afsa
JF-Expert Member
- Dec 6, 2012
- 1,983
- 1,574
Zitto Zubeir kabwe
Mwongozo wa namna ya kuishi na Magufuli kwa wanasiasa, wastaafu na wafanyabishara

Moja
Usisema CCM bali sema CCM ya Magufuli. Wala usijaribu kusema Serikali ya CCM bali Serikali ya Magufuli. Katika fikra zake, yeye ni zaidi ya Chama kilichomuweka madarakani. Yeye ndiye Chama na yeye ndiye Katiba ya Chama na vile vile yeye ndiye vikao vyote vya chama na mwenye pumzi ya chama na si wanachama wala yeyote yule.
Mbili
Mpigie simu ama mtumie ujumbe mfupi wa maandishi ama omba kumtembelea mara kwa mara. Madaktari kutoka China ambao walimfanyia vipimo wanaeleza kuwa mbali na magonjwa mengine ana ugonjwa uitwao “Bipolar”. Baadhi ya dalili za ugonjwa huo ni kutojiamini na kuhisi kila wakati kuna mtu anataka kukutendea jambo baya, kukosa usingizi, kuwa na mahusiano mengi ya kimapenzi, kuwa na wasiwasi na vitu ambavyo wakati mwingine havipo, na kadhalika.
Tatu
Ukipata wasaa wa kuonana naye ana kwa ana, msifie, usimwambie mabaya yake bali mazuri peke yake na mshauri kuongeza bidii hata kama anakwenda katika mwelekeo hovyo. Mpe habari nzuri tu, kama hazipo zitengeneze. Habari mbaya humpa hisia tofauti, moja hudhani kuwa wewe ni mhusika kusababisha zitokee lakini mbili hudhani kwamba kumwambia kwako kunaonyesha furaha yako kwa yeye au watu wake kufikwa na jambo baya na huenda moyoni ni dua yako kwamba mabaya yamtokee.
Nne
Tafuta chombo chochote cha habari, msifie hadharani.
Tano
Mpe jina la masikini mzalendo hata kama anaongoza kwa ufisadi kuliko viongozi wote waliomtangulia. Akishirikiana na mpwa wake ambaye amempa Ukatibu Mkuu Hazina ya nchi tayari wamenyonya shilingi trilioni 1.5 huku kila ndege iliyonunuliwa wakiwa wamepata discount kubwa na kuiweka mifukoni. Hayo ni machache kati ya mengi.
Sita
Mpe jina la mwadilifu hata kama ndoa yake imevunjika siku nyingi huku akiwa amezaa na wanawake lukuki nchini na kulala na visichana vyenye umri wa binti yake huku akivizawadiwa vyeo na fedha.
Saba
Mpe jina la mcha Mungu hata kama amekuwa na vikao vya siri kutaka kufanyika kwa mauaji ya Askofu Shoo na wazi wazi kutaka kufungia makanisa na taasisi za kijamii kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani jambo ambalo kijana Mwigulu Nchemba aligoma kulifanya na kuishia kuondolewa katika nafasi hiyo.
Nane
Usikae kimya. Ukikaa kimya anahisi unapanga jambo kumdhuru (dalili ya ugonjwa wa Bipolar). Ukikaa kimya inamsumbua kichwa na nafsi na atatafuta namna zote uzungumze hasa ambazo ni haramu. Mfano wa siku za karibuni ni Abdulrahman Kinana na Bernard Membe ambao wametajwa kuwa watu hatari na Mhariri wa Gazeti la Tanzanite. Wawili hao ni magwiji wa siasa ndani na nje ya Tanzania na ukimya wao unamfanya aweweseke. Ikumbukwe kuwa gazeti la Tanzanite linalipwa pesa ya uendeshaji takribani shilingi milioni 400 kwa mwezi na Idara ya Usalama wa Taifa chini ya Edward Nyaulingo ambaye ni Mkurugenzi wa Oparesheni. Malipo mengine hupewa na Air Tanzania ambayo hutangaza kupitia gazeti hilo. Hii inamaanisha kuwa kinyume na maadili ya Usalama wa Taifa, Nyaulingo na kitengo chake wanatumika na Magufuli kulazimisha waliokaa kimya kuongea ili nafsi yake ipate kutulia pale atakapojua wanachowaza. Hili likishindikana zitaundwa tuhuma dhidi ya wakaa kimya au ndugu au marafiki au watu wa karibu ilimradi tu lengo litimie.
Mwongozo wa namna ya kuishi na Magufuli kwa wanasiasa, wastaafu na wafanyabishara

Moja
Usisema CCM bali sema CCM ya Magufuli. Wala usijaribu kusema Serikali ya CCM bali Serikali ya Magufuli. Katika fikra zake, yeye ni zaidi ya Chama kilichomuweka madarakani. Yeye ndiye Chama na yeye ndiye Katiba ya Chama na vile vile yeye ndiye vikao vyote vya chama na mwenye pumzi ya chama na si wanachama wala yeyote yule.
Mbili
Mpigie simu ama mtumie ujumbe mfupi wa maandishi ama omba kumtembelea mara kwa mara. Madaktari kutoka China ambao walimfanyia vipimo wanaeleza kuwa mbali na magonjwa mengine ana ugonjwa uitwao “Bipolar”. Baadhi ya dalili za ugonjwa huo ni kutojiamini na kuhisi kila wakati kuna mtu anataka kukutendea jambo baya, kukosa usingizi, kuwa na mahusiano mengi ya kimapenzi, kuwa na wasiwasi na vitu ambavyo wakati mwingine havipo, na kadhalika.
Tatu
Ukipata wasaa wa kuonana naye ana kwa ana, msifie, usimwambie mabaya yake bali mazuri peke yake na mshauri kuongeza bidii hata kama anakwenda katika mwelekeo hovyo. Mpe habari nzuri tu, kama hazipo zitengeneze. Habari mbaya humpa hisia tofauti, moja hudhani kuwa wewe ni mhusika kusababisha zitokee lakini mbili hudhani kwamba kumwambia kwako kunaonyesha furaha yako kwa yeye au watu wake kufikwa na jambo baya na huenda moyoni ni dua yako kwamba mabaya yamtokee.
Nne
Tafuta chombo chochote cha habari, msifie hadharani.
Tano
Mpe jina la masikini mzalendo hata kama anaongoza kwa ufisadi kuliko viongozi wote waliomtangulia. Akishirikiana na mpwa wake ambaye amempa Ukatibu Mkuu Hazina ya nchi tayari wamenyonya shilingi trilioni 1.5 huku kila ndege iliyonunuliwa wakiwa wamepata discount kubwa na kuiweka mifukoni. Hayo ni machache kati ya mengi.
Sita
Mpe jina la mwadilifu hata kama ndoa yake imevunjika siku nyingi huku akiwa amezaa na wanawake lukuki nchini na kulala na visichana vyenye umri wa binti yake huku akivizawadiwa vyeo na fedha.
Saba
Mpe jina la mcha Mungu hata kama amekuwa na vikao vya siri kutaka kufanyika kwa mauaji ya Askofu Shoo na wazi wazi kutaka kufungia makanisa na taasisi za kijamii kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani jambo ambalo kijana Mwigulu Nchemba aligoma kulifanya na kuishia kuondolewa katika nafasi hiyo.
Nane
Usikae kimya. Ukikaa kimya anahisi unapanga jambo kumdhuru (dalili ya ugonjwa wa Bipolar). Ukikaa kimya inamsumbua kichwa na nafsi na atatafuta namna zote uzungumze hasa ambazo ni haramu. Mfano wa siku za karibuni ni Abdulrahman Kinana na Bernard Membe ambao wametajwa kuwa watu hatari na Mhariri wa Gazeti la Tanzanite. Wawili hao ni magwiji wa siasa ndani na nje ya Tanzania na ukimya wao unamfanya aweweseke. Ikumbukwe kuwa gazeti la Tanzanite linalipwa pesa ya uendeshaji takribani shilingi milioni 400 kwa mwezi na Idara ya Usalama wa Taifa chini ya Edward Nyaulingo ambaye ni Mkurugenzi wa Oparesheni. Malipo mengine hupewa na Air Tanzania ambayo hutangaza kupitia gazeti hilo. Hii inamaanisha kuwa kinyume na maadili ya Usalama wa Taifa, Nyaulingo na kitengo chake wanatumika na Magufuli kulazimisha waliokaa kimya kuongea ili nafsi yake ipate kutulia pale atakapojua wanachowaza. Hili likishindikana zitaundwa tuhuma dhidi ya wakaa kimya au ndugu au marafiki au watu wa karibu ilimradi tu lengo litimie.