Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Kumekuwa na mazowea kwa baadhi ya viongozi wakitumia andiko la Waraka wa Mtume Paulo kwa warumi, kama njia ya kuwafanya watu wasiikosoe serikali wala wasiipinge hata pale inapokosea.
Watu hao hutumia andiko ilo la Paulo hukunukuu baadhi ya maandishi yake yaliopo kwenye kitabu cha Warumi(waroma ;13:1-6) kwa ufupi kitabu hicho kinaeleza kuwa
Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo imeamriwa na Mungu.
Kitabu kinasistiza zaidi kuwa,Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.(mwisho wa kunukuu).
Lakini ni kweli kila mamlaka hutoka kwa Mungu?, maana kama kila mamlaka hutoka kwa Mungu na hivyo hatupaswi kuipinga mamlaka yoyote basi bila shaka kwa andiko hili wakina Nyerere, King Sobhuza wa Swaziland, King Mashoeshoe wa Lethoto na akina Ahmed Sekoutoure walifanya makosa makubwa kuutoa ukoloni.
Maana ukoloni nao ulikuwa ni utawala(mamlaka) hivyo kwa andiko hili bila shaka wapigania Uhuru walifanya kosa kuupinga.
Ni kweli kwamba kuna baadhi ya mambo watawala humwakilisha Mungu matharani tawala nyingi upinga ubakaji, matendo ya wizi(ufisadi na rushwa), uzinzi, uonevu, uuaji n.k lakini inakuwaje pale serikali inapogeuka na kuanza kutenda mambo hayohayo?
Tunajua fika kwamba Idd Amin alikuwa Muuaji na mtesaji ina maana kwa andiko hilo ilibidi watu wa Uganda wamvumilie Idd Amin?
Na kama kila mamlaka hutoka kwa bwana ina maana tuamini kuwa ule uvamizi wa Idd Amini kule Kagera ulikuwa na baraka kutoka kwa Mungu?
Mauaji ya waisrael 6mil yaliyotendwa na utawala wa serikali ya Hitler uko Ujerumani kwa andiko hili inamaana yale mauaji yalipewa baraka na Mungu kiasi kwamba ilibidi watu na jumuhia za kimataifa zimkalie kimya bila kumpinga wala kumkosoa (bila shaka sivyo)
Kumbe kuna siri gani juu ya hili andiko ? Mtume Petro anatujibu juu ya andiko hilo la Paulo , jibu hili na liwe dira hasa kwa wale watu wenyetabia za kukalili vifungu kama njia ya kuwatendea wengine uovu.
2 Petro 3:15-16 anasema;
Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa;
16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa(huyapotosha), kama vile wayapotoavyo maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.
Hapa mtume Paulo anatueleza kuwa watu wasio na elimu( juu ya mambo ya kiroho) wasio imara( katika imani) huyapotosha maandiko hayo kwa makosa yao wenyewe( mtu anafanya kosa ananukuu andiko ili kuhalisha kosa kumbe ilo andiko msingi wake huitaji imani kuliewa na siyo kulisomasoma tu kama wafanyavyo viongozi.
Watu hao hutumia andiko ilo la Paulo hukunukuu baadhi ya maandishi yake yaliopo kwenye kitabu cha Warumi(waroma ;13:1-6) kwa ufupi kitabu hicho kinaeleza kuwa
Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo imeamriwa na Mungu.
Kitabu kinasistiza zaidi kuwa,Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.(mwisho wa kunukuu).
Lakini ni kweli kila mamlaka hutoka kwa Mungu?, maana kama kila mamlaka hutoka kwa Mungu na hivyo hatupaswi kuipinga mamlaka yoyote basi bila shaka kwa andiko hili wakina Nyerere, King Sobhuza wa Swaziland, King Mashoeshoe wa Lethoto na akina Ahmed Sekoutoure walifanya makosa makubwa kuutoa ukoloni.
Maana ukoloni nao ulikuwa ni utawala(mamlaka) hivyo kwa andiko hili bila shaka wapigania Uhuru walifanya kosa kuupinga.
Ni kweli kwamba kuna baadhi ya mambo watawala humwakilisha Mungu matharani tawala nyingi upinga ubakaji, matendo ya wizi(ufisadi na rushwa), uzinzi, uonevu, uuaji n.k lakini inakuwaje pale serikali inapogeuka na kuanza kutenda mambo hayohayo?
Tunajua fika kwamba Idd Amin alikuwa Muuaji na mtesaji ina maana kwa andiko hilo ilibidi watu wa Uganda wamvumilie Idd Amin?
Na kama kila mamlaka hutoka kwa bwana ina maana tuamini kuwa ule uvamizi wa Idd Amini kule Kagera ulikuwa na baraka kutoka kwa Mungu?
Mauaji ya waisrael 6mil yaliyotendwa na utawala wa serikali ya Hitler uko Ujerumani kwa andiko hili inamaana yale mauaji yalipewa baraka na Mungu kiasi kwamba ilibidi watu na jumuhia za kimataifa zimkalie kimya bila kumpinga wala kumkosoa (bila shaka sivyo)
Kumbe kuna siri gani juu ya hili andiko ? Mtume Petro anatujibu juu ya andiko hilo la Paulo , jibu hili na liwe dira hasa kwa wale watu wenyetabia za kukalili vifungu kama njia ya kuwatendea wengine uovu.
2 Petro 3:15-16 anasema;
Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa;
16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa(huyapotosha), kama vile wayapotoavyo maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.
Hapa mtume Paulo anatueleza kuwa watu wasio na elimu( juu ya mambo ya kiroho) wasio imara( katika imani) huyapotosha maandiko hayo kwa makosa yao wenyewe( mtu anafanya kosa ananukuu andiko ili kuhalisha kosa kumbe ilo andiko msingi wake huitaji imani kuliewa na siyo kulisomasoma tu kama wafanyavyo viongozi.