo alidai kuwa hakukuwa na kura zenye migogoro kwa kuwa hawakukabidhiwa kutoka vituoni na kwamba kiutaratibu, kura hizo hujazwa kwenye fomu maalumu na kufungwa kwenye bahasha.
Source: Mwananchi newspaper
Bubegwa ambaye ni Mkuu wa Idara ya Usafishaji wa Manispaa ya Ilala na ambaye pia alikuwa Msimamizi Msaidizi Ngazi ya Jimbo hilo (ARO), alisema hayo jana alipohojiwa na na Wakili wa upande wa madai, Peter Kibatala.
Kesi hiyo namba 98 ya 2011 inasikilizwa na Jaji Profesa Ibrahim Juma na ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea nafasi hiyo kupitia Chadema, Fred akipinga matokeo yaliyompa ushindi Dk Mahanga, akidai kuwa sheria na taribu za uchaguzi zilikiukwa.
Dk Mahanga anatetewa na Mawakili Jerome Msemwa na Aliko Mwanamanenge na washtakiwa wengine, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala wakitetewa na Mawakili wa Serikali , David Kakwaya na Seith Mkemwa.
Akiongozwa na Wakili Mkemwa, shahidi huyo alidai kuwa walipokea fomu za matokeo ya ubunge kutoka katika vituo vyote 749 na kwamba baada ya kufanya uhakiki, hawakuona kura zenye migogoro.
Alidai kuwa baada ya uhakiki walianza kujumlisha matokeo kwa kusoma matokeo ya kila kituo kwa kila mgombea kuanzia saa nne usiku na kumaliza saa nane.
"Baada ya kumaliza kujumlisha tulimwita msimamizi (wa uchaguzi wa jimbo) ambaye alifika na kusaini fomu za matokeo na kisha akaenda kutangaza matokeo," alidai shahidi huyo.
Alisema wakati wote wa mchakato huo tangu kuanza majumuisho hadi kutangazwa matokeo, Mpendazoe hakuwepo wala wakala wake na badala yake walikuwapo mawakala wawili tu wa CCM na CUF pamoja na Dk Mahanga.
Akihojiwa na Wakili Kibatala ambaye alimuonyesha baadhi ya Fomu namba 21B za matokeo ya kura za ubunge kutoka vituoni alikiri kuwepo kwa kura zenye migogoro na kudai kuwa hajui kura hizo zilikopotelea na kukiri kuwa majumuisho ya kura ambazo Dk Makongoro alitangazwa mshindi, yalifanyika bila kura zenye migogoro kutatuliwa.
Lakini wakati akihojiwa na Mawakili Mwamanenge na Kakwaya, shahidi huyo alidai kuwa hakukuwa na kura zenye migogoro kwa kuwa hawakukabidhiwa kutoka vituoni na kwamba kiutaratibu, kura hizo hujazwa kwenye fomu maalumu na kufungwa kwenye bahasha.
Source: Mwananchi newspaper