uvugizi
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 1,350
- 1,098
hapa mimi naona CCM inaogopa kuyumba kwa chama, kwani hao mabandidu(wauza unga ) , principle kubwa uwe mfadhili wa chama, na mfurukutwa wa chama basi wewe utauza unga mpaka basi!!!, na vigogo wa serikali utawapa maelekezo .sijasikia watu wa upinzani hata mmoja hasa viongozi wanapendwa na hawa watu wa madawa ya kulevya , ni kwamba matajiri wa hela chafu wanachukia chadema kuliko maelezo. na hili la CCM wasipoliangalia litawagharimu sana ukiwa mfadhili mzuri wa CCM basi karibu kila kitu unapitia kwa mwenyekiti wa mkoa unakuta mambo yako yanaenda vizuri kama tenda n.k, basi na wauza unga wanapita humo humo, na maunga yao . yaani mwenyekiti wa ccm mkoa anakauli kushinda hata mkuu wa mkoa hili nalo janga , halafu wana njaa kweli kweli kwa nini wauza unga wasione nchi yao wanaishika wao imekuwa COLOMBIA!!!!!. yaani kumbe mwalimu aliona mbali sana ,huyu mtu mmoja tu anawazungusha akili si wamtaje tu na kamtandao kake sisi tunajeshi , vita vya haya madawa tuvianzishe na tuvimalize. yaani mpaka namkumbuka mrema kwa utendaji wake , naona wangepewa siku 7 tu , na ikibidi huko hong kong wafanye mpango kuwahoji washitakiwa na waliofungwa huko watusaidie jamani hili. tukifanya uzembe halitaisha na harakati za mwakyembe hazitaonekana .