Anayejua maandalizi ya kuelekea matumizi kamili ya gesi majumbani

Nsibhwene

JF-Expert Member
Dec 8, 2016
293
217
Hivi majuzi Prof. Maghembe, Waziri wa maliasili na Utalii alitoa tamko kuhusu ukomo wa usafirishaji wa mkaa unaotokana na miti. Katazo hilo lilitaka ifikapo julai mwaka 2017 haitaruhusiwa kusafirisha mkaa kutoka wilaya moja kwenda nyingine. Julai ndio hiyo inakaribia, Je maandalizi yakoje wana jamvi, maana tusijekuona kama ni agizo ni jipya hasa litakapoanza kutekelezwa.
 
Maandalizi? Unataka watu waende UDSM kusomea Kupika kwa Kutumia Gas? Kwani wanaotumia Gas kwa sasa waliandaliwa na nani?
 
Maandalizi? Unataka watu waende UDSM kusomea Kupika kwa Kutumia Gas? Kwani wanaotumia Gas kwa sasa waliandaliwa na nani?
Tuliahidiwa Gesi itaingizwa majumbani kama maji ya Dawasco yaani kama wanavyotumia Gesi nchi za ulaya
 
kuna nchi nyingi tena masikini kama Tanzania wanatumia Gesi kupika lakini sie tumekomalia makaa. Ukiuliza mtungi wa geni utakimbia kama kichaa, bei haigusiki. Haiwezekani Serikali ikazuia mkaa wakati hawajaweka mazingiza mazuri ya matumizi ya gesi. Bei lazima ipungue, tupate mashirika yenye uzoefu kwenye hii biashara lasivyo utasikia mitungi inaripuka utasema tuko syria.
 
Back
Top Bottom